Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Godbless Jonathan Lema

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Arusha Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. GODBLESS J. LEMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Katika Kitabu cha Mithali ambacho ameandika Mfalme Suleiman, hii ni sura ya 30 mstari wa 18 mpaka 19 anasema ifuatavyo: “Kuna mambo matatu yaliyo ya ajabu kwangu. Naam, kuna manne nisiyoyafahamu. Mwendo wa tai katika hewa, mwendo wa nyoka juu ya mwamba, mwendo wa merikebu katikati ya bahari na mwendo wa mtu pamoja na msichana.”
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mfalme Suleiman angekuwa anaandika, angeandika; “na utaratibu wa uchangiaji wa Wabunge wa Chama cha Mapinduzi.” Mnaikataa bajeti muda wote wa kuchangia, halafu mwisho mnaunga mkono hoja. Hili jambo pia lingemshangaza Suleiman. (Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa namwuliza Mheshimiwa Msigwa hapa, hivi sisi tukija upande huo na nyie mkaja upande huu, tukabadilishana Vyama lakini status quo ikabaki hivyo hivyo, mkabaki Mawaziri, Wabunge lakini mkawa CHADEMA na sisi CCM, mngeweza kubadilisha maisha ya Watanzania? Nikapata jibu msingeweza kwa sababu kimsingi tatizo siyo Chama chenu, ni akili zenu. Msingi kabisa, ni attitude. Attitude…
MHE. GODBLESS J. LEMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, basi attitude ni tusi, naliondoa hilo neno “attitude” kwasababu nyie mnasema ni tusi.
Mheshimiwa Mwenyekiti leo tunaongelea habari ya viwanda..
MHE. GODBLESS J. LEMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kinachopigiwa kelele hapa ni opportunity. Wabunge wote humu wa Upinzani na wa Chama Tawala, wanapigia kelele opportunities ambazo walipaswa kuzi-cease na ndiyo sababu nilipoanza na neno “attitude” mlipaswa kusubiri. Wabunge wote hapa…
MHE. GODBLESS J. LEMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nafuta neno “akili.”
MHE. GODBLESS J. LEMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la viwanda nchi hii na wala Serikali haiwezi kuleta viwanda vyote ambavyo vitaleta transformation katika Taifa hii. Ukienda nchi zote zilizoendelea, transformation ya viwanda imeletwa na private sector. Kwa hiyo, kama private sector ndiyo imeleta transformation ya viwanda, Waheshimiwa Wabunge wanaodai Serikali ya nchi hii lazima ilete viwanda, Wabunge wao ni lazima waanze kujua tofauti ya liability na Assets.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna Wabunge wanachaguliwa wapya. Anachaguliwa Mbunge mwezi wa Kumi; mwezi wa Kumi na Mbili ananunua gari ya shilingi milioni 400 halafu full back position ya kuendesha gari ile ni posho ya kikao. Tatizo hapa siyo kiwanda! Gari moja ya thamani ya shilingi milioni 400 ni viwanda nane China.
Kwa hiyo, tunapoongelea suala la transformation ya viwanda siyo Serikali peke yake, ni pamoja na transformation of the attitude. Wananchi kutoka kwenye negative mentality kwenda kwenye positive mentality na hiki ndicho nilikuwa nataka mwelewe. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, viwanda hivi mnavyosema hapa, havitakuja. Mtaonea Wizara hizi! Riba leo kwenye Commercial Bank ni asilimia 20 mpaka 22. Ukichukua shilingi bilioni moja Benki leo, utalipa riba ya shilingi milioni 220 kwa mwaka, maana yake ni takribani shilingi milioni 20 kila mwezi. Ndiyo sababu wananchi wengi ama watu wengi hawaingii katika mfumo wa investment, wanaenda katika mfumo wa buy and sell kwa sababu kununua kiwanda, kifike, ukijenge, kianze kufanya kazi upate leseni, ni jambo linachukua takribani zaidi ya mwaka mmoja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Benki zetu siyo rafiki na urafiki huu unaondoka kwa sababu base rate ya BOT ni asilimia 16, maana yake Benki zote zinaanza kuanzia asilimia 16 kupanda juu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, namna pekee ya kufanya transformation ya viwanda katika Taifa hili, ni lazima Wizara ya fedha na BOT waende wakashushe riba kwa watu ambao wanataka kufanya investment kwenye viwanda. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, investment ya Viwanda haiwezekani. Leo ukitaka kufungua Kiwanda, unahitaji kwenda kuchukua fedha Benki, utaenda kuweka property yako.
