Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Hon. Edwin Enosy Swalle

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

MHE. EDWIN E. SWALLE: Mheshimiwa Naibu Spika, natoa ushauri kwa Serikali kuwa itoe ajira za kudumu kwa Wenyeviti wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba Wilaya. Msingi wa hoja hii ni kuongeza uhuru wa Mabaraza haya, (independence of the tribunals).

Mheshimiwa Naibu Spika, ni maoni yangu kuwa kitendo cha kuajiri Wenyeviti hawa kwa mikataba ya miaka mitatu, mitatu ni kumweka Mwenyekiti katika hali ya kukosa uhakika wa ajira. Kwa mfano, Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania wamepewa security of tenure ili kulinda uhuru wa Mahakama. Maisha ni ardhi, ardhi ni mali. Hatuwezi kulinda mali muhimu ya wananchi ambayo ni ardhi inayosimamiwa na kuamuliwa na mtu ambaye hana uhuru, freedom ya ajira yake.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naunga mkono hoja.