Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii nami nichangie katika Wizara hii nyeti ambayo inawagusa Watanzania wengi. Niseme natokea kwenye maeneo ambayo pia ni wakulima, Mkoa wa Kagera.

Mheshimiwa Spika, wakati wengine wakiongelea miradi ya umwagiliaji, Kyerwa, Karagwe na majimbo mengine ya Mkoa wa Kagera hatuongelei miradi ya umwagiliaji. Wakati wengine wanalia na mbolea sisi hatuongelei mbolea, Mungu ametupa rasilimali, mvua ya kutosha, ardhi yenye rutuba na kila kitu, lakini tuna changamoto za kutosha.

Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Kagera tunazalisha kahawa lakini badala ya kahawa kuwa faida imekuwa ni karaha. Mheshimiwa Waziri Mkuu alikuja Kyerwa wakati fulani, nadhani moja ya kati ya kitu alichowaambia wananchi wale akasema sasa kahawa imekuwa ni ngumu kuuza kwa sababu ya janga la Corona, lakini wale wakulima ambao wanategemea kahawa per se haujaweza kuwapatia masoko, unategemea nini kitatokea? Kwa hiyo, nieleze sisi Mkoa wa Kagera tuna changamoto ya masoko ya kahawa.

Mheshimiwa Spika, nimepitia takwimu, ukiangalia uuzaji au uzalishaji wa kahawa Afrika ya kwanza inakuwa Ethiopia, ya pili ni Uganda, lakini ukiangalia ukubwa wa nchi ya Uganda ukakalinganisha na Kagera au na Tanzania, Uganda ni sawa na Kagera tu, lakini kahawa inazalishwa maeneo mengi Tanzania, Uganda wanatuzidi nini? Ukweli ni kwamba Uganda wanaweza kupata kahawa kutoka Tanzania. Jibu liko very simple kwa sababu wanaweza ku- offer price nzuri. Jana Mheshimiwa Mama Rwamlaza ameeleza hapa na mimi nikaangalia price ya kahawa za maganda bado sisi tuko chini.

Mheshimiwa Spika, pia ukirudi kwenye ranking za nani anazalisha kahawa bora, baada ya Ethiopia Tanzania inakuwa ya pili. Kwenye kuzalisha kahawa kwa wingi Afrika tunajikuta tuko kama wa sita, which means sisi bado tuna- advantage ya kuzalisha kahawa bora na ku-penetrate kwenye soko lakini hatufanyi vizuri.

Mheshimiwa Spika, nini imekuwa changamoto yetu ya msingi? Changamoto ya msingi ni vyama vya ushirika na nimeongea hapa mara nyingi kwamba mfumo tulionao wa vyama vya ushirika haufanyi vizuri, ukweli tuuseme. Hatuwezi kuendelea kung’ang’ania mfumo eti kwa sababu Ilani ya Chama chenu imeongelea ushirika, haiwezekani!

Mheshimiwa Spika, lakini nimepitia kidogo record hapa, nilikuwa napitia audited record za vyama vya ushirika hapa ambayo mmeweka kwenye ripoti yenu. Wanasema kati ya vyama 6,021 vilivyopata hati yenye kuridhisha ni 289, hii ya mwisho anasema hati chafu ni vyama vya ushirika 1,670. Kwa hiyo, sasa na hao watu mnaowang’ang’ania hawawezi hata kuandaa records na ukweli ndio uko hivyo, wanakusanya, hawawezi kulipa kwa sababu hawana fedha, it is obvious wanategemea fedha kutoka benki za biashara, kutoka kwenye Benki ya Kilimo lakini inakuja kwa muda gani? Hawa wakulima wanataka fedha waandae mashamba na waweze kupeleka watoto shule. Imekuwa ni changamoto, mnapata kigugumizi gani kuruhusu mfumo huria ukafanya kazi, ndicho kinachofanyika Uganda. Nimeenda Uganda kwa nauli yangu kwa ajili ya kwenda kuona wao wanafanyaje kuhusiana na zao hili la kahawa kwa sababu Kagera na Uganda ni almost the same, maisha na mazingira ni yaleyale, sisi tumekosea wapi?

Mheshimiwa Spika, mimi niwashauri naomba muache mfumo huria u-take place na badala yake mu-intervene kwenye haya makosa madogomadogo na yapo. Mheshimiwa Waziri umekuwa unaongelea butura, ni kweli butura ipo na inaumiza watu, lakini bado Serikali ina uwezo wa kusimamia na kuzuia hicho kitu kinachoendelea, lakini butura ina tofauti gani na biashara ya benki? Watu wanavyoenda kukopa benki si wanakopa kwa riba? Hata butura watu wanakopa kwa riba, cha msingi ni lazima muone mnaweza ku-regulate vipi ili wakulima wasiumie, hicho ndicho naweza kushauri. Mjue kwamba mnavyozidi kuwabana wakulima mnatengeneza maisha yao yawe magumu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini hoja yangu ya pili kwa sababu ya muda niongelee masoko ya kibiashara yale mliyoyajenga Murongo na Nkwenda na maeneo mengine ambayo katika swali la jana nilieleza yamesimama tangu mwaka 2013. Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Kyerwa aliwahi kuuliza swali kuhusu umaliziaji wa haya masoko aliambiwa kwamba zimetengwa shilingi bilioni 1.9 kwa ajili ya kumalizia yale masoko. Swali lilelile akauliza Mheshimiwa Mama Rwamlaza, akaambiwa zimetengwa shilingi 2.5 billion.

Mheshimiwa Spika, nikauliza swali lilelile kwenye Bunge lililopita nikajibiwa uwongo huohuo, nimerudisha hilo swali jana, majibu ninayopewa kwamba, wametenga shilingi milioni 500 kwa ajili ya kwenda sasa kufanya feasibility study kuona yameishia wapi, waanzie wapi kuyajenga, it is not fair Mheshimiwa Waziri. Yale masoko mkiyajenga pale Murongo kwetu ni biashara. Kila kitu kinatoka Uganda upande wa pili kuja Tanzania, wanachokichukua Tanzania ni yale majani tu ya migomba kwa ajili ya kupika sijui wanafanyia na kitu gani kingine. Hii unaiona haiko sahihi. Bado tuna fursa za kufanya biashara, nimewaambia Mikoa ya Kagera hatuhitaji mbolea au irrigation, tunachokitaka ni intervention ya soko basi, mengine tutafanya vizuri.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru. (Makofi)