Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

Hon. Kenneth Ernest Nollo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

MHE. KENNETH E. NOLLO: Mheshimiwa Spika, nami nashukuru kwa kunipa nafasi niweze kuchangia Wizara hii ya Kilimo ambayo ndiyo Wizara mama na ni tegemeo katika uchumi wetu.

Mheshimiwa Spika, kwanza mimi niseme kwa masikitiko makubwa matarajio niliyokuwa natarajia bajeti hii kutoka kwa Profesa Mkenda si kwa kiwango hiki ilivyokuja.

Mheshimiwa Spika, nilikuwa na matarajio makubwa sana, nilijua Wizara hii bajeti yake itakuwa na transformation lakini ukiiangalia na bajeti zilizopita it is all most the same. Sioni picha kubwa ambayo nilikuwa nayo ya Profesa Mkenda. Kwa kweli bajeti hii binafsi sijaridhika kutokana na nilivyokuwa na matarajio makubwa kutoka Profesa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, bajeti hii kwenye miradi ya maendeleo imetengwa shilingi bilioni 150 ukiacha matumizi mengine. Hivi kweli kilimo cha nchi hii unakipangia bilioni 150 Tanzanian shillings, kwa kweli hatuendi mbele.

Mheshimiwa Spika, nikija Kanda ya Kati kupitia kwenye bajeti huoni strategic vision kwamba hapa Kanda ya Kati kilimo kinakuja kuwekwa sawasawa, huoni programme, huoni chochote. Ukiisoma bajeti imegusagusa tu kwa kudonyoadonyoa na ni story kwamba hapa tulifanya hivi na pale tulifanya vile, lakini picha hasa kubwa ya Wizara ya Kilimo tunaelekea wapi huioni kwenye bajeti.

Mheshimiwa Spika, mimi nataka niseme na nashauri Mheshimiwa Waziri na Mheshimiwa Naibu Waziri tukimaliza bajeti hii hebu waende nje; Waziri aende Egypt lakini Naibu Waziri aende Zimbabwe. Zimbabwe wamenyang’anya mashamba kutoka kwa Wazungu na dunia nzima ikajua sasa Zimbabwe inaenda kufeli lakini wamefanya mapinduzi makubwa sasa kwenye kilimo, kwetu hapa hapana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nchi yetu hailimi, tuko strategically positioned kwa ajili ya kuilisha Middle East na Uarabuni…

SPIKA: Mheshimiwa Waziri wa Maji unakatiza kati ya mzungumzaji na Kiti lakini pia nilishazuia watu kumfuata Waziri Mkuu, ulikuwa haupo ndiyo maana, endelea Mheshimiwa.

MHE. KENNETH E. NOLLO: Mheshimiwa Spika, sisi tumekaa katika position nzuri ya kuilisha Middle East na nchi za Kiarabu ambazo wenzetu kule ni jangwani, lakini ukienda kwenye masoko ya Doha na Abu Dhabi vitu vyote vinatoka South America hadi ndizi na mchicha sasa hii nchi tunaenda huko lini? Ukiwa kwenye ndege unatua hata tu barabarani unakwenda Arusha unakwenda wapi hakuna plantation zozote katika nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, matreka yanayoingia hapa huwezi kulinganisha na Zimbabwe ambao Waafrika wenzetu wameingiza. Kwa hiyo, mimi nachoona bado tunapiga mark time, ASDP I&II zilifadhiliwa sana na donner partners walivyojitoa kwenye basket fund ile ya kusaidia kilimo sasa hivi hakuna ni story tu, ASDP II haina kitu.

Mheshimiwa Spika, nadhani kwenye kilimo tuwe serious, aligusia Mheshimiwa Kandege hapa hakuna kitu ndugu zangu tuseme ukweli kama tunataka kweli twende kwenye kilimo hatujaamua ndugu zangu. Wenzangu wameongelea Minjingu na maeneo mengi hatufanyi vizuri. Sasa nchi hii tunataka kuendelea, lakini tunaendeleaje kilimo tunakipuuzia? Kwa kweli nataka niseme bajeti hii imekuja chini ya kiwango hai-reflect hasa tunataka twende wapi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nchi yetu kama nilivyosema tumejaaliwa tunalima sana mahindi na nchi zinazotuzunguka wanatutegemea sisi lakini bado hatujakaa sawasawa. Hatuwezi kulisha South Sudan, kuna watu tu wametu-block hapo karibu basi hatuwezi kwenda South Sudan. Congo walikuja wanataka…

T A A R I F A

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, naomba kutoa taarifa.

SPIKA: Ndiyo, Mheshimiwa Naibu Waziri tafadhali.

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, naomba kumpa taarifa mchangiaji rafiki yangu Nollo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, pamoja na nia njema sana ya maelezo yake juu ya mchango wa sekta ya kilimo, naomba nimpe comfort kidogo, najua baadaye Mheshimiwa Waziri ataeleza, lakini katika bajeti hii ya mwaka 2021/2022 ASDP II kupitia mradi utakaofadhiliwa na IFAD, Wizara ya Kilimo (mazao na mifugo na uvuvi) tutapata zaidi ya shilingi bilioni 150. Pesa hizi zitakwenda moja kwa moja katika vikundi kusaidia mambo ya mbegu na mengineyo. Kwa upande wa mifugo huko tutakapofika katika Wizara yangu pia vilevile itaonekana.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naomba nimpe comfort na ikimpendeza baadaye nafikiri kupitia Mheshimiwa Waziri atamuonyesha kwa undani zaidi.

SPIKA: Ahsante sana, Mheshimiwa Nolla unapokea taarifa hiyo?

MHE. KENNETH E. NOLLO: Mheshimiwa Spika, siipokei taarifa hiyo kwa sababu hatujapata hizo fedha kutoka IFAD, tunaanza kujadili kwamba tukiokota fedha tugawane, sasa ni story hiyo.

MBUNGE FULANI: Maoteo.

MHE. KENNETH E. NOLLO: Hatuwezi kujadiliana maoteo. Mheshimiwa Spika, kwa kweli nachotaka kusema Serikali iwe serious kwenye kilimo kwani bado hatujawa serious. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nije kwenye Jimbo langu la Bahi tuna skimu za mpunga za umwagiliaji, hazijafanyiwa ukarabati muda mrefu. Mara ya mwisho zimefanyiwa ukarabati mwaka 1998. Skimu ya Ntitaa mwaka 2004 IFAD walitujengea ilifanya kazi mwaka mmoja lile tuta likavunjwa mabilioni ya shilingi hatujawahi tena kuendelea.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nachotaka kusema hebu tuichukulie Wizara hii kama MSD inavyofanya kazi. Kilimo kikianza kufanya kazi kama MSD tutaendelea. Tuchukulie kwamba huu ni uhai wa nchi. MSD inaleta dawa na ndiyo maana tunaendelea kuwa na afya, lakini kwenye kilimo bado tunacheza.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja, ahsante. (Makofi)