Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Martha Festo Mariki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. MARTHA F. MARIKI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha mchango wangu wa maandishi katika wizara hii ya Ulinzi.

Kwanza napenda kuipongeza Wizara hii kwa kazi kubwa inayoifanya kwa kuhakikisha Taifa linakuwa salama muda wote. Tunatambua uzalendo wao kwa Taifa hili na sisi kama wawakilishi wa wananchi tutakuwa nao bega kwa bega.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pamoja na pongezi hizo tuna changamoto katika Mkoa wa Katavi wa mgogoro baina ya jeshi na wananchi wa Mpanda Manispaa.

Mheshimiwa Naibu Spika, mgogoro umekuwa wa muda mrefu sana, namuomba sana Mheshimiwa Waziri kupitia Serikali watoe tamko kwani wananchi hao wamekuwa wakifanya shughuli za maendeleo katika maeneo hayo kwa muda mrefu kutokana shughuli za jeshi katika eneo hilo imesababisha mgogoro na wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sana Serikali itoe tamko ili wananchi wajue hatima yao kwani mpaka sasa wananchi hawajui nini hatima ya mgogoro huo.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.