Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

Hon. Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Spika, ahsante mchana huu kuchangia bajeti ya kilimo kwanza naunga mkono hoja pamoja na kuunga mkono hoja naomba nichangie katika maeneo mawili jambo la kwanza ni suala la mfumo wa stakabadhi ghalani na jambo la pili ni suala la export levy kwenye zao la korosho.

Mheshimiwa Spika, tujiulize ni kwa nini mfumo wa stakabadhi ghalani uliletwa na Serikali naomba Waheshimiwa Wabunge wenzangu tupitie sheria ya mwaka 2005 iliyeanzisha mfumo wa stakabadhi ghalani na sheria ile iliyeanzisha export levy kwenye zao la korosho kwa nini tulianzisha hivi vitu viwili.

Mheshimiwa Spika, stakabadhi ghalani ilianzishwa kwa ajili ya kutatua changamoto ya masoko kwenye zao la korosho na mazao ya biashara mwaka 2005, baada ya kuanzisha na kweli mwaka 2006/2007 korosho zilikuwa zinauzwa 150 mpaka shilingi 200 kwa kilo moja baada ya mfumo wa stakabadhi ghalani kuanzishwa korosho ikawa inauzwa shilingi 600 mpaka 800 kwa kilo moja.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo ndugu zangu naomba sana Wabunge wezangu tuende tukaangalie sheria hii na hapa ninaomba wanaye husika bodi ya leseni za maghala, Wizara ya Kilimo pamoja na viwanda na biashara kuna haja ya kutoa elimu ya mfumo wa stakabadhi ghalani kwa wakulima na hasa ukianzia kwa Wabunge wenyewe tuliokuwa humu ndani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa sababu Mkoa wa Mtwara Lindi Tunduru ukimwambia habari ya mfumo wa stakabadhi ghalani haufai kwenye korosho haufai kwenye ufuta utapigwa mawe. Lakini tunapoanza na jambo hili changamoto lazima ziwepo kwa sababu mfumo wa stakabadhi ghalani unakata mirija ya watu waliokuwa wanafaidika na mnyororo wa biashara hii ya ufuta, mnyororo wa biashara ya korosho mnyororo wa biashara ya kahawa na mazao mengine ambayo yako kwenye sheria ya mfumo wa stakabadhi ghalani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mtwara tulipoanza mfumo wa stakabadhi ghalani wakati huo nakumbuka Tyson ndiye aliyekuwa waziri alitukanwa hadharani kwenye mkutano wa hadhara, viongozi wa shirika waliathirika mazao yao mikorosho ilikatwa nyumba zilichomwa moto kwa sababu ya watu wa kati ambao walikuwa wafaidika katika mfumo wa kawaida ili kujua kwamba...

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Taarifa Mheshimiwa Mpakate.

T A A R I F A

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, nilikuwa nampa taarifa mbali na mchango wake mzuri kwa sababu imeingia kwenye hansard aliyekuwa waziri wa kilimo aitwe Tyson anaitwa Stephen Wasira. (Makofi)

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Spika naipokea taarifa kwa mikono miwili.

SPIKA: Mheshimiwa Mpakate anayekupa taarifa anamjua vizuri Mheshimiwa Stephen Wasira kwa hiyo yuko sahihi. (Makofi/Kicheko)

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Spika, yuko sahihi naipokea taarifa yake wakati huo vurugu zilikuwa ni kubwa kuliko hizi unazoziona leo hapa kwenye korosho kwa sababu wafaidika wa mfumo wa zamani ndio waliokuwa wanawaambia wakulima wagome kufuata mfumo wa stakabadhi ghalani na haya ndio yanayotokea maeneo mengine kwenye mazao mengine. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Naomba turejee kwenye sheria ya mfumo wa stakabadhi ghalani na kwa nini Serikali iliamua kuanzisha huo mfumo stakabadhi ghalani. Na bahati nzuri zaidi ni sheria iliyopitishwa kwenye Bunge hili la Jamhuri la Muungano wa Tanzania, walianza na mazao makuu ya uzalishaji 2009 wakaongeza kwenye mazao mchanganyiko sikatai kuna changamoto ambazo Serikali inatakiwa izifanyie kazi, naomba changamoto zote zilizojitokeza kwenye mfumo wa stakabadhi gharali pamoja na ucheleweshaji wa wakulima kupata siwezi kufanya. (Makofi)

MHE: DKT. HAMISI A. KIGWANGALLA: Mheshimiwa Spika, Taarifa.

SPIKA: Taarifa unapewa Mheshimiwa Mpakate endelea Mheshimiwa.

T A A R I F A

MHE. DKT. HAMISI A. KIGWANGALLA: Mheshimiwa Spika, naomba nimpe taarifa rafiki yangu mtani wangu Mheshimiwa Daimu Iddi Mpakate kwamba kila mfumo ambao utawekwa kwa ajili ya kununua mazao ya biashara ama ya chakula utakuwa na losers na winners.

Mheshimiwa Spika, mfumo uliokuwepo awali una losers na winners’ wake, na huu mfumo wa stakabadhi ghalani nao una losers na winners wake miongoni mwa watu ambao ni winners ama wafaidika mfumo huu mpya ni watu ambao wanakaa kwenye kikao kuzigungua zile zabuni wakishaona killichowekwa mle ndani utoka nje kwenda kwa wale wanunuzi ambao wame-submit zile zabuni na kuzungumza kuhusu asilimia 10 ambayo inawekwa over and above bei ambayo alikuwa ameiweka pale ambayo ulipwa pembeni. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa hao wanafaidika na hiyo ten percent hao ni winners, kwa hiyo hata ule mfumo wa zamani nao ulikuwa na watu ambao walikuwa wanafaidika na watu ambao walikuwa wanaonewa na huu mpya pia una watu ambao wanafaidika na watu wanaoonewa kwa hivyo Serikali ifanyie kazi hayo mapungufu ya hiyo ten percent ambayo huwa ilikuwa inawekwa juu ya bei ambayo mtu ame-bid kwenye karatasi nashukuru. (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Daimu unapokea taarifa hiyo?

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Spika, kwanza nikubaliane kwamba kila mfumo una winners na losers na ndio maana nimesema hata mfumo huu unachangamoto ambazo zinatakiwa zifanyiwe kazi na Serikali kwa hiyonakubaliana na maelezo yake kwamba wanatakiwa wafanyie changamoto zote zilizojitokea katika utekelezaji wa mfumo wa stakabadhi ghalani hili wakulima waendelee kunufaika kuliko vile ambavyo vilikuwa mwanzo. Naamini mfumo huu unawasaidia sana wakulima kufaidika ingawa kuna changamoto hizo ambazo mwezangu amezieleza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niende moja kwa moja kwenye export levy mwaka 2018 Serikali ilivyoamua kubadilisha sheria ya export levy iliahidi mambo yote ambayo yalitokana na maamuzi ya wadau wa zao la korosho kukubaliana export levy waanzishe yatayafanya. Miaka mitatu iliyopita Serikali imekusanya zaidi ya bilioni 210 kutoka kwenye sekta ya korosho kama export levy mwaka wa fedha 1920/2021/2018/ 2019 lakini Serikali haijapeleka hata shilingi moja.

SPIKA: Mheshimiwa Mpakate bahati mbaya muda ndio huo.

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Spika ahsante naunga mkono hoja. (Makofi)