Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi na kwa sababu muda ni mfupi nitachangia kidogo na ninaanza kwa kuunga mawazo yote ya Kamati.

Mheshimiwa Spika, Wizara kwa kweli inafikia haiwezi kufanya maajabu bila ya kupata fedha za kutosha na hasa fedha za kutosha za maendeleo kama nilivyosema kwenye taarifa ya Kamati mpaka mwezi Aprili kwa upande wa uvuvi ilipata asilimia 31 tu na miaka yote mitatu iliyopita ilikuwa inapata fedha pungufu kwenye fedha za maendeleo. Kwa hiyo, ninaomba na ninaishauri Serikali iongezee fedha hizi Wizara kusudi iweze kufanya mambo mazuri kwenye uvuvi pamoja na mifugo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo lingine ninalotaka kuongelea ni ufugaji wa kisasa; wananchi wote waelewe kuwa kufuga siyo kuchunga, tuweze kufuga ufugaji wa kisasa Wizara waweze kujikita kutoa elimu ili kusudi tuweze kufuga ufugaji wa kisasa, tuweze kupata maziwa ya kutosha, ng’ombe mmoja anaweza akatoa maziwa lita 32 kwa siku. Nenda mkajifunze kwa mwekezaji wa Iringa yule ASAS ambaye anafuga ufugaji wa kisasa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nikifika hapo naomba Wizara pia iangalie hawa wawekezaji iweze kuwapa mazingira mazuri ya uwekezaji, kwa mfano uwekezaji kwenye viwanda vya samaki, unakuta wawekezaji wengine wanapata shida, uwekezaji kwenye mifugo waweze kuwawekea mazingira mazuri tuweze kupata uwekezaji wa kisasa. Kwa mfano, kwa upande wa maziwa bado tunaagiza maziwa mengi kutoka nje, mimi nashangaa tuna mifugo mingi ni nchi ya tatu Tanzania, lakini bado tunaagiza maziwa kutoka nje. Wizara tuangalie jinsi ya kuboresha maziwa tuweze kuzalisha na kusindika maziwa yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niende tena kwenye Bwawa la Mindu wote mnalijua Bwawa la Mindu pale Morogoro, naomba wale wananchi wawekewe utaratibu mzuri unaoeleweka waache kuvua kwa kujiiba, waweze kuvua kwa utaratibu uliopo kusudi waweze kunufaika na Bwawa hilo la Mindu.

Mheshimwia Spika, nikienda Kilombero kwenye Mto Kilombero sasa hivi Samaki wamepungua zamani samaki walikuwepo wawekee mazingira mazuri kusudi samaki waweze kuzaliana na wananchi wa Kilombero na wa Morogoro waweze kupata kitoga ile waliokuwa wanavua kwenye Mto wa Kilombero. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, uzalishaji wa vifaranga wananchi wengi sasa hivi wamehamasika kufuga vifaranga kwa hiyo iwepo uzalishaji wa vifaranga na elimu kutoka kwa Maafisa Ugani wa Uvuvi ambao sasa hivi ni wachache. Naomba liangaliwe ufugaji huo huo wa vifaranga ili kusudi waweze kupewa wananchi waweze kufuga kwenye mabwawa pamoja na vizimba, uvuvi ni uvuvi mzuri sana kwa hiyo inaweza ika…

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa NARCO naomba matatizo yote yaliyopo kwenye NARCO yaweze kutatuliwa, pia muda wa kupewa vitalu usiwe mwaka mmoja wapewe vitalu kwa muda mrefu kusudi aweze ku-own kwani kitalu chake na aweze akawekeza vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wale wananchi wanaozunguka ranchi hizo hizo waweze kunufaika na ranchi hizo. Nikija kwenye Ranchi ya Kongwa mpaka sasa hivi naomba iangaliwe vizuri kwa sababu sasa hivi imezungukwa na magugu ya Kongwa, hayo magugu ya Kongwa yaweze kutolewa kusudi iweze kuonekana kuwa ni ranchi na wananchi waliozunguka ranchi hiyo waweze kunufaika na vitalu hivyo.

Mheshimiwa Spika, naomba kutoa kuwa masoko kuna masoko vijana wanaweza wakanufaika na masoko kusafirisha wanyama na nyama nje, kwa hiyo waweze kupewa elimu jinsi ya kuweza kuwanufaisha vijana na watu wengine nje bado wanahitaji nyama, bado wanahitaji maziwa kusudi tuweze kunufaika na masoko ya nje. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuimarisha afya ya wanyama…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante sana.

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, namalizia kwa kusema naunga mkono hoja, lakini naomba tasinia hii ya uvuvi na mifugo iangaliwe vizuri inanufaisha wananchi wengi, ahsante sana. (Makofi)