Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Niipongeze michango ya Wabunge walio wengi lakini pia mimi nieleze changamoto ya mawasiliano na hasa ya simu kwa Mkoa wetu wa Kagera. Wakati ninyi mnaongelea kijiji kwa kijiji sisi tunaongelea changamoto ya kata kwa kata yaani inafika mahali kata nzima hawana mawasiliano. Changamoto kubwa ya maeneo yale ni kwa sababu yana miinuko, unaweza kuweka eneo moja kwa sababu kuna bonde eneo la pili lipo na changamoto ya mawasiliano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana nimeomba dakika tatu kueleza changamoto kubwa ya mawasiliano hususani kwenye Jimbo la Karagwe na Kyerwa kwa ndugu yangu pale. Jimbo la Kyerwa kama maeneo mengine tuna changamoto pia au tuna fursa ya kupatikana kwenye mipaka ya nchi ya Rwanda na Burundi. Sasa changomoto hiyo ambayo inapaswa kuwa fursa ya kibiashara kwetu imekuwa ni changamoto kwenye suala la mawasiliano.

Mheshimiwa Mwenyekit, kuna changamoto ya kuingiliana kwa mawasiliano upande wa Uganda. Ukiangalia kata nyingi ambazo ziko mpakani ina maana sisi tunakuwa na weak connection muda wote zinakuwa zinaingiliana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiagalia kama Kata za kama za Murongo, Bugomora, Kibale, Kibingo ukifika tu unapata meseji ya welcome to Uganda hapo wewe huwezi kufanya mawasiliano ni changamoto kubwa sana. Sio hapo tu ukifika Kata kama za Isingiro, Kaisho na maeneo mengine unaambiwa welcome to Airtel Rwanda, kwa hiyo, tunajikuta muda mrefu sana tuna changamoto ya mawasilisano. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine ambalo ni kama bonde na liko mpakani wa Rwanda katika Kata ya Songambele linaitwa Kitega, siku moja nimeenda huko nikasema hivi hii nchi mbona kama hili eneo linaweza likavamiwa likachukuliwa kwa sababu hawana mawasiliano ya aina yoyote na wako jirani sana na Rwanda. Kwa hiyo, naomba nielezeā€¦

T A A R I F A

MHE. ESTER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI. Taarifa.

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nataka nimpe taarifa Mheshimiwa Anatropia kwamba kweli kabisa sisi tunaokaa mipakani kwa mfano kule Tarime ukifika mitaa ya Sirari wanakuambia welcome to Kenya unaingia kwenye roaming. Kwa hiyo, wale watu wanaingia gharama kubwa maana wanaoneka kama vile wako nje ya nchi.


Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nataka nimpe hiyo taarifa kwamba hayo matatizo yanawakumba watu ambao wako mipakani. (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Anatropia.

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa naipokea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, changamoto ya mawasiliano aliyoyasema Mheshimiwa wa Tarime na maeneo mengine ndiyo kwa kiwango inatukuta Kagera. Niombe sana na sisi Kagera hebu tukumbukeni na oneni Kagera kuna fursa ya biashara. Nimeeleza sisi Kyerwa tunapakana na nchi nyingi, kwa hiyo, tuna fursa nyingi za kibiashara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini mwisho kabisa changamoto ya mawasiliano ya redio, jamani kwa nini mmeamua kutufundisha tuanze kuongea Kinyarwanda na Kiganda tu maana ndiyo redio tunazozisikia kule. Unataka kupata redio za Tanzania mpaka ifike saa kumi na mbili jioni ndiyo utasikia Redio Tanzania wamefungua, nadhani sio sahihi kabisa. (Makofi)