Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

Hon. Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

MHE. DKT. ASHATU K. KIJAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana na nikushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia kwenye Wizara hii muhimu kwa maendeleo ya watu wetu.

Mheshimiwa Spika, naomba nianze kwa pongezi kwa Mheshimiwa Rais wetu mama Samia Suluhu Hassan kwa mwongozo wake sahihi alioutoa na hasa kusababisha mfumo wa stakabadhi ghalani kusitishwa kwenye Mkoa wa Dodoma mwaka huu, 2021. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ni uongozi makini na sina wasiwasi na uongozi wa Profesa Mkenda, nimefanya naye kazi ni kiongozi makini, nina uhakika atatuvusha Watanzania. Lakini pia Mheshimiwa Naibu Waziri, kaka yangu Bashe nikupongeze sana tumeanza mbali tangu tukiwa wanafunzi. Nafahamu uwezo wako, simama kwenye haki na Mwenyezi Mungu atakusimamia utatenda vyema. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimepongeza kwa kufutwa kwa stakabadhi ghalani au kusitishwa kwa mwaka huu 2021. Lakini Wanakondoa wamenituma niulize kwa Serikali, je ni mwaka huu tu 2021? Au mfumo huu kwa mikoa ambayo hatuna mfumo ambao ni strong wa ushirika, hauruhusiwi tena kufanya kazi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimetumwa kuuliza suala hili kwa sababu mwaka jana Mkoa wa Dodoma na hasa Kondoa tulipita kwenye mazingira magumu sana. Nilimsikiliza vizuri Mheshimiwa Mbunge wa Songwe jana Mheshimiwa Mulugo akiongea mpaka kufikia kutishiwa kwa ajili ya kutetea wananchi wake. Mheshimiwa Mulugo, mwenzako Kondoa mwaka jana ilikuwa ni zaidi ya kuuwawa, sasa sijui zaidi ya kuuwawa ni nini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ni hatari mno, unaposimama na wananchi unawaeleza mfumo wa stakabadhi ghalani ni nini? Mfumo wa stakabadhi ghalani hauji kwenye masoko peke yake. Tunapoongelea kwenye masoko hapa tunaukuta mfumo wa stakabadhi ghalani na TMX, hapa ni climax. Lazima uwe umeshaanza kufanya kazi kuanzia kwenye uandaaji wa mashamba ya wananchi. Wananchi wanaandaje mashamba? Wanapataje mbegu bora na sahihi? Wananchi hao wanatunzaje mazao yao? Wananchi hawa, je wana vyama vya msingi kwenye maeneo yao? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wewe unatoka Dodma, nimekusikia jana umesema na wewe unashukuru mwaka huu kusitishwa lakini wananchi wetu wameumia. Wapo wananchi wameamua kuacha kulima zao la ufuta kwa sababu ya mfumo huu wa stakabadhi ghalani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa Mheshimiwa Waziri, Profesa Mkenda kaka yangu nikuombe sana hebu angalia huo mfumo. Kwanini wananchi wanaupigia kelele? Yaani Serikali inasema unamsaidia mwananchi halafu mwananchi anapiga kelele? Hapa mbona ni vitu viwili ambavyo havieleweki. Unakuja kufuta mfumo wa stakabadhi ghalani tayari wakulima wameacha kulima ufuta, umetusaidia kweli? Hebu tunaomba tuanzie mwanzo tusimame imara tuone ni jambo gani tunatakiwa kufanya. Kwanini mfumo wa stakabadhi ghalani?

Mheshimiwa Spika, walikuja pamoja, stakabadhi ghalani pamoja na TMX, na kwa hili naomba niishauri Serikali yangu tukufu. Soko lile la bidhaa TMX wamewekeza kiwango kikubwa kwenye miudnombinu ya TEKBOHAMA. Mifumo ile iliyowekezwa tusi--justify kwa kuumiza wananchi wanyonge, hapana. Kwa hiyo, jambo la msingi kwenye mfumo ule wa TMX soko la bidhaa kwanza Serikali iangalie pale ambapo ipo Wizara ya Fedha ni sehemu sahihi ya kuweka soko la bidhaa? Soko la bidhaa linatafuta masoko. Masoko yanatafutwa na Wizara ya Viwanda na Biashara, inakuwaje TMX ina-hang kwenye Wizara ya Fedha. Inakuja inajiunganisha na Wizara ya Kilimo hapa katikati kuna kitu kinakosekana. Kwa hiyo, tusiende kuwaumiza wananchi wetu kwa sababu ya vitu ambavyo hatujavifanyia kazi vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba nim-quote Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika. Alisema maneno yafuatayo; the future millionaires and billionaires of Afrika will come initially from agriculture. Kilimo…

SPIKA: Ahsante sana.