Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. ABDALLAH H. ULEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu. Pili, naipongeze sana Serikali kwa jitihada zake za uchumi wa viwanda kwenye nchi yetu. Pia, nampongeza Mheshimiwa Waziri na kwa namna ya pekee kabisa nampongeza Mheshimiwa Rais wetu, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa niende kwenye hoja moja kwa moja. Naomba Mheshimiwa Waziri anieleze ni namna gani iliyo rahisi kabisa viwanda vinaweza kupata malighafi ya gesi kwa ajili ya uzalishaji wa umeme? Mfano, Kiwanda tarajiwa cha marumaru (tiles) cha Goodwill Ceramic Tiles kinahitaji gesi na wawekezaji hawa wapo tayari kabisa kujenga bomba kwa gharama yao wao wenyewe (Mkopo kwa TPDC): Je, Wizara itasaidiaje kuharakisha jambo la namna hii?
Mheshimiwa Mwenyekiti, wawekezaji hawa pia wa Goodwill Ceramic pia wameomba bei ya gesi iweze kuwa stable (imara). Naiomba Wizara ya Viwanda isaidie pia katika kuhakikisha inashirikiana na Wizara ya Nishati na Madini kuharakisha jambo hili pia. Mwisho, naipongeza tena Serikali kwa jitihada hizi na kusisitiza kuwa jitihada hizi ziendelee kwa manufaa ya Taifa letu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.