Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

Hon. Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

MHE. JEREMIAH M. AMSABI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa nafasi hii ya kuchangia Wizara ya Kilimo.

Mheshimiwa Spika, kwanza, naipongeza sana Wizara hii ya Kilimo kwa kazi kubwa na nzuri wanayoifanya ambapo tunaona kwa mwaka jana imechangia zaidi ya asilimia 58 ya ajira katika nchi yetu. Ukiangalia Serikali yetu katika mapato inavyo vyanzo vingi, ikiwemo kutoka katika bandari, madini na utalii lakini tukienda kwa kipato cha mwananchi mmoja mmoja kule vijijini zaidi ya asilimia 95, 98 sehemu zingine wanategemea kilimo peke yake. Leo kilimo kinapoendelea ku-perform poorly maana yake wananchi watakuwa na hali mbaya sana.

Mheshimiwa Spika, kule tunapotoka Wabunge wote wanafahamu hali za wananchi ni mbaya sana na hakuna initiative ya maana na ya pekee inayoweza kusaidia sana, yenye high potential for poor growth kama kuwekeza katika kilimo. Hata hivyo, trend zinaonesha sasa hivi hasa kwenye Jimbo langu na Majimbo mengine jirani naona kilimo kinaendelea kushuka na kila wakati watu wanaendelea kukata tamaa. Sababu kubwa ni masoko, kwa kweli masoko yanaendelea kuwa shida. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nikitoa mfano, katika takwimu za Shirika la Chakula na Kilimo la Dunia (FAO) Agosti, 2020 wameonesha Tanzania ni nchi ya tatu katika Afrika kwa kulima tumbaku kwa wingi ambapo Kenya ni ya tisa na South Africa ni ya saba. Hata hivyo, katika uuzaji wa cigarette, Shirika la FAO limeonesha South Africa ni ya kwanza, Kenya ni ya pili na Tanzania ni ya sita. Kwa hiyo, unaona wenzetu wamewekeza sana katika viwanda vya kilimo. Kwa hiyo, lazima Wizara sasa iende kuangalia inavyoweza ku-priotize katika masoko. Motivation kubwa sana ya kilimo kwa wananchi ni masoko tu kuwepo, haya mambo mengine yatakuja. Tukiwa na masoko ya uhakika wananchi watalima sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niwaombe sana Wizara waangalie pia katika suala hili zima la kilimo biashara, bado kuna high cost of production katika nchi yetu kwa sababu ya inputs za agriculture zinauzwa kwa bei kubwa. Kwa mfano, mbolea au pembejeo kwa ujumla wake gharama ni kubwa, sasa hatuwezi kushindana katika masoko na wenzetu wakati sisi uzalishaji wetu ni gharama kubwa ukilinganisha na wenzetu. Ukienda nchi zingine zao lilelile katika unit ileile price inakuwa chini ukilinganisha na kwetu kwa sababu inputs cost yake iko chini sana. Kwa hiyo, niombe sana Wizara iende kuhangaika sana na suala hili.

Mheshimiwa Spika, watu hawashindwi jambo kwa sababu hawana uwezo wakati mwingine watu wanashindwa kwa sababu ya wrong priority. Kwa hiyo, niombe priority kubwa sana katika Wizara hii sasa i-shift kwenda kuwekeza fedha nyingi katika kutafuta masoko, tutafute masoko ndani na nje ya nchi kwa wingi sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niombe sana pia Wizara iende kuangalia, wakati mwingine hatufanyi vizuri katika masoko kwa sababu ya unfavorable terms of trade. Ukiangalia wenzetu Kenya katika exportation maeneo mengi kuna free tariffs lakini kwetu bado cost zetu hata katika kusafirisha ni kubwa. Kwa hiyo, niombe sana Wizara iangalie suala hili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna kazi ilifanyika pale Serengeti katika Skimu ya Nyamitita. Leo ukienda pale Nyamitita kumewekwa fedha nyingi na Serikali lakini bado skimu ile ya umwagiliaji haijakamilika niombe Wizara waende kuikamilisha.

Mheshimiwa Spika, kuna maeneo mengine mazuri sana ya umwagiliaji ambapo wananchi wanapambana sana lakini wanafeli kwa sababu hawajapata support ya Serikali.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante sana.

MHE. JEREMIAH M. AMSABI: Mheshimiwa Spika, maeneo kama ya Isenye, Nata, Nyambuleti yanahitaji skimu za umwagiliaji.

SPIKA: Ahsante sana.

MHE. JEREMIAH M. AMSABI: Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo naunga mkono hoja. (Makofi)