Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

Hon. Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Spika, kwanza niwapongeze Mheshimiwa Waziri, Naibu wake Makatibu Wakuu na timu yote ya Wizara.

Mheshimiwa Spika, hali ya ushirika katika Wilaya ya Nyasa si nzuri. Kuna malalamiko makubwa ya wakulima wa kahawa hasa AMCOS za Nambawala na Luhangalasi.

Mheshimiwa Spika, Bonde la Lituhi lina potential kubwa ya kilimo cha umwagiliaji na ndio eneo linalotegemewa zaidi kwa kilimo. Changamoto ni ukosefu wa miundombinu.

Mheshimiwa Spika, nashauri Serikali isaidie kutatua changamoto hiyo.

Mheshimiwa Spika, eneo nililolitaja la Lituhi kwenye orodha ya skimu mliyotoa kwenye kiambatisno cha bajeti limetajwa kama Ruhuhu.