Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Saada Mansour Hussein

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. SAADA MONSOUR HUSSEIN: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana na nakushukuru kwa kunipa nafasi hii na mimi kuchangia. Kwa vile ni mara yangu ya kwanza kusimama katika Bunge hili tukufu, nakishukuru Chama changu cha Mapinduzi kwa kuniteua. Pia nawashukuru Umoja wa Wanawake wa Tanzania Taifa (UWT) pamoja na wanawake wa Mkoa wa Kaskazini Unguja kwa kuniamini ili niwe mwakilishi wao. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchangia umuhimu wa Hospitali ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania iliyopo Bububu kuboreshwa. Hospitali hii ni muhimu kwa kuwa ndio hospitali kubwa ya jeshi ndani ya Zanzibar, hivyo ninashauri Wizara ya Ulinzi iongezewe fedha kwa ajili ya kuongeza majengo na vifaatiba.

Pia ninashauri Wizara hii ijengewe majengo maalum ya kutoa huduma kwa viongozi wetu wa Kitaifa pale wanapoumwa. Hospitali nyingi za binafsi za Zanzibar na za Serikali hazina faragha za kutosha kwa matibabu ya viongozi, hivyo majengo hayo yakiwepo yatarahisisha huduma na kuwa kimbilio kwa viongozi na wananchi kwa ujumla. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, Wizara ya Ulinzi haina jengo la Wizara ndani ya Zanzibar, Wizara hii ni ya kimuungano, hivyo ninashauri iwe bajeti hii ama bajeti ijayo Serikali ianze mchakato wa kuanzisha ofisi ya jengo la Wizara ndani ya Zanzibar. Ofisi hiyo itasaidia shughuli za Wizara ndani ya Zanzibar ikiwemo kutoa huduma kwa urahisi kwa askari wetu wa JWTZ wanapotaka huduma za kiwizara.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hayo machache naunga mkono hoja. (Makofi)