Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

Hon. Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Spika, naomba nichangie kwa njia ya maandishi kwenye hoja iliyoko mbele yetu.

Mheshimiwa Spika, suala la kwanza kabisa naiomba Serikali ifikirie namna ya kurejesha export levy na ifanye kazi kwa malengo yaliyokusudiwa, asilimia 65 ni ya masuala ya korosho na asilimia 35 iende Serikalini.

Suala la pili ni kuhusu Bodi ya Korosho. Bodi hii haipo kwa muda mrefu kabisa, anaachwa Director General afanye mambo mengi wakati hata uwezo wa kufanya hayo mambo hawezi na badala yake ni kukuza migogoro kati ya watumishi na kujinufaisha zaidi, Director General wa korosho aondolewe, ameshindwa kusimamia tasnia, kazi ni maugomvi na wafanyakazi wenzake na wadau wa tasnia kwa sababu tu za kimaslahi.

Mheshimiwa Spika, pia programu za miche na pembejeo bure kwa wakulima zirudishwe ili kuweza kusadia maeneo mengine ambayo yanalima korosho.

Mheshimiwa Spika, bei ya gunia zipo juu sana hali inayomgharimu mkulima. Hata akichangiwa mnunuzi anapunguza bei ya mkulima, kwenye mjengeko wa bei, pale mnunuzi anapoongezewa gharama maana yake anakata pesa kwa mkulima.

Mheshimiwa Spika, ile sheria iliyofanyiwa marekebisho ni Sheria Na. 18 ya mwaka 2009 na kanuni zake za mwaka 2010. Kwa kubadili kifungu Na 17A ambacho kilikuwa kinaelekeza jinsi ya kukusanya export levy na kuigawa ambapo asilimia 65 ilikuwa inatakiwa ipelekwe kwa ajili ya maendeleo ya tasnia ya korosho na asilimia 35 ipelekwe kwenye Mfuko Mkuu wa Serikali. Baada ya sheria hiyo Na. 18 ya mwaka 2009 kufanyiwa marekebisho mwaka 2017 kwenye kifungu na 17A; ikaelekezwa kwamba fedha zote zipelekwe katika Mfuko Mkuu wa Serikali na tasnia ikiwa na mahitaji itaomba.

Mheshimiwa Spika, ukweli ni kwamba tangu fedha hizo zichukuliwe na Serikali tasnia imedorora, uzalishaji umeshuka kutoka tani 320,000 hadi tani 205,000 mnaweza kuona hasara ambayo Serikali imeisababishia industry ya korosho na imepelekea kukosa mapato kwa wakulima, wadau na Serikali yenyewe. Pia tangu hizo fedha kuzuiliwa Serikali imepeleka kiasi kisichozidi shilingi bilioni 15 kwa ajili ya maendeleo ya tasnia wakati madeni na mahitaji ya kuendeleza tasnia ni zaidi ya bilioni 100. Hivyo turejee kwenye sheria ile ya awali ambayo ilikuwa inapeleka export levy asilimia 65.

Mheshimiwa Spika, jambo lingine ni kwamba wakati sheria inabadilishwa tayari tasnia ya korosho iikuwa inadai zaidi ya shilingi bilioni 150. Hivyo ni vyema fedha hizo zipelekwe kwenye tasnia ya korosho kwa kuwa sheria ikitungwa hairudi nyuma, bali huenda mbele.

Mheshimiwa Spika, kumekuwa na maneno mengi kuhusu suala la unyaufu, na Serikali bado haijaweka wazi suala hili, kuna haja ya kujibu hoja kwamba je, kuna unyaufu ama laa, Serikali ifanye utafiti wa kutosha kwa sababu katika kila jambo linalotokea huwa linaharibu sana mjengeko wa bei.

Suala lingine ni kuhusu madeni ya wazalishaji wa mbegu ambazo zilisambazwa maeneo mbalimbali nchini, watu hawa hawajalipwa, wengine walikopa kwenye mabenki sasa wanafilisiwa, akina mama waliunda vikundi lakini bado hawajaweza kupata pesa na madeni yako wazi, bado kuna watoa huduma ambao wadai Serikali, kuna walio- supply magunia msimu wa mwaka juzi, nao walikopa.

Mheshimiwa Spika, hivi karibuni yamefanyika mabadiliko katika ngazi mbalimbali za uongozi kwenye vyama vikuu, kumekuwa na utaratibu wa kurithishana madeni, COASCO wakafanye ukaguzi hasa Chama Kikuu cha Ushirika cha Mtwara na Newala, vinginevyo madeni haya yanabaki kwa wakulima na hasara inakuwa kwao.

Mheshimiwa Spika, irekebishwe sheria pia inayowatambua wakulima wote kama wanachama, kwa sababu pesa zinazokusanywa kwenye faida inayopatikana kwenye mauzo wanakula viongozi, sawa na pesa za maendeleo zinazotokana na makusanyo, hazirudi kwa jamii.

Mheshimiwa Spika, matumizi mabaya ya fedha ya Bodi kutoka kwa DG wa Bodi ya Korosho, zaidi ya shilingi bilioni mbili Wizara ichukue hatua za kinidhamu, rejea ukaguzi wa COASCO.

Mheshimiwa Spika, nawasilisha kwako Taarifa ya matumizi ya Director General wa korosho Kutoka Ofisi ya Mkaguzi wa Ndani. Wizara ya Kilimo inatakiwa kufanya ukaguzi mara moja ili kuepuka hasara ambayo Serikali inaweza kuipata.

