Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

Hon. Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa kunipatia nafasi na nianze kwa kuunga mkono hoja na pili naunga yote yaliyoongelewa kwenye taarifa ya kamati.

Mheshimiwa Spika, nianze kwa kusema kuwa ili tufanikiwe katika kilimo chetu kwa kuzalisha kwa tija lazima tuangalie kweli masoko kwa sababu tukiangalia masoko mambo yote yatajituma na wakulima watajituma wenyewe kwa wenyewe. Kwa mfano, tukiangalia kuna kitengo cha masoko katika wizara, nilikuwa nakuomba kuwa Mheshimiwa Waziri akiangalie hicho kitengo cha masoko kifanye kazi kisikae tu kitafute masoko kusudi wakulima waweze kupata masoko ya mazao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa mfano kuna mazao ya miwa, Mheshimiwa Waziri alitembelea viwanda vyote vya miwa anajua matatizo yote ya viwanda vya miwa, anajua matatizo yote ya skimu zote za miwa, nilikuwa nashauri kuwa Mheshimiwa Waziri tulikuwa wote kwenye baadhi ya viwanda naomba kuwa matatizo yote yaweze kutatulika. Leo asubuhi nimeongea na wakulima wa miwa Kilombero, Iyovu bado matatizo yapo palepale, kwa upande wa masoko naamini kuwa wale wakulima miwa matatizo yote yakitatuliwa wakulima wa miwa hawatakuwa na tatizo la masoko. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, na hapa Tanzania tutaweza kuzalisha sukari ya kutosha kuweza kuwa hatutakuwa na deficit yoyote kwenye sukari. Kwa mfano kule Iyovu wanatupa miwa ambayo haiwezi kuzalisha kwa sababu kiwanda ni kidogo, lakini kulikuwa na tatizo la kupanua kiwanda, hilo tatizo likiisha wataweza kufanikiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tulikuwa tatizo wanachoma miwa ya wakulima na hiyo miwa hainunuliwi inakaa tu, ukienda Dakawa kiwanda bado hakijaisha, ukienda kule Mtibwa bado wanamatatizo yao kwa hiyo matatizo yakiisha hiyo ni mfano mmoja wa masoko. Kwa mfano kama masoko yapo chukulia kuwa uzalishaji wa wakuku wa singida unaona kuwa wanauzwa tu kwa sababu masoko yapo ili masoko yaendane pamoja na miundombinu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nikisema miundombinu naelezea barabara za mashambani, nikisema miundombinu naelezea viwanja vya ndege, kwa mfano wakulima wa parachichi, wakulima wa mazao ya bustani najua Mheshimiwa Jacqueline yupo pale wakati mwingine wanapata matatizo kwa sababu ya usafirishaji kwenda nje lakini soko lipo. Kwa hiyo Mheshimiwa Waziri tuangalie mazao ya bustani kwa sababu yanazalisha kwa mara moja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naongea haraka haraka nakwenda kwenye pembejeo, najua wewe ulisemea pembejeo hasa kwenye mbegu, mbegu za alizeti kama kamati pamoja na wizara tuliwaambia kuwa lazima tusimamie uzalishaji wa mbegu za alizeti na kweli tutasimamia kusudi hizo mbegu za alizeti ziweze kuzalishwa kwa wingi na hasa kilimo cha umwagiliaji kama mlivyoona kuwa hela nyingi zitakwenda kwenye kilimo cha mbegu na hasa kwenye umwagiliaji. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ukiangalia upande wa mbolea pamoja na viwatilifu lazima na vyenyewe viangaliwe kusudi tuzalishe kweli kilimo chenye tija lazima tuangalie masoko, tuangalie pembejeo pamoja na kilimo cha umwagiliaji. Ukiangalia sasa hivi tuna tatizo la mvua kama hatutajikita kwenye kilimo cha umwagiliaji tutakaa tunasema tunalima, lakini tunalima vitu vyetu vinakauka. Uvunaji pamoja na mabwawa pamoja na skimu zetu lazima zitengenezwe tuweze kupata kilimo cha umwagiliaji. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo lingine ni tafiti, tafiti hapa nasema tafiti wa udongo lazima udogo ufanyiwe utafiti huwezi kuweka mbolea tu kama utafiti kwenye udogo haujafika ili tuzalishe vizuri lazima tutoe hela za tafiti, lazima tufanye tafiti kwenye sehemu mbalimbali. (Makofi)

SPIKA: Ahsante sana.

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, Mwisho Afisa Ugani pamoja na bajeti lazima itolewe na mfumo wa ushirika lazima uangaliwe. Ahsante nakushuru sana. (Makofi)