Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

Hon. Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Spika, kwanza nikushukuru nichukue nafasi hii kukushukuru kabisa kwa kunipa nafasi kuchangia Wizara hii nyeti. Lakini pia nachukua nafasi hii kumshukuru Waziri, Naibu Waziri Pamoja na watendaji wote wa Wizara wakitambua kwamba wanaongoza Wizara ambayo ni mtambuka ni Wizara ambayo katika sekta ni Wizara toka tunapata uhuru tunazungumzia Wizara ya Kilimo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ni Wizara ambayo ukitaja sekta zingine zote unaweza ukasema zimeanza baada ya Wizara hii ya Kilimo. Lakini nichukue nafasi hii kuwapongeza kwa kazi kubwa mnayoifanya changamoto ni nyingi wakati mwingine kuzimaliza kwa muda mfupi yawezekana isiwe kazi ya rahisi lakini tuna imani kwa sababu sasa tumempata Waziri kijana ambaye ni Professor, tumempaka Naibu Waziri kijana ni imani yangu sasa mtakwenda kubadilisha kilimo kutoka kwenye nadharia sasa iende kwenye vitendo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ni imani yangu kwamba kwa miaka yote toka uhuru hakuna ambacho hakijawahi kuandikwa kwa maana ya research kama utafiti kwenye zao lolote la kilimo nchi hii. Kazi kwenu sasa kwenda kutumia research zilizoandikwa na wataalamu hao ili sasa kutumia nafasi zenu za vijana muiondoe nadhania hii ya kilimo ambayo imekuwa ikizungumzwa na wananchi na Pamoja na Waheshimiwa Wabunge iende kuwa vitendo.

Mheshimiwa Spika, lakini Wizara hii haiwezi kufanya mazuri kama haina fedha angalia tazama bajeti tunayoijadili sasa ni bilioni 2.9 kama haitaenda yote maana yake haya tunayozungumza ukiacha nje ya mifumo hii ambayo Wabunge wamekuwa wakilalamikia, maana yake bado haiwezi kufanya vizuri vile ambavyo wananchi wanahitaji. Nichukue nafasi hii kuiomba sana Serikali hii bilioni 2.9 iliyoombwa na Wizara hii wapeni yote ili angalau tunaporudi bajeti ya mwakani tuweze sasa kushikana mashati sawasawa tukiwa tumewapa fedha sasa za utekelezaji na uendelezaji wa utekelezaji wa Wizaa hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nizungumzie maeneo yangu mawili ndani ya jimbo langu eneo la kwanza ni eneo la kilimo cha umwagiliaji mradi wa Chereche nilikuwa naangalia taarifa ya Mheshimiwa Waziri hotuba yake na randama sijaona ikitajwa. Chereche ni mradi ambao wa umwagiliaji una heka Zaidi ya 350 unahudumia zaidi ya wananchi ambao walikuwa wakifanya shughuli pale Zaidi ya watu 300 na kitu.

Mheshimiwa Spika, mradi huu wa umwagiliaji umeanza toka mwaka 2002, lakini toka mwaka 2018 umesimama una miaka minne tunakwenda miaka mitano umesimama na haufanyikazi yoyote unaweza ukaona wananchi waliokuwa wanafanya shughuli za kiuchumi pale mpaka leo wanaenda wapi. Lakini nimeangalia kwenye bajeti humu nilikuwa naangalia kwenye taarifa ya Mheshimiwa Waziri haupo tuna mradi wa umwagiliaji upo Kijiji cha Rabol Kata ya Rabol, Tarafa ya Loimbo una zaidi ya heka 250 kwa mara ya kwanza Serikali iliamua kufufua mwaka 2012 kwenda mwaka 2013 wakaitengea bajeti 2016 kwamba sasa tunakwenda kuufufua huu mradi ili uwanufaishe wananchi wa maeneo yale Kijiji cha Loimbo. Hivi ninavyozungumza mpaka leo ile bajeti 2016 haikwenda kwenye utekelezaji nimeangalia kwenye bajeti ya Serikali bajeti ya Mheshimiwa Waziri haimo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pia tuna mradi wa umwagiliaji Ochuna wananchi wanalima mpunga kule ni mradi wa umwagiliaji ambao wananchi masikini ya Mungu wanahangaika lakini wanachangamoto zao za miundombinu ndani ya ule mradi haipo ni imani yangu Mheshimiwa Waziri atakapokuwa amesimama kesho kufanya majumuisho aniambie na kwa sababu nimekwisha zungumza naye kabla ya hapa haina haja ya sisi tena kurudi kule na wakati ninaye Waziri ndani ya Bunge hili. Atoe tamko na atoe maelekezo wale watendaji wote ambao wamesahau kuingiza kwenye bajeti ili angalau sasa nitakaporudi na mimi Jimboni nirudi nikijua hawa wananchi wanatokaje hapa na wanakwendaje. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana na naomba niunge mkono hoja. (Makofi)