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo watu wengi wanakufa na pressure kwa sababu ya riba. Ili viwanda nchi hii vifanikiwe, nendeni mkaongee. Wizara ikaongee na Wizara ya Fedha na Benki Kuu. Riba ya viwanda lazima iwe tofauti na riba nyingine zote katika uwekezaji. Sasa attitude haitawakwaza tena. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti na Mheshimiwa Waziri, kuhusu General Tyre; niliwashauri kwenye Kamati, wakati General Tyre inajengwa pale palikuwa ni pori, leo General Tyre iko katikati ya residential, huku kuna nyumba za PPF, nyuma kuna mtaa wa Lolieni. Niliwaambia njooni tuongee na Halmashauri ya Jiji na mimi na-control lile Jiji, kila kitu ni mimi Kamati ya Mipango Miji ni mimi, Meya ni mimi kila kitu ni mimi. Kwa sababu mnataka shilingi bilioni 68 ili m-take off, mkija Arusha kuliko lile eneo muendelee kulazimisha kuweka kiwanda pale njooni tuwape heka 100 kilometa 20 kutoka Arusha Jiji na lile eneo muende mkatengeneze iwe ni commercial areas, mtengeneze proper residential.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mnawaza mkauza eneo la General Tyre kwa zaidi ya bilioni 30 ya Kitanzania, ikawa ni ubia wenu mkatafuta partner, lakini leo Mheshimiwa nakushauri ukifufua kiwanda cha General Tyre na mitambo iliyopo, tairi moja utauza shilingi milioni 10, ile mitambo ni mitambo ya siku nyingi, inatumia umeme mwingi na umeme wenyewe huu wa kusuasua, matairi yamebadilika, moulding zimebadilika. Leo kuna tairi za waya, pale kuna tairi za nyuzi, ni bora hiyo fedha mkaitumia kufanya research na analysis, mjue ni kitu gani mnataka kufanya kwenye kiwanda kile lengo siyo kufungua kiwanda, je, kiwanda kitakuwa effective? Lengo ni kiwanda kitakuwa effective.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri njoo Arusha tukubaliane tuwatafutie heka 100 nje ya Mji, tupeni lile eneo tuwatafutie shilingi bilioni 30, pale fedha iko! Lakini leo ukiweka kiwanda cha General Tyre pale na usitoe nje ya Mji pale ni residential, barabara ni nyembamba, unaingiaje kupeleka raw material? Unaingiaje kutoa raw material? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nakushauri sana Mheshimiwa Waziri ukitaka kuleta transformation kwa General Tyre lazima uchukue mwelekeo ninaokuambia mimi. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mishahara ya nchi hii ni midogo, hakuna purchasing power. Leo mtu kuingia supermarket ni prestige, leo mtu akionekana anaingia supermarket nchi hii ama akipanda ndege ni issue yaani leo kupanda ndege it’s a dream! Kwa hiyo, ili muweze kutengeneza viwanda na muweze kutengeneza wawekezaji waone kwamba nchi hii unaweza ukawekeza viwanda lazima kuwepo na purchasing power. Purchasing power, number one inakuwa created na mishahara ya Serikali pamoja na private sectors. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo ninaomba sana kwamba Serikali kama inataka kuona viwanda vinakuwepo katika Taifa hili ni lazima Serikali ifikirie kuongeza mishahara ya wafanyakazi. Lazima Serikali ifikirie kuongeza mishahara bora ya wafanyakazi ili kuwepo na purchasing power, siyo kupunguza kama ambavyo mnafikiria sasa, mtu wa shilingi milioni 30 apewe shilingi milioni 15. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Lukuvi hapa kila siku anafuta title na anatangaza! Mnafikiri mnasaidia nchi, msiwanyang‟anye watu ardhi mkatangaza. Mwekezaji mnayemuita kuja kuwekeza kwenye kiwanda halafu anasikia kuna mtu amenyang‟anywa heka 3,000 huyo mtu atarudia Dubai kama alikuwa ana-connect ndege. Msinyang‟anye watu ardhi. Hata kama mkinyang‟anya watu ardhi, imekaa muda mrefu msifanye publicity kwa sababu ina threat wawekezaji wanaotaka kuja kuwekeza. Huwezi kuwekeza kwenye viwanda kama huna ardhi. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo dakika tatu zilikuwa zimebaki kwa sababu ya zile kelele kelele.
MHE. GODBLESS J. LEMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu TRA. Wafanyabiashara wa nchi hii wakiwaona TRA wanawaogopa kama wameona Field Force. Ili wafanyabiashara wawe na malengo ya kufikiria maono makubwa ni lazima TRA ijenge attitude ya kuwa na urafiki na wafanyabiashara na siyo wakali kwa wafanyabiashara. Viwanda na Biashara ni Wizara ambayo imesambaa sana, kilimo kiko ndani yake, Wizara ya Fedha iko ndani yake, kila kitu. Lakini hawa ili waweze kufanikiwa lazima muwape nguvu zaidi ya kufanya connectivity na hizi Wizara nyingine kwa ajili ya harmonize shughuli zao za kila siku. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri wa Mazingira leo anaweza akatoka hapa ama Naibu Waziri wa Mazingira akaenda Tanga akafunga kiwanda kwa sababu tu anataka aonekane kwenye tv bila kum-consult Waziri wa Viwanda na Biashara