Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. CHARLES J. P. MWIJAGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipatia fursa hii ya kuchangia sekta hii muhimu.

Mheshimiwa Spika, kabla sijaanza kuchangia rasmi, nitumie dakika moja kuliweka sawa jimbo langu. Kama inavyojulikana, mimi ninazo square kilometers 7,000 ambazo ni maji na nina Kata tatu za visiwani. Nitumie fursa hii kuwaomba wananchi wa Bumbile hasa Iyumbo, mtulie. Mamlaka ya TASAC imewazuia wananchi wetu wasipande mitumbwi kwenda kwenye Mwalo wa Kamugaza kwa sababu haujajengwa gati, mtulie. Nimemjulisha Waziri mwenye dhamana, nimemjulisha Mwenyekiti wa Sekta. Sijapata pesa za kujenga gati, lakini nitaomba hata kuuza mali zangu, nitajenga gati. Shida zangu na wananchi wangu nazijui mimi, mwenye shibe hamjui mwenye njaa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mkurugenzi Mkuu wa TASAC ana shibe yake na wasaidizi wake wana shibe zao, mimi nafanya kazi na Waziri na ikishindikana nitakuja kwako Mheshimiwa Spika. Mwenye shibe hamjui mwenye njaa. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, naanzia ulikoishia juzi. Juzi wakati tunahitimisha Wizara ya Kilimo, ulitoa mahitimisho mazuri na haya yalitokana na michango mizuri ya Waheshimiwa Wabunge, lakini zaidi mzungumzaji wa mwisho, Mheshimiwa Balozi Dkt. Kakurwa. Katika mahitimisho tulikubaliana wote kwamba sasa hatuwezi kwenda na mwendo huu, ila tunapaswa kuchupa. Ukarejea, tulipofanya mageuzi makubwa katika sekta ya nishati na sekta ya miundombinu. Kwa ruhusa yako nami uniruhusu nianze hapo.

Mheshimiwa Spika, katika Dira yetu ya Taifa 2020 - 2025, tuna mipango mitatu ya miaka mitano. Mpango wa Kwanza dhima yake ilikuwa kuondoa vikwazo, tulipambana. Mpango wa Pili, dhima yake ilikuwa ujenzi wa uchumi wa viwanda ili kuchochea mageuzi ya kiuchumi na maendeleo ya watu. Mpango wa Tatu ni kujenga uchumi shindani na viwanda kwa maendeleo ya watu. Kumbe tulikuwa tunafanya nini? Dhima ya kwanza tulikuwa tunajenga msingi; dhima ya pili, tukanyanyua boma na dhima ya tatu ni finishing. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sisi Wabunge wa Bunge la Kumi na Mbili tunahusika kwenye finishing. Finishing ya kufanya nini? Kuipeleka nchi hii ifikapo 2025 watu wawe na kipato, waondokane na umasikini, wawe na income per capita ya dola 3,000. Ama wasifike, angalau wafike Dola 1,700 kama alivyosema Mheshimiwa Prof. Muhongo. Pia tuwe na uchumi imara na shindani.

Mheshimiwa Spika, nizungumze la muhimu, siyo hiyo income per capita ya 3,000 ila muhimu ni uchumi jumuishi. Sasa unapotaka kwenda uchumi jumuishi, ni sekta za kiuzalishaji ambazo ndizo zinaweza kukupeleka kwenye uchumi jumuishi. Unaweza kuzidiwa mafuta, dhahabu, ukawa na income per capita kubwa, lakini kuna watu wanakula vumbi barabarani. Kumbe ukiimarisha kilimo, mifugo na uvuvi, ndipo unaweza kwenda kwenye sekta ambayo italeta uchumi jumuishi kwa Watanzania wote. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, siendi kwenye takwimu kwamba bajeti ni ndogo, hapana. Iwe kubwa ifanye nini? Nataka kuchupa. Bahati mbaya, tujifunze kwa wadogo zetu, lakini siyo bahati mbaya wadogo zetu ni rafiki zetu. Tujifunze Uganda, tujifunze Rwanda. Katika nchi zinazofanya vizuri kwenye mifugo Afrika, ni Mali, Ethiopia, South Africa na Uganda.

Mheshimiwa Spika, Uganda wanauza maziwa na bidhaa za maziwa nje na wanapata Dola milioni 100 kwa mwaka. Tanzania hatupati hata senti 50. Ukiuliza kwa nini? Wanasema ni sera. Kumbe siyo bajeti, kinachotangulia ni sera.

