Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

Hon. Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Spika, niwapongeze Mawaziri wa Kilimo wote wawili.

Mheshimiwa Spika, ni kweli inawezekana Mkoa wa Dar es Salaam hatufanyi kilimo lakini naomba kuongelea Halmashauri ya Temeke.

Mheshimiwa Spika, sekta ya kilimo ndio msingi mkubwa wa kukuza kipato na chakula kwa familia na jamii. Jumla ya Kaya 6,118 zenye wakulima 11,270 wanajihusisha na kilimo cha mbogamboga kwenye hekta 6000. Karibu hekta 250 za mihogo na hekta 5,750 za matunda na mbogamboga na uchangiaji wa zaidi ya asilimia 75.

Mheshimiwa Spika, huduma za ugani zinafanyika kwa kutoa ushauri kwa wakulima kuhusu maghala na masoko na maeneo ya uwezeshaji Idara ya Kilimo ya Halmashauri ya Temeke.

Mheshimiwa Spika, tunawakaribisha kuja tuwekeze katika maeneo ili kuleta tija katika sekta ya kilimo. Pia kuwekeza kwenye kilimo cha umwagiliaji ambazo hazijaanza kwa Temeke, upatikanaji wa masoko ya mazao ya kilimo cha mihogo /matunda/mbogamboga yapo na viwanda vya kutengenezea bidhaa za mazao ya kilimo kama zao la muhogo/mbogamboga/na matunda.

Mheshimiwa Spika, nauga mkono hoja na kazi iendelee.