Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kunipa nafasi hii na niwashukuru sana Waziri mwenye dhamana, Naibu Waziri na Katibu Mkuu wa Wizara hasa kwa kushughulikia kero za wavuvi kwenye eneo la Ziwa Tanganyika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi nitajikita zaidi kwenye eneo la uvuvi. Uvuvi ni eneo ambalo linaweza likalipatia pato la Taifa kwa kiwango kikubwa sana. Lakini kwa bahati mbaya sana Ziwa Tanganyika ni ziwa ambalo halijawekezwa kitu chochote ambacho kinaweza kikatoa tija kwenye sekta ya uvuvi. (Makofi)

Niombe sana Mheshimiwa Waziri sisi Watanzania tunatamani keki iliyo ndogo iweze kuwanufaisha sehemu zote, kwa bahati mbaya sana Mikoa ya Kigoma, Katavi, Rukwa ni mikoa ambayo inapakana na Ziwa Tanganyika na tunapakana na nchi jirani ya Zambia, Kongo na Burundi.

Mheshimwia Spika, mazao yanayozalishwa ndani ya maeneo hayo wanufaikaji wakubwa ni nchi jirani kuliko sisi ambao tuna eneo kubwa sana eneo la ziwa na hiyo ni kwa sababu Serikali haijawekeza kitu chochote ziwa Tanganyika lina kina kirefu na bahati mbaya asilimia kubwa ya mazao yanayotoka kwenye ziwa hili mengi yanapatikana kwa uvuvi ule wa kubahatisha. Tunaiomba Serikali sasa ahadi aliyotoa Mheshimiwa Rais ya kujenga kiwanda kwenye eneo hilo na kuhakikisha wanapeleka zana za kisasa liweze kutekelezwa, kinyume na hapo tutakuwa tuna shuhudia samaki ambao wanakufa ndio unawajua kwamba kwenye ziwa hili kuna samaki wakubwa kama hawa.

Mheshimiwa Spika, niombe Mheshimiwa Waziri aje na maelezo ya kutueleza uwekezaji mkubwa utakaowekwa kwenye Ziwa Tanganyika, tumeshuhudia kila mradi unaokuja kwenye Wizara unaelekezwa ukanda wa Pwani, unaelekezwa ukanda wa Ziwa Victoria na pengine Naibu Waziri anatoka ukanda wa Pwani na Waziri anatoka ukanda wa Ziwa Victoria. (Makofi)

Sasa tunataka watuthibitishie katika Mkoa wa Kigoma, Mkoa wa Katavi, Mkoa wa Rukwa ni mradi upi ambao watakuja kuwekeza kwenye ziwa Tanganyika. Nilikuwa naomba maelezo yatoke ya kutosha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwenye eneo hilo hilo bado tuna mialo ambayo inahitaji kujengwa kwenye ukanda wa ziwa, kwa bahati mbaya sana mialo iliyopo kwenye eneo hilo ni kidogo mno. Nilikuwa naomba maelezo ya Waziri atakapokuja kuhitimisha hoja yake ni lini ataleta mwalo kwenye Kijiji cha Karema, Tarafa ya Karema ambako kuna wavuvi wapo na wanahitaji huduma hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tuna eneo la mifugo; sisi tuna mifugo mingi sana ambayo imetoka Ukanda wa Ziwa iko kwenye Mikoa ya Kigoma, Katavi na Rukwa; tuna idadi ya mifugo mingi sana, lakini hakuna uwekezaji wa aina yoyote ile. Tulikuwa tunaomba atueleze Mheshimiwa Waziri sisi tutakuwa tunapokea tu idadi ya mifugo, lakini miradi ya maendeleo hakuna. Hakuna cha kiwanda chochote hata cha maziwa kilichoko kwenye maeneo hata kidogo, lakini bado wafugaji wanaishi kwenye mazingira ya kuhamahama kwa sababu hawana malisho ya kutosha. Tulikuwa tunaomba atueleze ni lini atatujengea mabwawa; atajenga mabwawa ambayo yatawasaidia wavuvi na wakulima na wafugaji ambao wapo kwenye maeneo hayo ili yaweze kuwasaidia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tunahitaji sana mipango ya masoko ya zao la ng’ombe tuna ng’ombe ambao ukweli wanauzwa kwa bei ya chini mno ni kwasababu hatuna masoko mazuri. Kwa hiyo, tunaomba sana atuhakikishie Mheshimiwa Waziri ana mikakati ipi ya kuimarisha masoko kwenye maeneo ya minada. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Selemani Moshi Kakoso.

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. (Makofi)