Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

Hon. Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Spika, nianze na suala la utafutaji wa masoko ya bidhaa za kilimo.

Mheshiiwa Spika, ushauri Serikali iangalie mahitaji ya ndani ya bidhaa au mazao ya kilimo, kisha ifanye zoning ya kuhakikisha hitaji hilo litashughulikiwa na wakulima wa kanda fulani. Mfano tunahitaji mafuta ya kupikia nchini, hivyo ianishwe mikoa ambayo itatakiwa kuchangia market share hiyo. Hii itasaidia Serikali, kuelekeza nguvu kubwa za uwekezaji hasa katika utafiti, mbegu bora, upatikanaji wa masoko, kuweka miundombinu bora, pia itavutia wawekezaji.

Pili, miji yetu pia ni masoko ya bidhaa za kilimo kama mbogamboga, iangaliwe miji ambayo mito inapita katikati yake, halafu ifanyiwe mkakati wa kilimo bora cha mbogamboga na ufugaji wa samaki wa kizimba, bila kuathiri mazingira. Mfano Mji wa Iringa unapitiwa na Mto Ruaha, Njombe, Mto Ruhuji na kadhalika.

Tatu, fedha za wafadhili katika kilimo ziwafikie walengwa ikiwa ni pamoja na za Serikali zilizowekezwa kwenye mabenki ya Kilimo.