Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

MHE. CASATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kupata nafasi na ninapenda kuchukuwa nafasi hii, kwanza kuwa shukuru Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na timu yake, lakini pia shukrani za pekee kwa Mamlaka ya Mawasiliano kwa maana ya TCRA ambapo miaka miwili iliyopita walitusaidia watu wa Mafinga katika Shule ya Msingi Mchanganyiko ya Makalala hii ni shule ya watoto wenye mahitaji maalumu siku hizi tunaita watoto wenye uono hafifu zamani tulikuwa naita watoto vipofu, wale wanamahitaji maalumu kwa maana vifaa wanavyotumia katika kujifundishia na kujifunzia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo TCRA walitusaidia lakini pia walitusaidia pale shule ya Sekondari Luganga kuwapa vifaa ili kuwawezesha wanafunzi kupata masomo katika namna ambayo kidogo inawepesi kwa hiyo, napenda kuwashukuru sana kwa ushirikiano huo na kwa kazi nzuri ambayo wanafanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pamoja na shukrani hizo ninayo maombi machache na mchango mdogo kwa wizara na kwa Serikali kwa ujumla. Asubuhi nilikuwa nina swali kwa Wizara ya Nishati kuhusu masuala ya umeme na sehemu ya majibu ya Mheshimiwa Waziri akijibu swali lake, alikiri kwamba Mji wa Mafinga unakuwa kwa kasi na kunaviwanda vikubwa 80, maana yake ni kwamba huu ni mji wenye mchango mkubwa sana katika uchumi wa Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ili Mafinga na Wilaya ya Mufindi kwa ujumla kama alivyosema pacha wangu David Kihenzile iendelee kuwa na mchango mkubwa na kama alivyosema Waheshimiwa wengine katika michango yao masuala haya ya matumizi ya simu yanaumuhimu wake. Kwa hiyo, niiombe Serikali kuna maeneo kwa mfano; Kijiji cha Mtula, Itimbo, Buliainga, Kisada, Ulole, na Maduma. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vijiji hivi viko umbali wa kama kilometa zisizozidi tano kutoka katikati wa mji wa Mafinga, lakini mawasiliano yake hayana huhakika. Sasa kama nilivyosema kama ni huu mji wenye viwanja vikubwa 80 maana yake kwanza kwa kukosa mawasiliano inachelewesha mchango wa hawa watu katika ukuwaji wa uchumi wa Taifa na wao wenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini namba mbili pia inacheleweza mapato ya Serikali kwa sababu wangekuwa na mawasiliano inamaana kwamba wangetumia simu wangenunua data, wangenunua muda wa maongezi lakini pia wangefanya miamala ya fedha kwa hiyo katika mzunguko mzima ule Serikali ingepata kitu ambacho inastahili kupitia kodi na tozo mbalimbali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niombe sana kwa Serikali kwenye yale maeneo ambayo yanashughuli kubwa za kiuchumi ni kweli hii ni huduma lakini pia ni biashara. Sasa unapowekeza lazima pia kama ni huduma maana yake kila mmoja itabidi imfikie ile huduma, lakini ukilingalia kwa jicho la kibiashara elekeza nguvu maeneo ambapo itakupa faida kwa haraka ili uweze kuwapelekea huduma wale ambao kwao mzunguko ni mdogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kwangu na hususani na watu wa Mafinga na Mufundi kwa ujumla kutokana na uchumi wetu kutokana na mazao ya misitu na bidii namna watu wanavyofanya kazi, naishauri Serikali sana itupie jicho kule wanaweza wakawekeza kule shilingi milioni 10 ikakupatia wewe milioni 100 ambayo ikaweza kupeleka huduma maeneo mengine. Kwa hiyo, nashauri namna hii ya kupeleka hizi huduma uziangalie pia katika jicho la kibiashara, kwamba unaweza ukanicheleweshea A ukamuwahishia B ili kusudi kesho uweze kumhudumia C na D na F kwa hiyo naomba sana hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesoma sana ripoti ya mara kadhaa PWC inaitwa Entertainment and Media Outlook 2018/2022 yaani African Perspective hawa mabwana wameelezea kwa matumizi ya internet kama Wabunge wengine walivyosema siyo tu katika suala nzima Media and Entertainment Industry, lakini pia katika mchango wake wa uchumi katika mataifa mbalimbali kwa mfano; mchana watu wengi wamesema sisi hapa Tanzania kweli tunanufaika na matumizi ya data na uwelewa umekuwa mkubwa tumeona juzi TCRA wametupa workshop na imetusaidia sana kupanua wigo wa mawasiliano na ufahamu wa suala nzima la internet katika maisha yetu ya kawaida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nitoe wito kwa Mheshimiwa Waziri na Wizara yako kwa ujumla na vyombo vyake Mfuko wa Mawasiliano na TCRA najua inawezekana huwa mna-platform, lakini niombe muwe na platform za watu ambao ni wasanii tuseme watu wa entertainment ili waweze kuwaambia ni changamoto gani ambazo wanakutana nazo inapokuja suala nzima la suala la matumizi mawasiliano katika ujumla wake. Kwa sababu tunaweza tukadhani kwamba tume exhaust hii potential lakini kumbe bado kwa sababu sisi pengine tumejifungia tuko na makaratasi na na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema, semina ya juzi ya TCRA sisi wengine imetufungua sana kwa mfano mimi nilikua najua kwamba gharama za simu katika Tanzania ni kubwa sana, lakini kutokana na Takwimu ambazo tumepewa kwenye ile semina nimebaina kwamba kumbe sisi katika Afrika Mashariki na katika SADC sisi ndiyo the cheapest. Sasa unaweza ukawa unatengeneza manunguniko na lawama kutoka kwa wananchi au kwa wadau kumbe simple because hawako informed. