Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Agnes Mathew Marwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. AGNES M. MARWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushuru sana kwa kunipa nafasi hii ya kuchangia wizara hii kwanza niwapongeze sana waziri na watendaji wote katika wizara hii, lakini pia nimpongeze kipekee dada yangu kwa awamu iliyopita daktari wa covid Mheshimiwa Waziri Ummy kwa kazi kubwa aliyoifanya kipindi kilichopita pamoja na Serikali nzima akiwemo Mheshimiwa wetu Hayati John Pombe Magufuli pamoja na mama yetu Samia kwa kazi nzuri waliyoifanya kipindi kilichopita ambayo sasa mama anaiendeleza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niseme tu kwa kweli hotuba ya juzi ya mama alipokuwa na wazee nampongeza sana Mheshimiwa wetu Rais kwa moyo huohuo Mwenyezi Mungu amwongezee sana na azidi kumpa hekima na sisi tunamuombea sana aliposema kwamba huduma ya afya kwa wazee iboreshwa. Naamini kabisa mama yetu wewe ni mama na bahati nzuri ulianza na baba, baba katuacha na wewe, kwa hiyo, tunaamini kabisa wazee hawa wanategemea faraja kutoka kwako kama ulivyosema Mheshimiwa Rais wetu kwamba huduma hii itaboreshwa tunaamini kabisa suala hilo litasimamiwa vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nikuombe waziri na watendaji wako, Mheshimiwa Rais ametoa maagizo huduma kwa wazee iboreshwa sio sasa mpaka aje kuanza kutumbuatumbua ndio muanze kufanya vizuri. Niwaombe sana hili suala mliangalie kwasababu hawa wazee pia watoto wao ni wapiga kura wenu na wao wenyewe ni wapiga kura wenu lakini pia kwa kura za kishindo walizozitoa sasa hivi watanzania wanasubiri na kutegemea matokeo chanya kwa wabunge wao na kwa serikali yao. Kwa hiyo, niseme tu naamini kabisa Mheshimiwa Waziri uliyechaguliwa ni jembe na ninaamini kabisa wewe ni mtendaji mzuri, hawa wazee watapata faraja kutoka kwako. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nikuombe sana, Mheshimiwa Waziri sasa aangalie hili suala la watoto wa chini ya miaka mitano. Kule kwetu Mkoa wa Mara na hasa katika hospitali nilizokwenda kukutana na malalamiko haya kwamba watoto wa chini ya miaka mitano wanalipishwa wakati watoto wale wanatakiwa wapate huduma bure. Nafikiri sio jambo zuri Mheshimiwa Waziri lifatilie na ikikupendeza naomba tuongozane nikakupeleke maana ushahidi ninao na baadhi ya stakabadhi walizolipia nilichukuwa kabis ushahidi ninao. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ila tu ukifika usiwatumbue urekebishe tu mambo ili yakae sawa kwa hiyo niseme tu kwa kweli wananchi wetu wanaumia, tusimamie vitu tunavyokuwa tunaviahidi lakini pia tufanya kwa kadri ya mapenzi ya Mungu tukiwa tunajua kwamba kesho ahera tutajibu nini, sio tu watupigie kura wakimaliza kutupigia kura watanzania hawa vitu vingine tunakuwa kama vile hatuwaatendei haki wakati sisi wenyewe ndio tumeahidi kutoka midomoni kwetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia niishukuru sana Serikali yangu ya Chama Cha Mapinduzi kwa kipindi kilichopita na sasa hivi kwa kutejengea hospitali nzuri sana ya rufaa hospitali ile kwa kweli ilikuwa na muda mrefu sana na sasa imejengwa iko vizuri, na imeanza kutoa huduma lakini tu kama alivyosema Mbunge mwezangu Mheshimiwa wetu waziri tungeomba sana kwasababu Mkoa wa Mara kiukweli ni kwamba ni mkoa ambao mnatakiwa muuweke ukae kimkakati kwasababu ndio mkoa uliomtoa Mhasisi wa Taifa hili Hayati Mwl Julius Kambarage Nyerere. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, basi ile hospitali ya rufaa irekebishwa vitu vilivyobaki ili kusudi sasa na mkoa wa mara wale wanaojua wale watu wanaojua maana kule sisi kuna bibi zetu ambao mpaka leo wanajua Mwl Nyerere yupo Butiama hawajui kama ameshakufa mpaka leo ukienda kule vijijini saa nyingine wanakuambia ah sisi tunaenda kuchagua chama cha Mwl Julius Kambarage Nyerere. Sasa kwasababu hiyo basi mazingira yaboreshwa hata sisi tuonekane kwamba akina Agnes tunatoka Mkoa wa Muhasisi wa Taifa hili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nikuombe sana Mheshimiwa wangu waziri ufanye kweli nakuamini sana waziri najua utafanya kweli. Lakini kipekee zaidi niseme tu hivi sasa, hivi tumejenga hospitali nyingi sana na nzuri sana tena za kimkakati zinazoweza kuwasaidia wananchi wengi sana, katika sehemu zote mikoa yote vijiji vyote hospitali zetu jamani ni nzuri sana. Lakini Vituo vya Afya vimejengwa vingi sana. Mheshimiwa Waziri kama vilevile ardhi walivyokaa kamati nane, basi Mheshimiwa Waziri na wewe pia ukakae chini na waziri au Wizara ya Ujenzi ili muangalie hizi hospitali ziweze kufikika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mama anataka kwenda hospitalini lakini sasa unakuta sehemu zenyewe hazipitiki ni mabonde kuinama sasa kama ni mabonde kuinama inakuwaje yani mabonde kuinama namaanisha kwamba hapa kuna shimo mara hapa kuna mtaro umekaa vibaya mara hapajarekebishwa. Kwa hiyo, niombe sana hii Serikali yetu naamini ni Serikali Sikivu, na haya mambo ambayo tunayashauri naamini kabisa yatatekelezeka. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimuombe sana mama yetu Mheshimiwa Rais mama yetu kipenzi Raisi wa kwanza mwanamke Tanzania kwa mambo haya yote tunayoyasema hapa mawaziri wake kama watayafuata na kuyashikiria naamini kabisa wakiyatekeleza, na hizi pesa zitoke kwa wakati sio tu tuwe tunaongea hapa maneno tunasema weeee! Pesa mara zimetoka kidogo.

NAIBU SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa kengele imeshagonga.

MHE. AGNES M. MARWA: …mara mkandarasi, nashukuru sana naunga mkono hoja. (Makofi)