Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, asilimia 80 ya mbao laini (soft wood) inatoka kwenye viwanda vilivyoko Mafinga, ambapo kuna kiwanda cha SAO-Hill na viwanda vya wajasiriamali wa kati ambao wanaajiri kati ya wafanyakazi 100 - 200 kwa kila mwenye kiwanda, hii ni direct employments, achilia mbali indirect employment. Kwa ufupi, uchumi Mafinga, Makambako, Iringa na maeneo yote ya jirani unategemea sana suala la uvunaji wa misitu kwa nia ya kuvuna mbao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, katika kitabu chako Mheshimiwa Waziri, sijaona ukigusia viwanda vya mazao ya misitu, hususan viwanda vilivyopo katika Mji wa Mafinga. Kitakwimu, Mafinga na Mufindi inachangia pato la Taifa kwa kiwango cha juu. Mara kadhaa kama Wilaya imekuwa ranked No.3 katika kuchangia pato la Taifa, mchango mkubwa ukitoka katika uzalishaji wa mbao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu ni kwamba Serikali iwasaidie wenye viwanda vya kati kwa kuwadhamini ili wapate mashine za kisasa za kuchania mbao. Ilivyo sasa, hata kama mtu ana shamba la miti, mabenki yanaogopa kukopesha kwa dhana ya risk ya moto. Hawa wajasiriamali wakipata mashine za kisasa wataweza kutumia mabaki kuzalisha vitu vingine kama ulivyosema tooth pick, chip board na kadhalika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee kuhusu umeme. Kiasi cha asilimia 30 ya muda wa kufanya kazi unapotea kutokana na kukatika kwa umeme. Nashauri Wizara ya Nishati TANESCO wafunge sub-station Mafinga ili kuondokana na tatizo la umeme. Kwa sasa umeme unaotumika unatoka Mgololo; na kwa kuwa Mji wa Mafinga umekua na viwanda vya kuchana mbao vimeongezeka, umeme unapofika, unakuwa umepungua nguvu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, nitashukuru kusikia kutoka kwako kuhusu namna gani viwanda vya mbao vya wajasiriamali wa kati vitakuwa incorporated kwenye michango ya Wizara na siku ufike na kuhakikishia hatutaagiza tenda tooth pick nje. Ahsante.