Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa nafasi hii. Kwanza kabisa nianze kuipongeza Serikali yetu na kuishukuru kwamba tunashukuru kwa kutusaidia kutujengea soko la Kimataifa la mifugo na mazao ambalo lipo pale Kakozi ambalo lipo mpakani kabisa kati ya nchi ya Tanzania na Zambia ni kilometa moja tu kutoka Tanzania kuingia Zambia. Soko hili liligharimu karibu, Serikali iliidhinisha pesa karibu bilioni 8.645 na mpaka sasa hivi tumepewa kiasi cha pesa bilioni 3.09. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe kwa kusema hivi kutokana kuwepo kwa soko hili la mifugo na mazao pale ni soko kubwa sana ambalo ninaamini kwamba Serikali wakati inaidhinisha kiwango hiki cha pesa na kutafuta mpango huu mzuri kwamba soko likajengwe pale ni mahsusi kabisa walizingatia kwamba ni kwa sababu tupo mpakani ina maana kwamba tutawahudumia Watanzania wa mikoa yote lakini pamoja na nchi zote ambazo zinatupaka kwenye lile eneo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa basi, ombi langu kwa Serikali, iko sababu kubwa sana Wizara hii iweze kufika kwenye lile soko ambapo tunaendelea na ujenzi japokuwa tunashukuru limeshakamilika kwa kiasi fulani na tumeshaanza kufanyia kazi. Ifike ili tuweze kushauriana muweze kuona miundombinu namna gani tumejipanga katika kuboresha kwenye hilo eneo la ufugaji na eneo lingine ambalo litakuwa linahusu Wizara ya Kilimo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo kwa kuwa soko hili ni kubwa kwa kiwango hiki, naiomba Serikali ipo haja na sababu ambayo tunaweza tutakapoweka kiwanda cha kusindika nyama mahali pale inaweza ikatunufaisha sana. Itatunufaisha sana kwa sababu karibu mikoa yote ya Katavi, Rukwa na mikoa mingine iliyoko karibu nasi ya Nyanda za Juu Kusini na mikoa mingine itaenda kwenda kutumia soko hili kwa sababu kua mnada kabisa wa kisasa ambao unatarajiwa kujengwa mahali pale, machinjio ya kisasa kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa wasiwasi wangu tunaweza, wakati tutakuwa tunafanya shughuli hizi za ufugaji tukawa tunawanufaisha wenzetu wa nchi za jirani. Sasa twende kuongeza thamani kwenye haya mazao ambayo yatatokana na ufugaji. Kwa hiyo, tukipata kiwanda cha kusindika nyama mahali pale, kuna soko kubwa sana la nyama kwenye nchi ya Kongo, Zambia na nchi zote ambazo ziko kwenye zile nchi za SADC. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo liko andiko ambalo nimeziandikia baadhi ya Wizara hapa kuona kwamba kama tuko mpakani na soko lile liko pale mpakani kuna hati hati ya kwamba chochote tutakachokuwa tunazalisha pale kinaweza kikawa kinaenda nchi ya Zambia kinyume na utaratibu. Kwa hiyo, nimeiandikia andiko Wizara ya Fedha, Kilimo, Viwanda na Biashara, Uwekezaji, Mifugo yenyewe na Wizara ya Ulinzi na Usalama kwamba ninaiomba Serikali yangu Sikivu wkae wajadiliane waone kuna umuhimu wa sisi kutupatia geti pale ili tuweze kulinda mapato yote ambayo hayatapaswa kutoka pale kwa sababu soko litakapoanza kufanya vizuri na muingiliano wa watu utakuwa mwingi. Kwa sababu kuna njia zaidi ya 10 ambazo zinaizunguka lile soko ambazo zinatoka pale sokoni kuingia nchi ya Zambia na wakati mwingine huwa tuanzitumia hizo njia kupita ambapo wakati mwingine inakuwa ni kipindi cha Masika, barabara hazipitiki. Kwa hiyo, sitatamani kuona tunaenda kuzinufaisha nchi za wenzetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niingie kwa kuwasemea watu wa Momba kwenye suala la mifugo. Kwenye sensa ambayo ilikuwa imefanyika mwaka 2012 tulionekana tulikuwa na ng’ombe 128,218, mbuzi 78,522, kondoo 10,071 na kuku 155,233 na kwa ajili ya muda pamoja na mifugo mingine. Kwa miaka ya karibuni ambayo imeongezeka sasa tumeonekana kuwa na ongezeko la mifugo hii karibu mara tano kwa sababu tumepokea wenzetu wengi wa Jamii ya wafugaji, Wasukuma na Wamaasai ambao wamekuwepo maeneo yale. Sasa, kutokana na ongezeko hilo, kumeonekana uhitaji mkubwa sana wa kuhitaji malambo pamoja na majosho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikianza na lambo ambalo lilikuwa limeanza kujengwa kwenye Kata ya Mkomba ambapo Shirika hili la Debit kwenye mwaka 2016/2017 liliweza kutupatia kiwango cha pesa milioni 150 ambapo lambo hili lilikuwa linapaswa kukamilika kwa thamani ya milioni 800. Ombi langu kwa Serikali, kama mnaweza kufika, kupitia na kuliona lambo hili ili tuweze kuwasaidia wafugaji hawa wasiendelee kunung’unika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hayo yapo baadhi ya malambo ambayo yalikuwa yanatumika, lakini hayana ubora na yanahitaji kurekebishwa kwa sababu ongezeko la wafugaji limekuwa kubwa mara tano kama ambavyo nimesema. Naomba ukarabati wa malambo yafauatayo; lambo ambalo liko Kata ya Ivuna, Mkomba, Mpapa, Chitete, Msangano. Pia ombi langu kwamba kama tunaweza tukapata majosho kwenye Tarafa ya Ndalambo ambayo pia kwenye Bonde la Mto wa Kasinde pamoja na Tesa kuna ongezeko kubwa sana la watu hawa ambao ni wafugaji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hayo kwenye suala la ufugaji tunaomba kuboreshewa vifaa vya uimarishaji ili kwa ajili ya kuboresha koo za mifugo ambazo ziko pale. Hii imeonekana ni changamoto lakini na vifaa vya hawa Maafisa Mifugo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye eneo la uvuvi naomba niende tu moja kwa moja niziongelee changamoto ambazo zinawapata wavuvi ambao wako ndani ya Jiji la Momba. Wavuvi ambao wako ndani ya Jimbo la Momba wanaomba jambo moja kama sio matatu au manne. Tunaomba tupate engine za boti kwa sababu mpaka sasa tunaendelea kuvua kwa kutumia uvuvi wa kienyeji kwa kutumia tu mitumbwi. Kwa hiyo, tukipata engine hizi tutaweza kutengeneza maboti ambayo angalau yanaweza yakawa ni ya kisasa.

Mheshimiwea Mwenyekiti, pia tunaomba kupata mikopo kwa wavuvi. Pia tunaomba kupata soko zuri ambalo liweze kutusaidia kuweza kukusanya mapato ndani ya halmashauri pia kukusanya mapato kwenye Serikali Kuu. Kwa sababu, pamoja na kwamba tunavua kienyeji, tunaweza kuvua kuanzia tani 7,000 mpaka tani 100,000 na pamoja na kuvua huku, tunalitosheleza soko la Mbeya Mjini, Tunduma, Vwawa na Mlowo. Kwa hiyo, tutakapokuwa tumepata hivi vifaa tunaweza kuzalisha tani kubwa na kwa wingi lakini pia tutaongeza mapato ndani ya halmashauri yetu pamoja na mapato kwa Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema haya, naunga mkono hoja. (Makofi)