Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

Hon. Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kuniona.

Mheshimiwa Spika, kwanza nishukuru sana kwa hotuba nzuri iliyosheheni mikakati mizuri ya kuboresha na kuinua sekta ya kilimo. Naamini wakipata fedha hizi ambazo zinaombwa basi wataweza kutubadilishia sura ya kilimo na pengine tutaona tija ikiongezeka kwa kasi katika sekta hiyo.

Mheshimiwa Spika, nianze kwanza kwa mtizamo wa kinadharia kwamba, duniani kote tija kwenye kilimo inaongezwa kwenye nchi zote tija inaongezeka kuliko idadi ya watu, watu wanaongezeka kwa asilimia mbili au chini ya asilimia mbili wakati tija kwenye kilimo, kwenye mataifa takribani yote inaongezeka kwa asilimia siyo chini ya saba.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naamini kwamba kutokana na hilo ni kwamba tunachangamoto kubwa ya kuhakikisha kwamba bei za wakulima zitapanda, haziwezi kupanda ikiwa kwamba supply inaongezeka kuliko demand. Na pili hili linajitokeza hapa kwetu pia kwamba mwaka ambapo tumepata neema ya mvua zao likawa kubwa, mahindi walikuwa wanasema bei za mahindi zinashuka kwa zaidi ya nusu inashuka by more than fifty percent na nyingine hata thirty percent ya mwaka ule ambapo kumekuwa na changamoto za uzalishaji inashuka zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, na kwamba mkulima anajaribu sana anatumia gharama nyingi lakini inapokuja kuuza kwa sababu ni cobweb theory iko hapo inaitwa cobweb theory inakuwa kama mkulima hawezi kuwa tajiri. Kwa hiyo, njia pekee ya kuweza kuwa wakulima wenye kupata utajiri ni lazima tujitofautishe na wengine duniani tujue kwamba ni zao lipi ambalo likizalishwa lina soko. Kwa mfano, tukiweza kuwahamasisha watu kutumia organic crops tukaweza kuotesha bila kutumia nanii sana unakuta kwamba bahati nzuri ndiyo unapata bei nzuri.

Mheshimiwa Spika, unatofautisha zao lako na la wengine duniani iwe Kahawa iwe chochote kile lakini organic ndiyo kinatafutwa, lakini pia kuna mazao kama maparachichi/avocado hizi ambazo pia na zenyewe zinaweza kupata demand kubwa ni vitu vya kuhamasisha tusing’ang’anie vilevile vya zamani, tusing’ang’anie tu mahindi tung’ang’anie vitu ambavyo tunaweza tukauza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nashangaa katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri hajazungumzia masuala mazima ya horticulture, mboga mboga, matunda na vituo kama hivyo ambayo kweli unaweza ukaotesha mara tatu, mara nne hasa ukiwa na umwagiliaji ukaotesha throughout the year na ukawa tajiri. Lakini nataka kusema kwamba hilo ni jambo ambalo lazima walivalie njuga kwa sababu linahitaji mkakati ambao ni endelevu ili tuweze kulitekeleza hili.

Mheshimiwa Spika, kwa upande mwingine watu wameonyesha changamoto sana kwenye ushirika lakini nataka niseme kwamba, nadharia ya ushirika inabakia palepale ni nadharia nzuri hatuwezi kuwasaidia wakulima bila kuwa na ushirika. Tatizo la ushirika ni nini? utawala bora na hiyo lazima sheria hii ya ushirika ibadilishwe ili kuwe na udhibiti zaidi kwa wale wanaochaguliwa kuongoza taasisi hizi, waweze kutoa mrejesho kwa kuwa na financial statements zinazotoka na zinaenda kwa wanachama wake na wanazijadili na wale viongozi wanaoshindwa wanatolewa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nafikiri hilo ni jambo la msingi na matatizo yote bila Serikali kujikita na Mrajisi ile Ofisi ya Mrajisi kuwa na uwezo hatutaweza kuleta nidhamu kwenye ushirika na kila wakati tutasema kwamba ushirika ni wezi na nini lakini wataendelea kuiba kama hawana udhibiti wa kutosha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna issue ya skimu za umwagiliaji, kule kwetu kuna skimu ya Kahe hasa ile ya Mawala kule kunachangamoto sana na naomba kwamba kusema kweli tumeorodheshewa nyingi kwenye kwenye kiambatisho tuliyopewa na Mheshimiwa Waziri, lakini naamini kwamba kuna ambazo ni kubwa na zinahitaji marekebisho makubwa haraka sana na hasa hii ya kwetu za Kahe kule ndiyo tunazalisha, Kilimanjaro hatuna Mpunga isipokuwa sehemu hizi za Kahe.

Mheshimiwa Spika, naomba pia tuangalie mambo mengine kwa mfano kuwezesha wakulima kupitia constituency au ward mechanization centers tusiseme kwamba tunawasaidia wakulima kwa kuwapa mmoja mmoja lazima tuwe na center moja ambayo itachukua na vifaa vile mtu anaweza akakodisha kwa bei nafuu au akakodishiwa bila kuchajiwa mpaka akaja akakatwa wakati anapouza mazao yake.

Mheshimiwa Spika, lakini ni vigumu mkulima kununua trekta na mwisho waziri amezungumzia hili la kuongeza mitaji kwa wakulima. Lakini nafikiri badala ya kuwapa fedha tuwape lease arrangement ambapo yaani wanapewa mashine halafu wanalipa polepole wanapoendelea kuuza vifaa vyao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, namshukuru Mheshimiwa Waziri kwa kufirikia hilo la kwamba financing ni kitu cha msingi na naona amesema anaunda kamati ambayo itamsaidia kufirikia zaidi namna gani wakulima wapate mikopo ya riba nafuu.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naunga mkono hoja. (Makofi)