Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

Hon. Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa nimpongeze Waziri wa Kilimo pamoja na timu yake kwa kazi nzuri na yenye tija wanayoifanya, na kwa hakika vipaombele vyote hivi vikifanyiwa kazi nchi yetu itakuwa imetimiza malengo yake ya asilimia 75.

Mheshimiwa Spika, nchi yetu ina asilimia 75 ambayo ni wakulima, lakini kinachoonekana wakulima hawa hawapati huduma kama inavyotakikana. Ushauri wangu kwa Serikali ijipange kuhakikisha inapeleka pembejeo za kutosha na kwa wakati, mfano nchi yetu ina mazao ya kibiashara zaidi ya sita ikiwemo kahawa; na kahawa hii inalimwa pia katika Milima ya Usambara ila cha kushangaza na kusikitisha zao hili la kahawa linakufa, hivi ninavyoandika Lushoto kahawa imekufa.

Mheshimiwa Spika, kwa mantiki hii naomba niishauri Serikali yangu tukufu iende ikafufue zao la kahawa katika Wilaya ya Lushoto kwani zao hili lilikuwa linainua sana uchumi wa Lushoto. Kwa hiyo, niendelee kuiomba Serikali iende kufufua zao hili la kahawa pamoja na kupeleka wataalam wa kutosha.

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Lushoto ni ya wakulima wa mbogamboga na matunda, na mazao haya ndio mazao tegemezi kwa Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto, lakini sijawahi kusikia wakulima hawa wanapelekewa pembejeo, lakini pamoja na hayo mazao ya wakulima hawa mengi yanaozea mashambani. Kwa hiyo, niiombe Serikali yangu iwapelekee wakulima hawa wa mbogamboga na matunda pembejeo pamoja na kuwatafutia masoko wakulima hawa.

Mheshimiwa Spika, pia Wilaya ya Lushoto ina milima na mabonde mengi, hivyo wakati wa msimu wa mvua kunakuwa na maporomoko makubwa ambayo yanaleta asali kwenye mashamba pamoja na kuharibu miundombinu ya barabara na kupelekea hasara kubwa kwa wakulima.

Mheshimiwa Spika, je, Serikali haioni kuwa ipo haja ya kujenga mabwawa kwa ajili ya kukinga maji hayo ili wakulima wetu hasa wa Wilaya ya Lushoto waweze kulima kilimo cha umwagiliaji kuliko ilivyo kuwa sasa ardhi yote yenye mbolea inasombwa na maporomoko yanayosababishwa na mvua?

Mheshimiwa Spika, naomba sana Serikali itenge pesa za kutosha ili iwajengee mabwawa wakulima wa Jimbo la Lushoto.

Mheshimiwa Spika, naunga hoja mkono kwa asilimia mia kwa mia.