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nikuombe Mheshimiwa Waziri, kutana na jamii ya Media and Entertainment Industry, fahamu changamoto wanazokutana nazo, fahamu na wenyewe fursa gani wameziona katika jicho la Media and Entertainment Industry, bila shaka kwa pamoja mnaweza kwenda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini usiishie hapo tu ningeomba katika hiyo platform kadri itakavyo kupendeza washirikishe pia na watu wa izara ya habari na utamaduni kwa sababu wao pia wanawasimamia wasanii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitakupa mfano leo hii mtu akitengeneza filamu yake inatakiwa ikaguliwe na bodi ya filamu, lakini hiyo bodi ya filamu ofisi yao ipo Dar es Salaam tu. Hili jambo nimelisema sana TCRA nadhani wapo level ya kanda, NEMC wapo level ya kanda, lakini kwanini bodi ya filamu, BASATA na COSOTA wao wakae tu pale Dar es Salaam na siku moja nilisema hapa. Msanii ametoka Mafiga Bumilahinga au ametoka Tandahimba au ametoka Kigoma, kwanza ameingia gharama au Shinyanga kwa dada yangu Lucy, ameingia gharama za kusafiri, anaingia gharama za malazi anafika katika zile ofisi anaambiwa bwana printer imearibika. Sasa katika dhama hizi unamwingizia huyu mtu gharama za kile kitu anachokifanya, lakini wakati mwingine unakuwa ume-discourage. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ninaomba sana kuna potion kubwa sana katika suala nzima la Media and Entertainment Industry, Mheshimiwa Waziri kaa na hawa wasanii, kaa pia na wizara inayohusika na hilo jambo kwa pamoja naamini na wataalamu wako walivyokuwa wasikivu kwa jinsi nilivyowaona TCRA juzi mtajuwa tu kuna potential kubwa kiasi gani wapi watu hawa muweze kuwasaidia wapi muweze kuwa-guide. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu mtu mwingine alikua analalamika kwamba wakati mwingine sheria zetu yaani haziko ku-facilitate zimejiongoza sana kwenye kudhibiti kuliko ku-facilitate. Kwa hiyo, ukikaa na hawa wadau wataweza kukupa mawazo na kueleza kwamba jamani hapa rekebisheni hili hapa lina-potential hii, hapa sisi kama wasanii tutanufaika moja mbili ta, hapa kama Serikali tutanufaika moja, mbili, tatu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho ni siku ya tatu na asubuhi nilisema nimepita pale TANESCO kuna foleni unawakuta hadi watu wazima wamesimama pale, watu hawawezi kununua LUKU online mpaka sasa hivi. Nimeona Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana kwa maana Waziri wa Nishati ameshaanza kuchukuwa hatua, lakini that one is not enough na nimesema hii mambo ya kuombana excuse kutupa tahadhari na kutuomba radhi kwamba kutakuwa na 1,2,3 kweli haya mamifumo pengine siyo ya kwetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naamini kwenye wizara yako na TCRA ukishirikiana na vyuo, kampasi zinazohusika na hayo mambo ya IT, DIT, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, UDOM mnaweza mkawa na mifumo ambayo itakuwa na backup system, kwamba mfumo A ukifa kuna weza ukawepo mfumo wa dharura ambao unaweza kusaidia lile tatizo kwa muda ule ili kusudi kupata suluhisho la kudumu katika tatizo kuu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sasa mimi hapa ninajitolea mfano; naomba ku- declare interest, nina hotel Mikumi toka jana tunawasha generator siyo kwamba hatuna fedha ya kununulia Luku, tunayo fedha ya kununulia luku lakini you can’t buy online kweli Waziri amesema twende ofisi ya TANESCO hivi mtu leo hii atoke Mkonze kwa hapa Dodoma kwa mfano aje akasongamane pale TANESCO. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja kwanza TANESCO yenyewe inajikosesha mapato ambayo ni Serikali, lakini pili unapararaize shughuli za uzalishaji sisi wenye viwanda 80 Mafinga kama leo viwanda 30 vimekosa kuwa na LUKU toka juzi. Hivi ni ajira kiasi gani umeziathiri, pay as you n kiasi gani umeathiri, SDL kiasi gani, umeathiri? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, unaweza kuona Mheshimiwa Waziri nakuomba sana hii sekta na hii wizara nikwambie kitu yaani wewe ndiyo kila kitu, ukienda kwenye umeme ni wewe, nimesema Media and Entertainment Industry ni wewe, ukienda kwa Mheshimiwa Lukuvi unataka kulipa hizo kodi za ardhi itakuwa ni wewe, ukienda kwenye kulipa mishahara utakuwa ni wewe. Kwa hiyo, ninaomba uiangalie hii wizara na wataalamu wako kwa jicho ambalo ni pana kweli kweli ili kusudi changamoto unazokutana nazo kwenye mambo ya online tuweze kuondokana nayo kwa sababu tunaenda kwenye uchumi wa viwanda. Kwa hiyo, kwanza tupate mapato lakini pia tu-speed up uchumi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo nakushukuru naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)