Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Hon. Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

MHE. JUDITH S. KAPINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwa sasa hivi Tanzania na dunia nzima tumesimama katikati ya mabadiliko makubwa ya teknolojia ambayo kwa kiasi kikubwa yamebadilisha yataendelea kubadilisha namna tunavyoishi, namna tunavyofanya kazi na namna tunavyoshirikiana na watu wengine. Huko tunakoelekea, kwa namna ambavyo mabadiliko ya teknolojia yanatokea, haina shaka kwamba kwa ujumla maisha yetu yatabadilika kwa kasi ambayo tusiyoitarajia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tunakumbuka, tukiangalia hapa tulipo na tulipotoka, mapinduzi ya kwanza ya viwanda namna ambavyo yalikuwa yanaendeshwa, yalikuwa yanatumia njia ya maji pamoja na mvuke, yaani water na steam power. Mapinduzi ya pili yali-advance kidogo yakawa yanatumia electronic power; mapinduzi ya tatu yakaenda yakawa yanatumia electronics and information technology. Hapa tulipo sasa hivi yame-advance kiasi cha kwamba tunatumia mchanganyiko wa nguvu kazi yaani za mikono, kidijitali na mbinu za kibaiolojia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema haya ili niweze kueleweka kwamba hapa tulipo tuko katika nyakati ambazo hazijawahi kutokea katika historia ya dunia na mabadiliko yanayoenda sasa hivi kwa kasi ambayo yanatokea haijawahi kuwa recorded toka dunia imeanzishwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema pia ili tuone umuhimu wa kuwekeza katika masuala ya teknolojia, sayansi pamoja na uvumbuzi, lakini hatutaweza kufanikiwa kwa sababu masuala yote yanayohusiana na sayansi, teknolojia, uvumbuzi, mawasiliano na habari hayajawekwa pamoja katika nchi yetu, yaani yameparanganyika. Yapo Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia lakini masuala ya information na communication na ICT yako kwenye Wizara hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Elimu kama tunavyofahamu ni dubwana kubwa namna hii, masuala ya sayansi na teknolojia, hayawezi kuendelezwa pale kwa kasi ambayo sisi tunaitaka na ndiyo maana leo hii nataka nishauri Serikali yangu sikivu. Wakati umefika sasa tu-centralize masuala yote yanayohusiana na sayansi, teknolojia, uvumbuzi, habari na mawasiliano kwenye sehemu moja. Sehemu sahihi ni Wizara hii ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme kwamba kwa nini tu-centralize leo? Ni kwa sababu tunapaswa kujisuka upya ili tuweze kwenda na kasi ambayo dunia inaenda. Lazima tukae kwenye mstari ambao the rest of the world wapo. Leo hii tulipokaa hapa nchi 24 duniani zimeshaweka makubaliano ya kumaliza matumizi ya mafuta ya petroli kuanzia mwaka 2025, ina maana watakuwa wanatumia magari ya umeme ama magari ya gesi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii tulitakiwa tuwe tuna mkakati wa kutuwezesha sisi kuungana na dunia kupambana na mabadiliko ya tabia nchi kwa kuwekeza kwa wataalam ambao wanaweza kubadilisha mifumo yetu ya magari kwenda kwenye mifumo ya magari aina ya umeme na gesi. Haya yote hayawezekani kwa sababu mambo yote haya yamekuwa decentralized. Hakuna sehemu moja ambapo tunaweza tukajisuka kama nchi na kwenda katika kasi ambayo dunia yote inaenda leo hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ni rai yangu kwa Serikali ya chama change, ni wakati umefika tu-centralize sayansi, teknolojia, uvumbuzi, mawasiliano na habari kwenda kwenye Wizara hii ili yaweze kufanyiwa kazi kwa kasi ambayo sisi tungeitamani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukizungumzia kwa mfano leo, kuna nchi kadha wa kadha zinanufaika na startup program za vijana kwa sababu wamejisuka na system yote imekuwa centralized. Leo South Africa wanaingiza takribani 1.3 trillion kwa startup program 10 tu za vijana. Imagine pesa ambayo Serikali yao inapata kama wana startup programs 100. Kenya tu hapo wamewekeza kwenye startup programs na wanapata zaidi ya USD milioni karibia 300 kwa program 10 tu. Sisi tunaweza kufanya haya; startup programs chini ya COSTECH hazijipambanui zaidi kiuchumi kwa sababu hazijaweza kusukwa ipasavyo kwa mifumo ambayo tunayo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana nasema vijana