Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Hon. Martha Festo Mariki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

MHE. MARTHA F. MARIKI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi nami niweze kuchangia katika Wizara hii muhimu, Wizara ya Afya. Awali ya yote namshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kunijalia uzima na afya njema.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kipekee sana napenda kuishukuru Serikali ya Awamu ya Tano kwa jinsi ambavyo ilivyotutendea mambo makubwa wananchi wa Mkoa wa Katavi kwa kuhakikisha kwamba, imetekeleza Ilani ya Chama Cha Mapinduzi kwa kutupatia hospitali kila wilaya, iliahidi na ilitekeleza. Wananchi wa Mkoa wa Katavi wanasema ahsante sana Serikali ya Awamu ya Tano iliyopita, lakini kipekee tunamshukuru sana Mama yetu Samia Suluhu kwa jinsi ambavyo anaendelea kuchapa kazi na kuhakikisha kwamba, huduma za afya nchi nzima zinaboreshwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wa Mkoa wa Katavi kwanza tunatoa shukrani za dhati kipekee kwa kupata zahanati nyingi na vituo vya afya katika Mkoa wetu wa Katavi. Tumepatiwa zahanati za kutosha, lakini vituo vya afya vya kutosha katika Mkoa wetu wa Katavi katika wilaya zetu mbalimbali. Lakini changamoto kubwa tuliyonayo wananchi wa Mkoa wa Katavi katika wilaya zetu tumepatiwa vituo vya afya, lakini vituo vile vya afya tuna ukosefu mkubwa sana wa watumishi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wetu wa Katavi takribani mkoa mzima tuna upungufu wa watumishi katika kada ya afya takribani asilimia 72 ambapo watumishi tulionao ni sawa na asilimia 28. Kwa jinsi Mkoa wetu wa Katavi ulivyo na muingiliano wa watu wengi utaona watumishi hawa ni wachache sana kuhakikisha kwamba, wanaenda kutatua changamoto katika kuhakikisha wananchi wa Mkoa wa Katavi wanapata huduma zilizo bora katika afya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini wananchi pia wa Mkoa wa Katavi katika vituo vyetu vya afya kuna upungufu sana wa vifaa tiba. Tuna upungufu wa vifaa tiba takribani asilimia 60, ambao sisi tunao ni kama takribani asilimia 40. Tunaiomba sana Wizara ya Afya waweze kutupatia watumishi ili waweze kwenda kutatua changamoto katika vituo vyetu vya afya kwa kuhakikisha wananchi wetu wa Mkoa wa Katavi wanaenda kuhudumiwa ipasavyo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini wananchi wa Mkoa wa Katavi tunaomba sana Serikali yetu sikivu, Serikali yetu tukufu, huduma ya MSD tunaomba katika Mkoa wetu wa Katavi iweze kuboreshwa. Serikali imekuwa ikitenga pesa kwa ajili ya dawa katika Mkoa wa Katavi, lakini MSD wanatuambia baadhi ya dawa hakuna. Sasa tunaomba sana Wizara ya Afya wahakikishe kwamba, wananchi wa Mkoa wa Katavi tumakwenda kupata dawa ili wananchi wa Mkoa wa Katavi waweze kupata huduma iliyo bora katika kuhakikisha kwamba, afya zao zinaenda kuwa safi ili waweze kwenda kuchapa kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi pia wa Mkoa wa Katavi tunasema asante sana Serikali yetu kwa jinsi ambavyo imeona umuhimu ikaamua kutujengea hospitali ya Mkoa wa Katavi ambayo kwa jinsi ninavyoiona ile ramani, jinsi ilivyokaa niiombe sana Serikali, hospitali ile isitumike kama hospitali ya Mkoa hospitali ile kwa ramani jinsi inavyoonesha inafaa kuwa hospitali ya rufaa. Ukiangalia mwananchi wa Mkoa wa Katavi tunatumia gharama kubwa sana kwenda kufuata rufaa katika Mkoa wa Dar-es-Salaam katika Hospitali ya Muhimbili, lakini kwenda Ikonda pia ni mbali sana, lakini ukiangalia kwenda Bugando ni mbali sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wa Mkoa wa Katavi wamekuwa wakitumia gharama nyingi sana kufuata rufaa katika mikoa hii ambayo ni mbali sana na ukizingatia miundombinu yetu katika Mkoa wa Katavi bado ni mibovu. Hivyo, niiombe sana Serikali kwa kuwa, walitenga hela katika Hospitali hiyo ya Mkoa wa Katavi ambayo ina hadhi kabisa ya kufanywa kuwa hospitali ya rufaa au hospitali ya kanda kwa watu wanaotokea katika mikoa hiyo ya Katavi.

