Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

Hon. Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

MHE. ANTHONY P. MAVUNDE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi. Ili kukiboresha kilimo cha zao la zabibu hapa Dodoma ni lazima Wizara sasa iweke nguvu kwenye kituo cha utafiti cha TARI Makutupora ili kuboresha huduma za ugani na kuwafanya wakulima waweze kuzalisha kwa tija.

Mheshimiwa Spika, hivi sasa kwa Dodoma wakulima wetu wanatumia gharama kubwa kulima kwenye shamba la hekari moja lakini wanachokipata ni tofauti na gharama waliyoitumia na hivyo kusababisha gharama kuwa kubwa sana. Ekari moja ya mkulima aliyelima vizuri zabibu Dodoma inaweza ikmapa mpaka tani tatu. Huyu ndiye aliyelima vizuri. Lakini ukienda Afrika Kusini, Western Cape mkulima anapata tani 12 kwa ekari moja.

Mheshimiwa Spika, niiombe Wizara, pamoja na kwamba tuna kituo pale cha Makutupora, tunaomba mafunzo yaendelee na ikiwezekana maafisa ugani hawa muwapeleke wakajifunze Afrika ya Kusini. Mheshimiwa Waziri, wasindikaji wa zabibu wa Dodoma walikuwa wako tayari kuwalipia maafisa ugani kwenda Afrika Kusini kujifunza. Itakuwa ni jambo la ajabu sana kama private sector wenyewe wakiwalipia maafisa ugani wa Serikali na Serikali ipo. Mheshimiwa waziri, nikuombe waende wakajifunze Afrika ya Kusini ili tuongeze tija ya mkulima wa zabibu wa hapa Dodoma. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, na hii ndiyo inasababisha St. Anna ya Afrika Kusini inauzwa shilingi 8,000 hapa Dodoma na Dompo ya Dodoma inauzwa shilingi 12,000 kwa sababu ya gharama za uzalishaji ni kubwa sana niiombe Serikali katika eneo hili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Hivi sasa Rwanda wame-take advantage, hivi sasa wanawakaribisha Wajerumani, muda sio mrefu wataanza kuwa wazalishaji wa bulk wine wakubwa hapa East and Central Africa. Wanyarwanda walikuwa wanakuja Mpunguzi, Mvumi na Chamwino kununua zabibu sasa hivi hawaji. Wameanza kulima wenyewe. Wakenya walikuwa wanakuja, sasa hivi hawaji, wanalima Mount Meru kule.

Mheshimiwa Spika, ukiangalia kwa Afrika, ukiondoa Afrika Kusini nchi nyingine hapa ya Kiafrika kama sisi kwetu hapa ni Tanzania peke yake ndiyo tunazalisha wine kwa kiwango kikubwa sana. Afrika ya Kusini wanazalisha tani lita bilioni 1 za wine kwa maana. Dodoma kwa maana ya Tanzania hatujawahi kuzidi lita milioni 15. Kuna kazi ya kufanywa hapa na niombe Serikali itusaidie katika hili. Wawapeleke wataalam wakajifunze, vinginevyo zabibu yetu itaendelea kulala na itaoza mashambani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la pili ambalo nataka nilichangie; Ilani yetu ya Uchaguzi inasema kuhusu ajira na naona ajira nyingi zinatengenezwa kwenye Sekta ya Kilimo. Nimesoma jarida the global employment trend, inasema sekta mbili zitachangia sana kwenye kutatua changamoto ya ukosefu wa waajira hasa kwa vijana, viwanda na kilimo. Hapa kuna mpango mkakati wa Wizara wa kuwahusisha vijana kwenye kilimo.

Mheshimiwa Spika, iko fursa kubwa sana ambayo hatuitumii vizuri. Katika viwanda vya usindikaji wa matunda hivi sasa, hasa kutumia Mzee Bakhresa kwa viwanda vyake. Wana mahitaji ya tani za matunda 120,000 za maembe kusindika lakini capacity iliyoko hivi sasa ni takriban tani 25,000 kwa hiyo iliyobaki yote wana-import pulp kutoka nchi za nje.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Bashe unafahamu mzee Bakhresa alikuwa tayari kuisaidia Serikali kwenye kuandaa mashamba na kuweka miundombinu ya umwagiliaji ili vijana wengi zaidi wapewe mashamba ya kutosha tuanze kuuza matunda hayo kwenye viwanda vya Bakhresa na Sayona ambapo mahitaji yao ni tani 120,000 lakini hivi sasa wanapata tani 25,000 tu. Serikali ione jitihada sasa, ione ulazima wa kutayarisha mashamba makubwa soko la uhakika lipo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwenye ukwaju Bakhresa anahitaji tani 15,000 za ukwaju kwa mwaka. Sisi tuna uwezo wa tani 4,000, anaingiza pulp kutoka nje ya nchi. Hili ni eneo ambalo pia tunaweza tukalifanyia kazi vizuri. Mananasi yetu, mengi yaliyoko hayafai kutengeneza juisi na mananasi pekee ambayo yanafaa kwa Afrika ni MD2 ambayo yaliingizwa miaka 42 iliyopita nchini Ghana kutokea Costa Rica ambayo ndiyo hata akina Bakhresa na Sayona wanayahitaji. Sasa tuna vijana hapa ambao wengi wangeweza kufanya kazi ya kilimo. Serikali, nawaomba kazi yenu nendeni mkatayarishe mashamba ya kutosha, wekeni miundombinu, soko lipo. Tukifanya hivyo tutakuwa tumewasaidia vijana wa Tanzania. (Makofi)

SPIKA: Ahsante sana.

MHE. ANTHONY P. MAVUNDE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. (Makofi)