Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Lucy Thomas Mayenga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. LUCY T. MAYENGA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa nianze kwa kushukuru kwa kunipatia nafasi hii, ninajisikia furaha na fahari kubwa leo kwa mara ya kwanza katika miaka yangu yote ambayo nimekaa Bungeni ninasimama hapa kuchangia Wizara hii ikiwa chini ya Amiri Jeshi Mkuu mwanamke. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba Watanzania wote kwa ujumla wetu tumpatie zawadi kubwa moja tu Mheshimiwa Amiri Jeshi MKuu, ni tulitaje jina lake kwa wema popote tulipo ili aweze kupata moyo wa kufanya kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niipongeze sana Jeshi letu, Jeshi hili limetuheshimisha watanzania kwa muda mrefu sana jeshi hili limekuwa likifanya kazi nyingi sana, licha ya kazi ambazo ziko kwenye Katiba yetu kisheria, lakini limekuwa likifanya kazi nyingi sana kwenye jamii yetu kwa maana hiyo na limekuwa likituheshimisha sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini sio tu kwenye nchi yetu, Jeshi hili limekuwa likifanya kazi kubwa sana na zipo kihistoria, zipo nchi ambazo haziwezi kuelezea mafanikio waliyonayo ya uhuru wao bila kutaja mchango wa Jeshi la Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, baadhi ya maeneo mbalimbali katika nchi hii au nje ya Tanzania yamekuwa yana matatizo kadhaa, lakini Jeshi hili limekuwa likienda, matatizo yao yanakwisha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nizungumzie kwa kifupi kuhusu suala zima la mchango wa jeshi letu katika operation za amani duniani, jeshi hili limekuwa likishiriki katika operation za amani katika nchi mbalimbali. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hivi sasa kama ambavyo tunafahamu wapo Lebanon, wapo Darfur, wapo Congo na kadhalika. Kazi wanayoifanya kule ni kubwa sana na kwa kweli mimi ningeomba jeshi hili kazi hii iendelee kwa sababu inawapa exposure na ni faida kwao pia kiuchumi kutokana na posho wanazozipata. Lakini pia vilevile jeshi hili wanajeshi hawa wanapokwenda kule wanakuwa pia na nafasi ya kujipima uwezo wao pamoja na majeshi mengine ya nchi mbalimbali. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwasababu kazi hii inafanywa chini ya Umoja wa Mataifa, kuendelea kwa jeshi letu kuaminika kwa wanajeshi kupelekwa huko kwa kweli ni sifa kubwa sana na wanastahili pongezi kubwa sana. Lakini kwenye hili mimi nilikuwa naomba, ninaomba Mkuu wa Majeshi Mabeyo, kaka yangu kwanza nikupongeze kwa kazi nzuri sana. Mimi nilikuwa naomba kwenye operation hizi idadi ya wanawake iongezwe, wanawake wanaweza, leo tumeona akinamama…. (Makofi)

MHE. RIDHIWANI M. KIKWETE: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

MHE. LUCY T. MAYENGA: Mheshimiwa Naibu Spika, pale wamechafuka mabegani, akina mama wanaweza. Kwa hiyo mimi nilikuwa naomba kwamba kwenye…

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Lucy Mayenga, kuna taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Ridhiwani Kikwete.

T A A R I F A

MHE. RIDHIWANI M. KIKWETE: Mheshimiwa Naibu Spika, mimi naomba nimpe taarifa tu dada yangu tunapo mu-address Mkuu wa Majeshi hatumwiti kwa jina lake, yule anaitwa General Mabeyo. Ahsante sana. (Makofi/Kicheko)

NAIBU SPIKA: Haya sasa kwa sababu Mheshimiwa Lucy Mayenga anachangia Kiswahili basi ni Jenerali. (Makofi)

