Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

Hon. Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi nami niweze kuchangia katika hoja iliyoko mezani. Nianze kwa kusema Serikali nyingi duniani huongozwa kwa Katiba iliyojiwekea, Sheria zilizopo, Kanuni zilizopo, Taratibu zilizopo au Dira
ambayo imejiwekea kama nchi, lakini katika Serikali ya Awamu ya Tano tunaona mnaongozwa
kwa kauli mbiu ya hapa kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mtanielewa tu! Nasema mnaongozwa kwa hapa kazi, bila kufuata Sheria zilizopo, Kanuni zilizopo, utaratibu uliopo na Katiba mliyojiwekea. Nasema haya kwa mifano nitakayoitoa; Rais anafukuza watumishi wa umma! Ni kweli kwamba kuna baadhi ya watumishi wa umma sio waaminifu na wana upungufu. Pia, ni kweli kwamba kuna baadhi ya watumishi wako kwenye mamlaka ya Rais, wale aliowateuwa anaweza kuwaondoa, lakini kuna wale ambao wameajiriwa, ni sharti taratibu na sheria za kiutumishi zifuatwe. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mfano mwingine; mmesema mnatoa elimu bure, mtapeleka takribani shilingi bilioni 18 kwa Halmashauri! Mnapeleka kwa bajeti ipi ambayo hatujapitisha ndani ya Bunge? Bunge la Kumi, tulipitisha Bajeti, ni lini mmeleta Supplementary Budget ndani
ya Bunge, ili mtekeleze hili? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mfano mwingine, Rais alifuta sherehe za Uhuru! Ni kweli kwamba katika Bunge la Kumi kati ya mambo ambayo Upinzani tulikuwa tunapigia kelele, ni kufuta sherehe mbalimbali ambazo hazina tija, ni jambo jema. Amefuta sherehe za Uhuru akatoa agizo fedha zipelekwe kwenye ujenzi wa barabara ya Morocco; amefanya fedha hizo zimekwenda, taratibu za manunuzi, kutangaza tender, Sheria mliyojiwekea ya Manunuzi, mmefuata au mnasema tu hapa kazi? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine, kupitia vyombo vya habari, jana au juzi, Afisa mmoja wa Serikali amesema watapeleka shilingi milioni 50 kwa kila kijiji! Nawauliza kwa Bajeti ipi? Kwa Sheria ipi? Kwa Supplemantary Budget ipi mliyojiwekea? Au mnaongozwa tu kwa hapa
kazi, bila kufuata sheria zilizopo? Mtakuwa ni Serikali ya ajabu duniani kuongozwa na kauli mbiu badala ya sheria mlizojiwekea. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Hotuba ya Rais ameelezea kwa upana suala la amani na utulivu na mmekuwa mkijivunia amani na utulivu. Mnawaambia Watanzania kuna amani na utulivu, wakati hakuna demokrasia ndani ya nchi hii, demokrasia zinaminywa zinakanyagwa.
Kuna migogoro ya ardhi, wakulima na wafugaji, halafu mnasema amani na utulivu! Hakuna ajira kwa vijana, halafu mnasema amani na utulivu! Mahakama hazitoi haki kwa wakati, halafu mnasema amani na utulivu! Hospitalini hakuna dawa, kinamama wakienda kupata huduma
zipo mbali au wakati mwingine hazipatikani, mnasema amani na utulivu! Tumeona utumiaji wa nguvu za kidola wakati wa uchaguzi na baada ya uchaguzi, halafu mnasema amani na utulivu!
(Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, itafika mahali Watanzania hawatathubutu tena kuvumilia amani na utulivu wakati wana shida lukuki! Hakuna haki, watu wanakandamizwa, watu wananyanyaswa, halafu mnang‟ang‟ania kusema amani na utulivu! (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nimalizie machache kwa kusema katika Hotuba ya Mheshimiwa Rais, ameelezea hali ya kisiasa Zanzibar. Hili tunamwambia nalo ni jipu alitumbue, alifanyie kazi! Mshindi atangazwe! Si mmesema ninyi hapa kazi! Fuateni basi Sheria, Katiba na Taratibu mlizojiwekea. Mtangazeni mshindi wa Zanzibar, kwa nini mnaogopa? Mkiambiwa hili mnaogopaogopa na mnaanza kupiga-piga kelele, kuna nini kimejificha hapa? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tunataka suala la mgogoro wa kisiasa, kama amesema yeye atakuwa ni Rais wa kutumbua majibu basi atumbue na hili, Wazanzibari wapate haki yao waliyemchagua aweze kutangazwa. Ahsante. (Makofi)