Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Janejelly Ntate James

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. JANEJELLY J. NTATE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi hii nimshukuru Mwenyezi Mungu ambaye ataniwezesha kuchangia ninayoenda kuchangia.

Kwanza nimshukuru Mheshimiwa Waziri na Naibu wake na niwapongeze kwa kazi wanayofanya, wanafanya kazi kwenye mazingira magumu sana. Lakini pia naungana na Taarifa ya Kamati ya Kilimo, Maji na Mifugo asilimia 100 kwa yale yote ambayo wameshauri.

Mheshimiwa Spika, lakini mimi nijikite kwenye bajeti inayotolewa kwenye Wizara husika. Ukingalia bajeti iliyoletwa mbele yako kuombwa hapo bajeti ya Wizara yote ni shilingi 199,194,996,810; lakini uvuvi peke yake imepewa shilingi 122,350,470,000; mifugo imepewa shilingi 47,844,949,810.

Mheshimiwa Spika, ukitafuta percentage uvuvi wamepata asilimia 71.7; mifugo wamepata asilimia 28.3; ukiliangalia kwa macho ya kawaida uvuvi inaimeza mifugo, lakini hapa tunasema asilimia 60 ya Watanzania wako kwenye kilimo, uvuvi na mifugo.

Mheshimiwa Spika, lakini Idara moja ya Mifugo imemezwa na uvuvi, hapa watatokaje? Hatuwezi tukaona utendaji ulio bora kwenye mifugo lakini pamoja na bajeti hiyo kuwa ndogo, inachelewa kupelekwa kwenye Wizara na inapelekwa kwa asilimia ndogo sana, lakini tunataka mifugo na uvuvi viendelee. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wewe ni Mbunge wa muda mrefu ndani ya Bunge hili, unakumbuka historia nyuma Wizara ya Maji, Nishati na Madini zilivyokuwa pamoja, Idara ya Madini ilikuwa inazimeza Wizara zingine idara zingine hazikuonekana kabisa zilichokuwa zinafanya. Lakini kwa makusudi ya ushauri wenu kama Bunge mkashauri Wizara zikatoka tatu mle; ikatoka Wizara ya Maji, Nishati na Madini na mafanikio tumeyaona. Mimi niombe tu kwa kiti chako Mheshimiwa Balozi juzi alichangia akasema Bunge la Kumi na Mbili nasi tutoke na alama kwenye kilimo, uvuvi na mifugo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tuishauri Serikali isiangalie gharama ichukue maamuzi magumu ya kuzitenga hizi idara mbili; uvuvi iwe na Wizara yake na mifugo iwe na Wizara yake. Baada ya kulifanya hilo utendaji unaweza ukaonekana. Kwa kweli Waziri akiwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi mtu mmoja ni pasua kichwa, kwa sababu anagusa maisha ya wananchi chini kabisa kila Mtanzania anamgusa, lakini anamgusa kwa mazingira magumu sana ya bajeti kutotosha na ya kwamba kila mwananchi anatakwa aguswe. Lakini hapo hapo idara moja inapewa hela kidogo, idara nyingine inapewa hela kubwa, ni ngumu sana kufanya kazi kwenye mazingira hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pili nishauri kwenye uvuvi; niliwahi kusema kwenye Mpango wa Maendeleo kwamba Tanzania tumebalikiwa kuwa na maji ya kutosha, maziwa, bahari na mito lakini bado hatujawekeza kwenye uvuvi bado hatujajikita kwenye uvuvi. Leo hii kama Serikali ikichukuwa makusudi mazima kujenga vizimba kila maziwa yetu, wakawapa wananchi hata kwa kukodisha, tukawekeza mapato yatapatikana, ajira zitapatikana na uvuvi utaendelea. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba kuunga hoja mkono ahsante sana.