Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

Hon. Ally Anyigulile Jumbe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Kilimo

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kupata nafasi hii mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni ume-set standards na sisi ni wanafunzi wako na hata tunapochangia tunajua tuko na mlinzi wetu ambaye ni wewe na sisi tutakulinda. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sitachangia kwa hasira kama alivyofanya Mheshimiwa Mlugo na Mheshimiwa Tabasamu na wengine kwa sababu ninataka leo liwe ni fundisho tujifunze tusome tujue vizuri maeneo yetu tunakotoka.

Mheshimiwa Spika, nitaongelea mfumo wa pili aliousema mchangiaji wa kwanza Mheshimiwa Mhagama mfumo wa Stakabadhi Ghalani na nitahusianisha mfumo huu na zao lililoko Kyela zao la kokoa ambalo ni zao kati ya mazao muhimu yaliyowekwa katika mfumo wetu wa mazao saba Tanzania hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mfumo huu pia hata ulivyoingizwa Wilayani Kyela uliingizwa kwa ubabe hakuna aliyefanya utafiti hakuna aliyezungumza na mkulima kilichofanyika ni kwamba leo tunazungumza kesho makampuni yote yasinunue kokoa. Ilikuwa ni kitendo cha ukatili na kuna makampuni yalipoteza pesa zao. Ukiuliza wanakwambia Serikali imesema Serikali ni nani kama siyo sisi wananchi? Ndugu zangu hili lilifikia hatua ya kutuparang’anya wana Kyela tulifikia hatua ya kuanza kuichukia Serikali lakini ilikuwa ni kwa sababu ya watu wachache.

Mheshimiwa Spika, cocoa ni zao ambalo ni tofauti na mazao mengine yaliyoko Mtwara kama korosho ambayo yanalimwa kwa msimu. Kokoa inalimwa kwenye vivuli sisi Wanyakyusa zao la cocoa ni zao la heshima kuwepo nyumbani kwako. Zao lile hatulimi porini maana yake ni nini? Maana yake ni kwamba huwezi ukachukua mfumo unaotumika kwenye zao la korosho ambalo ni la msimu ukaja kwenye mfumo huo ukauleta kwenye cocoa ambayo inachumwa kila siku kwa msimu na kila mtu anaokota kidogo kidogo.

Mheshimiwa Spika, kilichotokea mfumo wa korosho ukahamishiwa kwenye mfumo wa cocoa matokeo yake ni kwamba wale wote waliokuwa wananunua cocoa makampuni yote yalipoteza pesa zao na hata walipokubali kilichofuata ni kwamba wale wote ambao walikuwa wananunua cocoa hizo walishindwa kuendelea na biashara kwasababu wengi pia walifikia kufilisika na kampuni mojawapo ni Baoland ambao mpaka sasa hivi hawanunui kokoa Kyela.

Mheshimiwa Spika, hili zao kwetu huwezi ukamfanya mtu asubiri kila mtu anachuma siyo zaidi ya kilo tano kwa wiki ukisema huyu mtu anayechuma kilo moja asubiri aziandae cocoa ndani ya siku tano kama kuna jua lakini apeleke mnadani akishapeleka mnadani anatakiwa kusubiri mwezi mzima ndipo apate pesa sasa wewe elfu 30 unaisubiri mwezi mzima kwa kweli haiingii akilini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa kinachotokea hawa watu wanashindwa kusubiri tumetengeneza tabaka la wanunuzi wa kati ambalo limejitengeneza automatically kwenye mfumo badala ya kununua kuuza hizo cocoa kwa shilingi elfu nne watu wanauza cocoa hizo kwa shilingi elfu tatu, na ni kwanini kwa sababu cocoa yao siyo cocoa kwa ajili ya kupata utajiri cocoa ya Kyela ni kwa ajili ya matumizi ya kila siku mtu anataka auze cocoa akamtibu mtoto, mtu anataka kuuza cocoa apeleke school fees kwa mtoto, anataka auze cocoa abadilishe mboga halafu auze cocoa angalau jioni akakae na wenzie anywe bia ndiyo kazi ya cocoa sasa leo unapomwambia mtu asubiri inashindikana.

Mheshimiwa Spika, sasa ninaomba niseme mambo machache ambayo ninaomba sana Serikali inisikilize hili zao katika dunia hii kokoa iliyopo Kyela ndiyo hamira ya cocoa inayotoka Ivory Coast, cocoa inayotoka Ghana kwa ubora kokoa yetu inaongoza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, na kuna fununu…

SPIKA: Dakika moja ya kumalizia

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE: Naunga mkono hoja.