wa Taifa hili watapata ajira zile milioni nane kwa urahisi kama tukiwekeza kwenye masuala ya teknolojia na hizi startup programs. Kwa sababu startup programs 10 tu zina uwezo wa kuajiri mpaka vijana 1,000. Sasa imagine una startup program 100. Ndio maana naendelea kusisitiza, ni wakati umefika kujisuka upya masuala yote yanayohusiana na sayansi, teknolojia na uvumbuzi yawe centralized hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sera ya ICT iko chini ya Wizara ya Mawasiliano lakini Sera ya Sayansi na Teknolojia, tena ya siku nyingi, iko Wizara ya Elimu. Sera ya Uvumbuzi mpaka leo mwaka 2021 hatuna Sera ya Innovation kwenye Taifa letu. Ndiyo maana nazungumzia habari ya ku-centralize masuala haya ili yaweze kufanyiwa kazi katika sehemu moja na tuweze kupiga kasi. Trust me not, ikifika 2025 hapa tutatafutana kwa sababu dunia inaenda kwenye kasi ambayo haijawa recorded sehemu yoyote ile. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa nijielekeze kwenye masuala yanayohusiana na ma-bundle. Kumekuwa kuna malalamiko kwa walaji wengi kwamba ma-bundle wanayotumia yanaenda kwa kasi mno. Inawezekana ikawa ni matumizi, lakini kuna tatizo sehemu. Wizara ilielekeza haya makampuni ya simu yaweze kuweka mita zinazoonyesha utumiaji wa ma-bundle, lakini tatizo linakuja kwenye speed ya ma-bundle ambayo tunauziwa. Hizi zinaitwa MPDS hazijawekwa wazi. Kuna makampuni wanatutoa speed ya 3 - 5 MPDS, lakini sasa ma-bundle tunayouziwa, leo Vodacom akinipa mimi bundle la 2GB na Tigo akinipa bundle la 2GB inawezekana la Vodacom likaisha kabla ya Tigo kwa sababu haijawekwa kwamba bundle la 2GB ambalo ninapewa inabidi liwe la speed gani, MPDS ngapi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana watumiaji wa mtandao mmoja wanalalamika kuliko watumiaji wa mtandao mwingine, kwa sababu hatuna hata kipimo na hatuwezi ku- trap matumizi ya mitandao yetu. Ndiyo maana leo unaweza ukanunua 2GB ikaisha. Ni haki kwa Mtanzania kulalamika kwamba bundle langu linaisha kama upepo, kwa sababu hatuambiwi speed ya ma-bundle tunayotumia ni MPDS ngapi; na ni vigezo gani vinatumika? Kwa hiyo, labda ifike kipindi tuuziwe ma-bundle kwa mantiki ya speed basi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii tunaambiwa Watanzania ni nchi ya nne kwa ma-bundle rahisi Afrika; lakini sasa kama bundle langu nanunua kwa bei rahisi napewa GB1 sawa, baada ya saa moja, nanunua tena GB1, hiyo ni rahisi in terms of quantity or in terms of speed? Kwa hiyo, ifike mahali sasa Wizara ituangalie hapa; kuna jambo hapa kwenye masuala ya ma-bundle. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, upande wangu wa pili naomba nizungumzie kuhusu masuala ya matumizi ya internet. Naipongeza Serikali, watumiaji wa internet wameongezeka mpaka kufikia milioni 29, lakini nachelea kusema kwamba watumiaji hawa kwa kiasi kikubwa ni watumiaji wa mijini. Sisi kule kwetu Mbinga Kata 29 na vijiji 117 hatuna internet. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, yaani vijiji vyote 117 tunahangaika, mpaka tufike mjini ndiyo tuweze hata kutuma document ama kufungua document kwenye simu. Naomba Waziri wakati anakuja hapa, atueleze sisi wananchi wa Mbinga Vijijini ni lini tutatatuliwa matatizo yetu ya internet? Leo hii kata zote 29 na vijiji 117, jamani naomba Waziri atuambie sisi wananchi wa Mbinga Vijijini tutafanyaje? Maana sasa tunakosa cha kufanya. Tunaomba tuangaliwe tupate na sisi 3G kwa sababu vijana wengi wako kule vijijini, siyo kwamba vijijini hamna vijana ambao wamesoma. Wanataka kuuza kahawa zao kwenye mitandao, wanataka kuuza unga wao kwenye mitandao, tuletewe na sisi kule ili tusije kufanya kazi mjini tukae kule kule kwetu tuuze biashara zetu kule kule tulipo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile tunafahamu kwamba mawasiliano ya simu ndiyo maisha siku hizi, lakini kata saba hata kupiga simu huwezi. Kata hizo, naomba niweke kwa record; Kitura, Kipololo, Ngima, Mhongozi, Ukata, Amanimakoro, Kihangimauka; na hapa Mheshimiwa Waziri
nataka nikupe taarifa nitashika shilingi, naomba utuambie ni lini kata hizi zitapata mawasiliano ya simu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naunga mkono hoja. (Makofi)