Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Dr. Joseph Kizito Mhagama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Madaba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuchangia.

Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa naomba niwapongeze sana Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na Makatibu Wakuu wa Wizara hii wote wawili pamoja na Wakurugenzi kwenye Wizara hii. Mimi nimefanya kazi nao na nime-interact nao, watu hawa ni watu makini sana na iwapo Bunge lako litawashauri vizuri, tutapata mapinduzi makubwa sana kwenye sekta hii, hiyo ndiyo imani yangu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, leo sikupenda nichangie kwa sababu ya mazingira yalivyo na mfumo na muundo wa Wizara hii bado haunishawishi kwamba maoni yetu yanaweza kuzaa matunda. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ukienda kwenye mapori yote ya Mikoa ya Rukwa, Ruvuma, Tabora, Katavi, mikoa yote ambayo wewe unaifahamu ambayo haikuwa na mifugo, mapori yote yamejaa ng’ombe. Madhara yake ni nini?

Mheshimiwa Spika, madhara yake ni kwamba katika muda mfupi ambao unaweza ukaupima kabisa kwa miaka, Tanzania inakwenda kuwa jangwa; na kwa nini tumefikia hapo? Tumefikia hapo kwa sababu wafugaji wetu kwanza hawana ardhi ya kufugia; lakini pili, hakuna malisho. Kwa hiyo wanahama, wanasafiri, wanakwenda, wanajaribu kuhangaika; lakini la tatu; ubora wa mifugo yetu ni duni, tunafuga wanyama wengi lakini tija ndogo kwenye ufugaji. Hizo ni baadhi ya sababu ambazo nilitaka nizitaje.

Mheshimiwa Spika, nafasi ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi kumaliza tatizo hili ni ndogo kwa sababu tatizo la kuhama wafugaji halihusu Wizara ya Mifugo peke yake na ndiyo maana nilikuwa nachelea kushauri Bunge lako liishauri Serikali iunde tume au iunde coordination team ambayo itahusisha Wizara zisizopungua tano, wafanye pamoja kazi hii ya kuratibu ufugaji nchini.

Mheshimiwa Spika, wafugaji wanahitaji ardhi, wanamuhitaji Waziri wa Ardhi, wanapotaka kuingia kwenye eneo kuna Maliasili, kuna Kilimo, kuna Mazingira, Wizara hizi zote kama hazitaamua kufanya kazi pamoja hatutakuwa na ufugaji bora nchini, tuta-fail tu. (Makofi)

SPIKA: Nakuongezea na Wizara ya Maji.

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA: Mheshimiwa Spika, na Wizara ya Maji, ahsante. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi niombe na nashindwa kwenda zaidi, hatuwezi kutoka hapa tulipo. Leo nchi hii inakwenda kuwa jangwa. Mimi ni mfugaji na nina ranchi, ninafuga lakini nikienda Songea Vijijini kila pori wapo wafugaji na ukiwauliza wanasema hatuna pa kufugia, hatuna ardhi.

Mheshimiwa Spika, leo tunashauri kwamba wapewe ranchi za Serikali, well and good, lakini kama hatuwajengei uwezo wa kuzalisha chakula cha mifugo kwa maana ya pastures, uwezo wa kutengeneza visima vya maji, uwezo wa kuzalisha ng’ombe bora, hatutamaliza tatizo hili kwa sababu tutamaliza hizi ranchi za Serikali lakini bado zitakuwa hazitoshi kwa sababu ng’ombe ni wengi sana.

Mheshimiwa Spika, mimi nikuombe na nitashika shilingi baadaye; Serikali ianzishe coordination team ya kuratibu ufugaji nchini. Ahsante. (Makofi)