Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuchangia Wizara hii muhimu sana na nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri kwa kazi nzuri wanayoifanya na kwa kweli kwenye hotuba yake nimepita nimeona miradi kadhaa wameweka kwa ajili ya wananchi wa Jimbo la Hai, ahsanteni sana.

Mheshimiwa Spika, nilikuwa naomba nianze kwa kuchangia kwenye eneo la Vyama vya Ushirika Maziwa na hapa niwapongeze sana wenzetu wa Vyama vya Ushirika ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro, lakini hususani Jimbo la Hai wanafanya vizuri sana na wanafanya vizuri kwa sababu wamejiratibu vyema na sasa hivi tuna mradi wa kutengeneza chakula cha mifugo pale Uduru ni kwa sababu ya ushirika mzuri; huko haufanani na kule kwingine nilipokua napigia kelele, lakini hapa wanafanya vizuri sana.

Nimuombe Mheshimiwa Waziri tafadhali tusaidie kuratibu vyama hivi vya ushirika kwa sababu viko tofauti tofauti vikae pamoja na wawe na mipango ambayo inatuwezesha kuwa wamoja, kama wakiweza kuunganisha nguvu yao tunaweza tukapata kiwanda cha maziwa na bahati nzuri walishaanza mchakato wa kutafuta eneo la kujenga kiwanda cha maziwa. Kwa hiyo, mtusaidie kuwa coordinate vizuri ili wawe na mpango uliofanana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini kwenye ushirika huo kumekuwa na changamoto kwa sababu hawajakaa pamoja kwa hiyo vyama viko scatterd, Mheshimiwa Waziri labda nikueleze kidogo namna ambavyo sisi tunafuga; katika Jimbo la Hai tuna ufugaji wa aina mbili tofauti, tuna wafugaji wa Kata hizi za upande wa Kaskazini wanafugia ndani. unakuta mwananchi ana ng’ombe wake wawili/watatu anawafugia ndani, kwa hiyo unalazimu kuwa tafutia chakula na madawa kwa kuwaletea ndani.

Mheshimiwa Spika, lakini upande huu wa tambarare wananchi wanafuga kwenye jamii ya Wamasai kwa kutafuta malisho. Sasa changamoto zao kubwa hasa sasa hivi wale ng’ombe ambao wanafugiwa ndani ni wale ng’ombe wa kienyeji.

Sasa niwaombe sana mtutafutie namna ambavyo tunaweza kupata mbegu mpya kwa sababu tunapata shida sana sasa hivi hata kupandisha wale ng’ombe, mwananchi ili aweze kupata mbegu ya kupandishwa ng’ombe anahitaji shilingi 20,000; hii ni changamoto kwa mwananchi wa kawaida.

Mheshimmiwa Spika, lakini pia analetewa mtaalamu anakuja kubandisha ng’ombe huyo anapandisha zaidi ya mara tatu/mara nne na hiyo shilingi 20,000 ni kwa wale ambao wako karibu na mjini; vijiji kama Ng’uni ambavyo viko nje ya mji kidogo wanakuwa-charged mpaka shilingi 50,000 kuweza kupandishiwa ng’ombe mmoja. Kwa hiyo niombe kwa sababu wenzetu wa Tengeru wapo pale karibu na Arumeru, basi tuleteeni mazingira haya yawe rafiki na ikiwezekana mtuletee mbegu ambazo zinaweza kufugika ambazo tunapata maziwa ya kutosha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tunayo changamoto nyingine kwenye vyama vyetu hivi vya ushirika; maziwa tunayoya kutosha na niwapongeze sana wenzetu wa kule Mronga kwa kweli chama kile kimejiimarisha vizuri, wamefika mahali mpaka wameweza kutengeneza kiwanda kidogo cha kuzalisha maziwa, kule Mronga na kule Ng’uni wamefanya vizuri sana. Sasa tunafikiria badala ya kuendelea kufanya vyama vidogo vidogo waungane pamoja tujenge kiwanda kikubwa na kizuri na pale Uduru wenzetu wa Tanga Fresh walikuwa wameweka cooler yao wanakusanya maziwa.

Mheshimiwa Spika, lakini kumekuwa na changamoto, hawa wakusanya maziwa wamekuwa wengi sana, tunaomba sasa tutafute namna ya ku-centralize awe mkusanyaji mmoja ili tuweze kuuza kwa tija. Sasa hivi huku mtaani wananunua shilingi 700, lakini ukiangalia kwa bei ya soko tuna uwezo wa kununua lita kwa shilingi 1,000 kama watakaa pamoja ikiwa ni pamoja na kupata wataalamu. Tunayo shida sana ndani ya Wilaya ya Hai wataalam tulionao hawatutoshelezi. Lakini kwa upande wa tambarare huku bado kuna shida tunahitaji wataalam wa kuwafundisha ndugu zangu na bahati nzuri mimi ni Laigonan nilipewa hishima hiyo na ndugu zetu Wamasai, sasa nina kazi ya kuwalea vizuri ili tufuge kwa faida.

Mheshimiwa Spika, mimi siyo muumini wa kupunguza mifugo, mimi ni muumini wa kuongeza, lakini tufuge kwa tija na maeneo tunayo tukifunga vizuri pamoja ya kwamba eneo lile la KIA lina mgogoro wa aina yake, lakini bado tunaweza kujipanga vizuri kama tutapata wataalamu. Lakini tunayochangamoto ya kuwa na majosho ya kuweza kuwahudumia wanyama wetu, niombe sana yale yalioko pale mengi yamekufa, hatuna hata moja linalofanya kazi.

Kwa hiyo, niombe na nimejaribu kupita kwenye bajeti yako sijaona jambo hili Mheshimiwa Waziri pamoja na kwamba nilikuandikia, sasa nikuombe sana utusaidie maeneo yale ya wafugaji upande wa tambarare waweze kupata maeneo ya kulishia, lakini pia waweze kupata majosho ili waweze kufuga kwa kisasa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini kubwa tunalohitaji upande ule ni elimu wapewe elimu kwa sababu ng’ombe ni deal, ukianza ngozi yake, ukienda maziwa, sasa tunafuga kwa upande wa tambarare tunajikita sana kwenye upande wa nyama maziwa tumesahau…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Mheshimiwa Saashisha Mafuwe…

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Spika, ahsante naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)