Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pongezi kwa Waziri wa Viwanda, Mheshimiwa Charles Mwijage, Mbunge na uongozi wote wa Wizara. Pongezi za pekee kwa Katibu Mkuu kwa hotuba nzuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na suala la kufufua viwanda. Naomba Serikali ifufue Kiwanda cha Nyuzi Tabora kwani kiwanda hicho ni cha zamani, pia ni mitambo ya kizamani ambayo imepitwa na wakati. Ni vema Serikali ikamshauri mwekezaji kuagiza mitambo mipya ya kisasa. Serikali ikajiridhishe kuona kama kweli mitambo ipo, isiwe wameihamisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukarabati wa majengo yaliyojengwa na Serikali ambayo alipewa mwekezaji ameshindwa hata kukarabati, ni vema apewe mwingine. Kukosekana kwa viwanda Mkoa wa Tabora ni kuongeza ugumu wa maisha kwa wakazi wa Mkoa wa Tabora, kusababisha ongezeko la uhalifu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Kiwanda cha Maziwa, niiombe Serikali kuwawezesha wawekezaji wa ndani ambao uwezo wao ni mdogo kimtaji kama vile mwekezaji anayemiliki Kiwanda cha Nyamwezi. Kukosekana kwa mitaji hiyo, pia kumechangia kufungwa kwa kiwanda hicho mara kwa mara, pia kufanya wafugaji kukosa mahali pa kupeleka maziwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali kutafuta wawekezaji ambao wanaweza kuweka kiwanda cha kusindika asali kwani Tabora ni centre ya mikoa jirani ambayo nayo wanayo asali kwa wingi kama vile Katavi, Singida na Kigoma. Hivyo basi, ni rahisi kwa mwekezaji kupata mahitaji ya kiwanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Kiwanda cha Tumbaku, naishauri pia Serikali kuleta wawekezaji Mkoa wa Tabora ili zao la tumbaku lisindikwe kwa urahisi na kuondoa usumbufu kwa wakulima. Pia wananchi wa Mkoa wa Tabora kupata ajira na mikoa jirani kuliko ilivyo hivi sasa ambapo mazao yote hupelekwa Morogoro.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iweke nguvu zote kwa kuwezesha bajeti ya viwanda vidogo vidogo (SIDO) kupewa fedha za kukuza uchumi kwa wajasiriamali, kwani SIDO imefanya kazi kubwa hapa nchini, imefanikisha kutoa elimu kwa wananchi wengi hapa nchini kwa kada mbalimbali hasa wanawake. Ofisi za SIDO zipewe vitendea kazi kama vile magari, vifungashio vya elimu ambavyo hujifunzia wajasiriamali hapa nchini.
Ombi langu kwa Serikali isaidie kiwanda cha SIDO ambacho hutengeneza sabuni, kusindika karanga, pia mikopo midogo midogo kilichopo Tabora; tumbaku ipewe kipaumbele kwa kutafuta wawekezaji kwani hulimwa Mkoa wa Tabora kwa 60%. Naunga mkono hoja.