Niwaombe sana Serikali, hospitali hiyo ilikuwa ikabidhiwe Januari tarehe 21. Sasa niwaombe tunaiuliza Serikali, ni kwa nini mkandarasi sasahivi hayuko site na hakuna kitu chochote kinachoendelea katika hospitali ile? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na ile hospitali ni muhimu sana kwa wananchi wa Mkoa wa Katavi, lakini kwa wananchi wa mikoa ya jirani, jirani zetu pale watatumia hospitali ile kama ya rufaa ili kuondokana na adha ya kufuata hospitali za rufaa ikiwepo Ikonda, ikiwepo Muhimbili, ambapo ni gharama kubwa nyingi sana. Niwaombe sana Serikali yetu Sikivu, tunaomba hospitali hii iweze kumalizika, ili wananchi wa Mkoa wa Katavi waweze kupata huduma iliyoboreshwa kwa ukaribu ili waweze kuchapa kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukizingatia Mkoa wetu wa Katavi wananchi wale ni wazalishaji wazuri sana wa kilimo wanahitaji huduma iliyo bora, lakini ukizingatia Mkoa wetu wa Katavi Rais wetu aliyepita, Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, aliona umuhimu wa mkoa ule akaamua atajenga bandari, alisema kwamba, atajenga bandari na bandari imeshaanza kujengwa. Kuna bandari inayojengwa Wilaya ya Tanganyika ambayo inaenda kutuunganisha na wananchi wa Kalemii, Kongo, ambako kuna dhahabu nyingi sana. Hivyo yote hiyo naeleza haya ili muweze kuona umuhimu wa hospitali ile kuweza kumalizika, ili iweze kutibu wananchi wengi sana wanaokuja katika Mkoa wetu wa Katavi kuhakikisha fursa nyingi sana za uchumi zinaenda kunyanyuliwa katika Mkoa wetu wa Katavi.

Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo, niiombe sana Serikali hospitali ile ni muhimu sana wananchi wa Mkoa wa Katavi wanaihitaji sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jambo lingine ambalo napenda kuchangia katika Wizara ya Afya, niwaombe sana, kumekuwa na sintofahamu akinamama wanapoenda kujifungua. Mama zetu wanapoenda kujifungua wanakutana na ghadhabu sana wanaambiwa kwamba, wanatakiwa wachangie damu, ila hata pale wanapopata watu wa kwenda kuwachangia damu wanaambiwa kwamba, ile mifuko ya kuchangia damu inauzwa, takribani wanatoa mpaka 16,000/=. Niwaombe sana Serikali waangalie jambo hilo aikinamama ni waaminifu sana na akinamama wana upendo mkubwa na Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niwaombe Serikali muweze kuwaangalia akinamama hawa waweze kwenda kujifungua. Ikiwezekana kama Serikali ilivyosema akinamama watajifungua bure, basi kweli waende kutekeleza hiyo kwa vitendo. Akinamama wa Mkoa wa Katavi na akimama wa Tanzania nzima tuhakikishe kwamba, wanajifungua salama na wanajifungua kwa bei nafuu, ikiwezekana ni bure kabisa kama Mama yetu Mheshimiwa Samia Suluhu jinsi alivyotuahidi. Hivyo, niiombe sana Serikali kupitia Wizara ya Afya mjitahidi jamani, akinamama wa Mkoa wa Katavi wanahitaji huduma iliyoboreshwa ili kuhakikisha akinamama wanajifungua na kuzaliana, tuweze kwenda kuzaliana tuongeze nguvu kazi katika Taifa hili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia, niiombe sana Wizara ya Afya, kutokana na huu upungufu ambao umeonekana ni mkubwa sana, hapa nitazungumzia Hospitali yetu ya Wilaya ya Mpanda ambayo kwa sasa inatumika kama Hospitali ya Mkoa. Hospitali ile jamani ina ufinyu sana wa maeneo kiasi ambacho kwamba, hata upasuaji imekuwa ni kitendawili kufanyika maeneo yale. Niwaombe sana Wizara ya Afya wakati tunasubiri hospitali hii ya rufaa iweze kukamilika niwaombe sana waiboreshe hiyo Hospitali yetu ya Wilaya ya Mpanda ambayo inabeba wagonjwa wengi sana, waiboreshe kwa kuangalia kukarabati miundombinu, lakini kuleta vifaa tiba. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ninavyoeleza hivi hata huduma tu ya CT-Scan katika Mkoa wetu wa Katavi haipo. Niwaombe sana Wizara ya Afya mtuangalie wananchi wa Mkoa wa Katavi. Naongea hivi kwa uchungu sana mtuangalie kwa sababu, mama zangu na baba zangu wanapata tabu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jambo lingine ambalo napenda kuchangia katika Wizara hii ya Afya niwaombe sana. Kwa kuwa, Serikali yetu imeahidi wazee watapata huduma bure, niwaombe sana mtuboreshee wazee waweze kupata huduma iliyo bora na salama. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naunga mkono hoja. (Makofi)