MHE. LUCY T. MAYENGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninaipokea taarifa hiyo kwa mikono miwili kabisa Jenerali Mabeyo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini baada ya kazi hizi ambazo zimekuwa zikifanywa nje ya Tanzania pamoja na hapa kwetu Tanzania, sina budi kutoa pongezi kwa jeshi letu kwa kazi kubwa sana ambayo wameifanya Kibiti. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba niwapongeze kwa sababu kazi ile kwenye masuala ya kivita, mimi sijawahi kuwa mwanajeshi wala sijawahi kuwa askari, lakini ninafahamu kwamba conventional war ni tofauti sana na gorilla war; aina ya mapigano na hali iliyokuwepo kule Kibiti, ilikuwa inafanana sana na gorilla war; humjui adui yako lakini kazi iliyofanyika ni kazi kubwa sana na ninaomba kwenye hili pia ili na sisi Tanzania tuendelee kuwa na amani kwa sababu inavyoelezwa ni kwamba wale magaidi wametoka sasa kwa upande wa Tanzania wamehamia kwa majirani zetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini Tanzania na Msumbiji au na hizi nchi zingine ambazo tuko nazo majirani Tanzania na Msumbiji hasa ambako ndio inasemekana kwamba wamekwenda kule tuko karibu sana. Kwa hiyo, ina maana kwamba na sisi tusipojiimarisha wasije tena wakaona kama tumelala lala wakarudi. Nilikuwa naomba tuongeze msimamo, tuongeze kazi, tuongeze nguvu kama ambavyo ilivyo. Na kwenye hili, ninaomba niendelee kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa kuendelea kuteua watu ambao wakiwepo kwenye maeneo kama haya strategically wataweza kutusaidia. Kwa sababu hawa ni watu ambao wana mafunzo ya hali ya juu wanajua wanachokwenda kukifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nitoe pongezi zangu kwa kulingana na seniority ya wanajeshi naomba niwapongeze sana Jeshi la Nchi Kavu, naomba niwapongeze sana Jeshi la Anga, naomba nipongeze sana Jeshi la Wanamaji pamoja na JKT, kwa kazi hii kubwa ambayo walikuwa wameifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini licha ya kuelezea kwamba wanajeshi hawa wamekuwa wakifanya kazi kubwa sana, mimi niwaombe with due respect kwamba kuna kitu ambacho kilikuwa kinatolewa kwa wanajeshi wetu kama motisha, kwa maana ya yale maduka ambayo yalikuwa yana duty free ya Jeshi. Lakini pia vilevile, mess ambazo zilikuwa zinaendeshwa katika utaratibu wa duty free kwa maana ya vinywaji na kadhalika.

Mheshimiwa Naibu Spika, hawa wanajeshi wanapokuwa wanakaa pamoja kwenye maeneo kama haya ya mess na kadhalika wanakuwa na cohesion lakini pia hii ni organizational culture, dunia nzima hivi vitu vipo. Sasa mimi nilikuwa naomba tukikaa tukasema kwamba labda pengine kuna either kubana matumizi au kwa njia moja au nyingine ile hali ambayo ilisababisha tukaondoa hivi vitu, mimi nilikuwa naomba tufanye tathmini kama ilikuwa kuna dosari dosari, ubadhirifu na kadhalika kwenye vitu kama hivi tujaribu kuangalia tena upya ili kama ikiwezekana tuweze kuwarudishia kwasababu hivi ndio vitu ambavyo vinawapa motisha wanajeshi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ninafahamu kwamba jeshi letu limekuwa likitoa huduma mbalimbali kwa wananchi wetu, hasa katika maeneo ambayo yamekuwa yakikabiliwa na majanga lakini pia vile vile yamekuwa yakikabiliwa na matatizo mbalimbali wakati wa dharura.

Nilikuwa naomba kutoa ombi Mheshimiwa Waziri wetu wa Ulinzi Mheshimiwa Kwandikwa ambaye anafanya kazi nzuri sana, nilikuwa ninaomba Mheshimiwa Waziri wetu na ninafahamu kwamba ni msikivu uweze kutusaidia katika Mkoa wetu wa Shinyanga yapo maeneo katika Wilaya mbalimbali Wilaya ya Kishapu, Wilaya ya Shinyanga Mjini, Wilaya ya Kahama, Majimbo yote pamoja na kwako Ushetu, kumekuwa kuna matatizo mengi sana sana sana, pia Wilaya ya Shinyanga Mjini na kadhalika kumekuwa kuna matatizo ya uharibifu mkubwa wa miundombinu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nafahamu kwamba masuala ya miundombinu yako kwenye Wizara ya miundombinu, lakini tunajua pia kwamba mchakato wa ujenzi wa madaraja kwenye maeneo mbalimbali huwa sio kitu cha mara moja.

Mheshimiwa Naibu Spika, nilikuwa nakuomba sana Mheshimiwa Waziri uweze kutusaidia uwepo wa madaraja kwa mfano kwa kwetu Shinyanga Mjini kuna Upongoji ambayo linaunganisha Ndala na Masekelo kuja Shinyanga Mjini, kuna Ibinza Mata ambayo inakwenda Kitangiri, kuna Uzogole kwenda Bugwandege, kuna Old Shinyanga kwenda Mwamalili na kadhalika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wetu wamekuwa wakipata shida, nilikuwa naomba haya madaraja ya muda ambayo mnayo basi muweze kukaa chini kuweza kuangalia ni jinsi gani mnaweza kuja kutusaidia. Ndugu zangu kwenye maeneo haya ambayo nimeelezea hali huwa ni mbaya, wananchi wanasombwa na maji, magari yanasombwa na maji, hali huwa inakuwa mbaya sana. Kwa hiyo, nilikuwa nakuomba sana Mheshimiwa Waziri muweze kuliangalia hilo na ninafahamu kabisa kwamba hili ukilikalia vizuri litawezekana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini la mwisho nilikuwa nataka kuzungumzia kuhusu suala zima la teknolojia. Wote tunafahamu kwamba, dunia inabadilika naomba tu kuelezea kwa kifupi, kuna kitu kinaitwa high tech. warfare naomba kuuliza, are we ready?

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo ahsanteni sana kwa kunisikiliza. (Makofi)