Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

Hon. Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipatia fursa hii ya kuchangia hotuba ya Mheshimiwa Rais.
Awali ya yote, nachukua fursa hii kuwashukuru na kuwapongeza wananchi wa Wilaya ya Muleba Kaskazini, Jimbo la Muleba Kaskazini kwa kunichagua, lakini zaidi namshukuru Mheshimiwa Rais kwa kuwa na imani na mimi kunikabidhi Sekta ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Sekta ambayo ndiyo inabeba kazi kubwa ya sehemu ya kwanza ya Awamu ya Tano ya Serikali yake.
Mheshimiwa Naibu Spika, dhima ya sehemu ya kwanza ya Awamu ya Tano ni kujenga uchumi wa viwanda ili kuchochea mageuzi ya uchumi na maendeleo ya watu. Ndiyo kazi ambayo tumepewa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama walivyochangia Waheshimiwa Wabunge, viwanda vitajengeka, lakini nani atajenga? Wabunge tuna nafasi ya mbele, kila Mtanzania ana jukumu na injini kubwa ya kujenga viwanda ni sekta binafsi.
Niwahakikishie, Serikali ya Mheshimiwa Rais amesema itaweka mazingira bora na hiyo ni moja ya kazi ambayo amenikabidhi mimi. Ukisoma taarifa ya Doing Business 2016, Tanzania tumewekwa mahali pabaya, hali siyo nzuri. Bado njoo kesho zipo. Hiyo ni kazi ambayo nitaisimamia na mimi ni tarishi mkuu. Nitatembea Wizara zote, Idara zote, kuhakikisha kwamba wafanyabiashara, wawekezaji, wenye viwanda, wanatendewa sawa na kwa haraka. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa nini tunakwenda kwenye viwanda? Kwa nini tunatoka kwenye uchumi wa uchuuzi? Sifa moja kubwa, viwanda vinatoa ajira kubwa sana. Tuna matatizo na vijana kwa sababu hatuwapatii ajira na Mheshimiwa Rais ameshatoa maelekezo. Nimepewa matrix mezani kwangu, nimeambiwa kila Mkoa kiwanda gani kiende; kila siku natafua wawekezaji wa ndani na nje ya nchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, tuna maeneo matatu tunayolenga; kuna viwanda vilivyopo sasa nchini, tutahakikisha vinafanya kazi na nitaondoa vikwazo vyote kama tarishi mkuu. Vile vile kuna wawekezaji wa ndani na nje wanaotaka kuwekeza, mimi ni mtumishi wenu, nitahakikisha nawatendea zaidi mnavyopenda ili muweze kuwekeza ili kutengeneza ajira nyingi, lakini nisiwafiche, muweze kuchangia kwa kutulipa kodi ili tuweze kupata maendeleo ya Watanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, namba tatu, kuna suala ambalo Mheshimiwa Rais amelizungumza kwenye hotuba yake kuhusu viwanda vilivyobinafsishwa. Kuna watu wanasema Mwijage ametoa maelekezo miezi sita sijui wafanye nini. Siyo miezi sita, amri ilishatolewa ya Treasury Registrar, wote mliopewa viwanda mwende mjisalimishe, ueleze hicho kiwanda unakifanyia nini. Niwaeleze, watu wasiwe na mtazamo hasi, siyo kweli kwamba viwanda vyetu vinafanya vibaya, hapana!
Mheshimiwa Naibu Spika, Breweries ilibinafsishwa, inalipa shilingi bilioni 400 kwa mwaka kama ushuru. Mbeya Cement inalipa shilingi bilioni 38 kwa miaka mitano, inafanya vizuri, inakwenda kuzalisha tani milioni moja ifikapo mwisho wa mwaka; na mwezi ujao nakwenda kufungua kinu kipya cha kuongeza usalishaji. Twiga Cement inafanya vizuri, lakini Moro Polister ilikuwa inazalisha kilometa 16 za urefu wa nguo leo inazalisha kilometa 60. Fikiria kilometa 60 ya nguo. Kwa hiyo, tusiangalie upande hasi na upande chanya upo. Aidha, kuna mazingira yasiyokuwa sawia kwa wawekezaji wa ndani, wanazidiwa na vitu vinavyotoka nje. Nitahakikisha kwamba mnatendewa haki ili tuweze kufanya kazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimesema Tanzania halitakuwa dampo la taka, substandard products hazitaingia nchini na nitasimamia. Nimemwambia Manager wa TBS ukae standby mimi na wewe tunafanya kazi sahani moja. Ndugu zangu tutahakikisha vipyeo vinakuwa sawia. Mtu analeta mzigo umejaa kwenye meli, anasema nimeleta nusu, amharibie kazi Mzee Mpango. Nitakusaidia kufanya kazi hiyo Mzee Mpango, kwa sababu ndiyo kazi niliyoanzanayo. (Makofi)
Mtu analeta finishing product anasema siyo finished product kusudi ampige magoli Mzee Mpango. Mjukuu wangu nitahakikisha mambo yanakuendea vizuri, kwa sababu hiyo ndiyo kazi ya taaluma yangu. Tutahakikisha uwanja wa ushindani upo sawa kusudi watu wafanye biashara. Watanzania wengi wameshindwa kufanya biashara kwa sababu uwanja wa ushindani haukuwa sawia.
Kwa hiyo, ndugu zangu Watanzania nitawaletea matrix, yule anayejua nini faida ya kwao ya kiwanda, aje aniambie. Shemeji yangu nikwambie, usiwe na wasiwasi, kiwanda cha mbolea kinajengwa Mtwara na wawekezaji wanagombania Mtwara.
Mheshimiwa Naibu Spika, niwatoe mashaka, watu wanaosema Bagamoyo isijengwe Bandari, Bagamoyo siyo Bandari, ni Bagamoyo Special Economic Zone. Ni zaidi ya Bandari! Kuna mji unajengwa Bandari square kilometer 100. Nimekwenda pale na nimewaagiza, Bandari mtengeneze kitu kinaitwa wet port kusudi meli zitakazokwenda kuvua, zikija zing‟oe pale Bagamoyo tuweze kufanya vitu vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, nitachangia zaidi kwenye Mpango. (Makofi)