Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Hon. Antipas Zeno Mgungusi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Awali ya yote, naomba uniruhusu niweze kutoa shukrani kwa Ofisi ya Waziri Mkuu na Ofisi ya TAMISEMI ingawa siyo Wizara hii, lakini waliweza ku-attend dharura ya Malinyi ya mafuriko ya maji yaliyoathiri barabara zetu. Fedha zimetolewa, sasa wakandarasi wapo site wanatatua tatizo Wanamalinyi watakuwa na amani hawataathirika tena na masuala ya mvua. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Wizara hii nina mambo mawili au matat. La kwanza, Jimbo langu la Malinyi lina changamoto ya mawasiliano, sehemu kubwa ya jimbo huwezi kupatikana, karibia asilimia thelathini au arobaini ya Jimbo ndiyo wanapatikana hewani, lakini zaidi ya asilimia sitini, sabini hakuna mtandao voice na data ndiyo kabisa ni changamoto kubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mpaka hivi ninavyozungumza Ofisi ya Mkuu wa Wilaya na Ofisi ya Mkurugenzi hazipatikani kwa maana huwezi kumpata mtu hewani akiwa kwenye Ofisi hizo mpaka jioni wakirudi mtaani ndiyo unaweza wakapatikana. Kwa hiyo, naona Wizara inanisikiliza naomba walichukulie hili jambo kwa udharura watu Malinyi waweze kusaidika tuweze kupata mawasiliano kama maeneo mengine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia changamoto ya cyber-crimes kwa maana ya wizi wa mtandao umeendelea kuwepo. Mnakumbuka tulifanya usajili wa line kwa njia ya vidole ili kuweza kudhibiti changamoto hii, lakini mpaka leo hii bado watu wanafanya utapeli na namba ambazo zinatumika kufanya utapeli bado zinapatikana hewani mpaka hivi ambavyo ninazungumza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi binafsi ni muhanga wa jambo hili, watu wame-forge akaunti kwenye mitandao ya facebook wanawatapeli watu kuna masuala ya ajira mtume nauli na kadhalika ili ufanyiwe mipango, namba ambazo zinatolewa watu wanapiga bado zipo hewani na watu wanaendelea kutapeliwa fedha. Nimefanya majaribio kadhaa rasmi kwa maana ya kuripoti Polisi miaka miwili iliyopita, tumeandika barua, nimepewa RB naambiwa watu wa cyber wanafuatilia lakini mpaka leo wanaendelea kutapeliwa na tunachafuliwa heshima zetu. Sasa mimi ni
kiongozi nina access ya kusema, sijui watu wangapi kwenye nchi hii wanakumbana na adha ya namna hii na hawezi kusema. Kwa hiyo, naomba Wizara ilichukulie jambo hili serious.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu, ni suala la mawasiliano ya simu katika vivutio vya utalii kwenye National Parks, Game Reserve na maeneo mengine. Kwa mfano, Hifadhi kama ya Mlima Kilimanjaro tuna watalii wengi wanapanda lakini asilimia 90 ya mlima ule mawasiliano hakuna. Watangazaji wazuri wa utalii ni watalii wenyewe, watalii wa ndani na watalii wa nje, watu wanapanda milima wanapenda ku-share experience yao moja kwa moja, watume picha kwenye mitandao, wafanye live video calls kuwahamasisha wengine lakini jambo hili haliwezekani kwa maana ya kwamba network hakuna kabisa mlimani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niombe tu Mheshimiwa Waziri alichukue hili washirikiane na Wizara ambayo ni mlaji ya Maliasili wahakikishe Mlima Kilimanjaro ambacho ni kivutio chetu kikubwa mawasiliano yawepo muda wote hasa ya data. Jambo hili linaendelea hata kwenye hifadhi zingine Ruaha, Ngorongoro maeneo mengine ya misitu yote yana changamoto kubwa za network. Kwa hiyo, naomba suala hili lichukuliwe kwa uzito kusaidia watalii kui-enjoy na kuwashawishi wenzao kwa kuona kwenye mitandao uzuri wa vivutio vyetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo changamoto pia ya doria, askari wetu ambao wapo porini wanafanya doria kulinda maliasili za nchi yetu, wanakutana na changamoto kubwa ya mawasiliano. Siyo mara zote radio call zinafanya kazi vizuri lakini mawasiliano ya simu yanaweza kuwa rahisi kuhakikisha watu waliopo kule porini wanafanya kazi vizuri, wanatoa taarifa kwa wakati, muda mwingine ni rahisi hata ku-track majangili, mambo ya kuviziana ni ya kizamani sana lakini technology ndiyo inafanya kila kitu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naamini Wizara inanisikia walichukue jambo hili, hata majangili ambao wapo porini wanapanga mipango unaweza ukawa-track kupitia technology. Maeneo makubwa ambayo yanaathari ya ujangili hayapatikani kwa simu tunatumia tu radio call. Kwa hiyo, naomba Serikali ilichukue suala hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa leo mchango wangu ni huu, nashukuru sana. (Makofi)