Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Hon. Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kunipatia fursa hii niweze kuchangia kwa dakika tatu kwenye hoja iko mbele yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulipokuja hapa Bungeni nilimueleza Mheshimiwa Waziri kwamba katika Jimbo la Muleba na Wilaya ya Muleba kwa ujumla tunayo changamoto kubwa ya mawasiliano na kwa heshima kubwa nilimpatia maeneo yote ambayo yana matatizo ya mawasiliano. Hata hivyo, leo wakati nasoma hotuba ambayo ameiwasilisha mbele yetu nimeshangaa sana, hakuna hata kata moja ambayo imezingatiwa kwenye bajeti hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuombe Mheshimiwa Waziri, kati ya kata zote ambazo nimempatia, kama mchangiaji aliyetangulia kusema Mkoa wa Kagera tunalo tatizo kubwa la mawasiliano, naomba chonde chonde atusaidie. Kata zote ambazo tumekupatia na sisi kama Mkoa wa kagera tunapaswa kuwa na usikivu wa mitandao, redio ambazo zinachangiwa na walipa kodi wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna maeneo unakwenda ukipotea tu huwezi kupata msaada. Tunapoongelea Kata za Karambi, Mmbunda na Buhigi hakuna mawasiliano hata kidogo. Nilikuwa na dhamira ya kushika shilingi lakini najua Mheshimiwa Waziri ni msikivu nakuomba utakapokuja kuhitimisha bajeti yako useme neno ili wakazi wa Mkoa wa Kagera roho zao zitulie kwamba tunakwenda kuwawekea mitandao au mawasiliano ili na wao wajisikie wanaweza kuwasiliana na Watanzania wenzao na dunia nzima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. (Makofi)