TAARIFA ZA MATUMIZI MABAYA YA OFISI KWA MKURUGENZI MKUU WA BODI YA KOROSHO TANZANIA NDUGU FRANCIS ALFRED KWA KIPINDI CHA MWAKA MMOJA

A: TAARIFA YA MALIPO YA POSHO YA MAKARIBISHO (ENTERTAINMENT ALLOWANCE) AMBAYO AMELIPWA MKURUGENZI MKUU WA BODI YA KOROSHO BILA MUONGOZO WOWOTE NA BILA KUFANYA MAREJESHO KWA KIPINDI CHA MWAKA SASA

Naleta kwako ushahidi wa malipo, na kwa taarifa zaidi ziko uko Bodi ya Korosho.

1. 4/9/2019 000461 Francis Alfred Mwakabumbe Entertainment Kikao Wizara ya Kilimo 500,000 840,000 200,000;

2. 26/8/2019 000444 Francis Alfred Mwakabumbe Entertainment Kikao Wizara ya Kilimo 500,000 840,000

3. 28/10/2019 000065 Francis Alfred Mwakabumbe Entertainment Mkutano wa Wadau wa Korosho Mkoa wa Pwani 500,000 240,000

4. 13/09/2019 000035 Francis Alfred Mwakabumbe Entertainment Kikao Wizara ya Kilimo 500,000 1,080,000

5. 3/12/2019 000216 Francis Alfred Mwakabumbe Entertainment Ziara Maeneo Mapya ya Uzalishaji- Dodoma,Tabora,Katavi,Songwe,Mbeya &Njombe 500,000 1,200,000

6. 31/12/2019 000249 Francis Alfred Mwakabumbe Entertainment Kushughulikia Masuala ya Msimu Rufiji 500,000 360,000

7. 7/1/2020 000262 Francis Alfred Mwakabumbe Entertainment Kikao na Wakuu wa Wilaya-Tunduru 500,000 120,000

8. 4/1/2020 000130 Dodoma City Square Restaurant Huduma ya Maji na Chakula Kikao na Mh. Waziri wa Kilimo 1,650,000

9. 6/2/2020 000140 Francis Alfred Mwakabumbe Entertainment Kikao na ANSAF -Dodoma 500,000 1,080,000

10. 24/02/2020 000162 Francis Alfred Mwakabumbe Entertainment Kikao Wizara ya Kilimo 500,000 1,200,000

11. 27/03/2020 000434 Francis Alfred Mwakabumbe Entertainment Kikao na Mkuu wa Mkoa Lindi 500,000 840,000

12. 1/11/2019 000072 Francis Alfred Mwakabumbe Entertainment Safari Dsm Kituo cha ITV 500,000 180,000

13. 5/11/2019 000075 Francis Alfred Mwakabumbe Entertainment Kikao Dsm - issue ya ACA 500,000 600,000

14. 14/112019 000090 Francis Alfred Mwakabumbe Entertainment Kikazi Kipindi TBC 500,000 360,000

15. 20/11/2019 000099 Francis Alfred Mwakabumbe Entertainment Kikao na Clouds 500,000 720,000 150,000

16. 9/1/2020 000272 Francis Alfred Mwakabumbe Entertainment Kushiriki Ziara ya Waziri Mkuu-Pwani 500,000 480,000

17. 20/01/2020 000295 Francis Alfred Mwakabumbe Entertainment Kikao cha Wizara ya Kilimo 500,000 1,200,000 300,000

Mheshimiwa Spika, taarifa hii nimeitoa kwenye mfumo wa Excel unaweza usieleweke sana, lakini kuna umuhimu wa kupeleka wakaguzi ili taarifa hii iwe vizuri. Jumla 8,000,000 11,340,000 650,000 1,650,000

Mheshimiwa Spika, hakuna muongozo wowote unaompa haki DG ya kulipwa posho ya entertainment, ni maagizo yake tu ya mdomo.

Mheshimiwa Spika, hajafanya marejesho mwaka umepita. Matumizi mabaya ya ofisi na madaraka na ufujaji wa fedha za umma.

Mheshimiwa Spika, issue ni matumizi mabaya ya ofisi kwa kuwa fungu hilo halikuwa kwenye bajeti.

Mheshimiwa Spika, DG ametumia bilioni 1.5 kutoka Mei, 2019 hadi Septemba, 2019 kinyume na bajeti iliyoombea fedha hizo Wizara ya Fedha kupitia Wizara ya Kilimo bila idhini ya mamlaka. (Bajeti iliyoombea fedha hizo imeambatishwa).

Mheshimiwa Spika, DG amefanya addendum ya pembejeo kwa msimu 2019/2020 na kampuni za BAJUTA International Ltd. sulphur tani 11,000 na kampuni ya TFC sulphur tani 8,000 bila idhini ya Kamati ya Zabuni (Tender Board). Ukiukaji wa Sheria ya Manunuzi ya Umma ya mwaka 2011 na kanuni zake za mwaka 2013 (addendum hizo zimeambatishwa kama vielelezo).

Mheshimiwa Spika, usimamizi mbovu wa mikopo ya pembejeo kwa wakulima hivyo kupelekea zaidi ya shilingi bilioni moja kutolipwa msimu 2019/2020. Fedha hizo zisipopatikana italazimu Serikali itafute fedha za kuwalipa wazabuni ambao waliikopesha CBT pembejeo ili iuze kwa wakulima kisha walipwe fedha.

Mheshimiwa Spika, matumizi mabaya ya ofisi, kwa mfano kutotumia muundo wa bodi uliopo katika kufanya kazi za ofisi mfano aweza kwenye idara akamtuma junior staff bila Mkuu wa Idara kuwa na taarifa hivyo kuleta migongano katika Idara na kazi kwa ujumla. Hiyo imetokea katika Kurugenzi ya Fedha, Idara ya Fedha, Kurugenzi ya Masoko, Kitengo cha Manunuzi na Idara ya Utumishi na Utawala.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha na naunga mkono hoja.