Mheshimiwa Spika, nikishamirisha ule mkakati wako wa kuchupa, tunapaswa tuanze kwa kubadilisha mindset ya ufugaji wetu, tutoke kwenye uchungaji twende kwenye ufugaji. Kwa hiyo, sera ninayoitaka ni sera ya kuwachukua hawa watu; kwa sababu nawasikia watu wanavyochangia. Watanzania na Wabunge walio wengi, hawataki uchumi wa kuwapeleka wachache juu na kuwaacha wengine. Mimi nakuwa makini ninapokuwa nachangia na ndugu yangu Mheshimiwa Balozi Dkt. Bashiru. Yaani ukileta sera ya kuwaacha walio wengi, unaona anaumia kweli. Kwa hiyo, sera inayotakiwa ni ya kuwachukuwa walio wengi.

Mheshimiwa Spika, ukiangalia, dairy industry ya Uganda, imechangiwa na wananchi walio wachache, lakini Serikali ya Uganda ilikopa pesa nyingi na kulikamata lile eneo lililofanya vizuri na kuwekeza pesa pale. Ndiyo ikafanyika local farming, ikafanya vizuri.

Mheshimiwa Spika, Uganda wanachakata maziwa lita milioni 2.8. Nilipokwenda Uganda ku-understudy, ile nafika walijua najua nakuja ku-understudy. Wakanieleza mambo yote, lakini wakasema Tanzania mna uwezo wa kuzalisha na kuchakata lita milioni nne. Nikasema mnajuaje? Wakasema habari zenu tunazijua. Mnaposema Tanzania nasi tunazalisha lita milioni 2.8, hoja siyo kuzalisha, hoja ni kuzichakata ili zifike kwa mteja. Unaposema unajenga uchumi wa Taifa, ujenzi wa uchumi wa Taifa ambao ni shindani, lazima uwe na kiburi cha kuuza. Hatuuzi nje. Tuna hali mbaya kwenye maziwa. Sasa tunachopaswa kufanya ni kukamata watu kuwafundisha njia mpya za kufuga kama walivyofanya Uganda.

Mheshimiwa Spika, watu wamezuiwa mambo ya kuhamahama; ndama anazaliwa Muleba, akija kuchinjwa ameshafika Lindi. Huyo ng’ombe ukimchinja, wastani wa kilo ni 100. Leo hii katika jimbo la Mheshimiwa Bashungwa kuna ndama wa miezi 18, ukimchinja unapata kilo 600. Waziri ulimwona, Katibu Mkuu wako alimwona na Wabunge niliokuwa nao; na Mheshimiwa Balozi Dkt. Bashiru alimwona na akaweka sahihi nikaiona sahihi yake. Tunapaswa kuipeleka sekta hiyo, ndipo tutakapoweza kuchukua walio wengi na kwenda kwenye level hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nizungumzie NARCO. Waziri ameizungumza vizuri kwamba asilimia 20 ya NARCO ndiyo ranchi ambazo wanazimudu na kuweka ng’ombe hao. Katika kuchupa, nitoe ushauri kwa NARCO; ubaki na eneo la asilimia 20 uache kupangisha. Haya maeneo unayopangisha uwaachie Halmashauri na Waziri wa Ardhi wawapangie wananchi. Nitapendekeza tuje na kitu kinaitwa Livestock Development Authority ambayo itakuwa na idara ya maziwa na idara ya nyama, kusudi ninyi sasa muwe mna-regulate na kuwaambia watu pasture ziko vizuri, pasture zinakwenda namna hiyo ili tuweze kuhakikisha kwamba sekta ya mifugo na sekta ya uvuvi zinachangia pato la Taifa zikiwa za kwanza.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Kaguta Museveni aliniambia, kufika 2022 kama sekta ya maziwa haitakuwa namba moja Uganda, Waziri anapoteza kazi. Leo maziwa ni sekta ya pili baada ya kahawa ukiondoa dhahabu, katika kuchangia uchumi wa Uganda. Waziri wa Mifugo (ni mjomba wangu) aliniambia kwamba 2022 maziwa yatakuwa yanaongoza. Sasa na sisi Taifa tujiwekee mpango kwamba samaki tuta-export kiasi gani? Maziwa kiasi gani? Sisi aibu tumezizoea, hata kwenye samaki; nusu ya Ziwa Victoria ni la Tanzania lakini Uganda wanatuzidi kwa ku-export samaki. Yaani unapata aibu, unakuwa mjinga mpaka unazoea ujinga. Sasa tuchupe. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Spika, nakimbilia kwenye maamuzi yako kwamba tuchupe, hii hali tuliyomo siyo ya kwetu. Sina shida na bajeti, uwasilishaji mzuri, lakini hii tunaitumia kama maandalizi ya kuweza ku-take off na kuchupa kwenda kwenye anga tunazostahili zenye kipato kikubwa cha watu walioshikamana wenye utulivu, amani na utawala bora tulionao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha. (Makofi)