Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

Hon. Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

MHE. BENAYA L. KAPINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru awali ya yote niungane na wenzangu hasa Mbunge wa Jimbo la Mbozi kwa masikitiko makubwa kusema kwamba sisi wa mikoa ya Kusini hususani Jimbo la Mbinga tumesahaulika sana, wananchi wa Jimbo la Mbinga kwa muda mrefu tukitambua kwamba wao ndio wakulima wakubwa nchi hii,wazalishaji wakubwa wa mahindi wazalishaji wakubwa wa kahawa lakini pia sisi ni wachimbaji wa madini mmesikia habari za mpepo mpepai ni wachimbaji wa madini sasa hivi tunachimba makaa ya mawe lakini kwa muda mrefu sana sana Mbinga imetengwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ni hivi tu karibuni tumebahatika kupata barabara moja inayotoka Mbambabay inapitita Mbinga inaenda Songea sasa pale inagawika nyingine inaenda Mtwara na unaweza kuja makambako njombe na kuendelea kwa mara ya kwanza lakini tumesubiri tangu kupata uhuru nchi hii. Wananchi wa Mbinga ni watiifu sana katika nchi hii na tangu hapo hawajawahi teteleka wamebaki kuwa watiifu.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwezi wa kwanza niliuliza swali hapa kuhusiana na barabara ya kutoka Kitai hadi Lituhi, nikajibiwa hapa majibu vizuri sana, barabara hiyo tutuijenga kwa awamu kuanzia mwezi wa nne majibu yale wananchi wanayasikia nimeenda hivi karibuni hapa wananiuliza mbona kimya imekuwaje kwa bahati nzuri nimepata swali la nyongeza Bunge hili nikaambiwa wako kwenye utaratibu wa tenda tena sio kwa kiasi kidogo tunaitengeneza hii barabara yote kuanzia Kitai mpaka Lituhi ikipitia Rwanda Ndongosi, na maeneo mengine. Lakini sasa lini tunaanza kuitengeneza hii barabara ilikuwa mwezi wa nne hamna kitu hii ni mwezi wa tano tunaenda na humu kwenye bajeti nashukuru nimeona kidogo kwa nini nasema kidogo nimeona hii barabara ina kilometa 90. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini hapa nimeona bilioni 11 na milioni 500 lakini maelezo yanasema kuna vipande vipande vya kwenda kulipa madeni kumlipa mkandarasi aliyekamilisha barabara ile ya kutoka Mbinga Mbambabay sijui ni kiasi gani. Lakini inaenda kulipa kipande cha Namtumbo sijui ni kiasi gani inaenda kulipa tena kipande kingine kule juu Masasi sijui sasa najiuliza na nashangaa, ni kiasi gani kinaenda kujenga hizi kilometa 90. Mambo haya ni ya ukweli au ndio yaleyale tunayosema sisi wa kusini sasa tusubirie wenzetu wamalize kujengewa hizo barabara zao kwa kweli kwa mtindo huu naungana na Mbunge wa Mbozi tuko tayari kufanya kitu hapa ndani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, haiwezekani kwani sisi sio watanzania sisi ni watanzania tunalipa kodi na tunazalisha sana kwa nini tusijengewe na sisi barabara kama huko zinakofumuliwa hizo nyingine. Kwa hiyo, ndugu yangu Mbunge wa Mbozi mimi niko tayari kukuunga mkono kichwa miguu kila kitu tukubaliane hapa na sisi tujengewe barabara. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mwezi wa kwanza pia nimeuliza hapa swali Rais wa nchi hii alipokuwa anapita kuomba kura alitoa ahadi ya kujenga barabara kwa kiwango cha lami, kuanzia Mbinga kwenda Litembo. Litembo ndiko sisi tunakotibiwa kuna hospitali ya misheni kule miaka yote tangu uhuru ndio inayotusaidia sisi, namna ya kufika hapo Litembo ni shughuli kubwa. Naibu Waziri Engineer Kasekenya anafahamu lakini pia hata Naibu Waziri wa TAMISEMI nilienda nae mpaka Litembo alishika mikono kichwani kwamba ehh hivi mnapitajepitaje huku tulimpeleka hivyo kwa hiyo yale uliyosema kwamba tuwapeleke.

Mheshimiwa Naibu Spika, nilijaribu kumpeleka Naibu Waziri wa TAMISEMI Mheshimiwa Silinde, halishika mikono kichwani na tulimchangulia kinjia fulani cha kujipenyeza angalau lakini tungempitisha zile njia tunazopita sisi nadhani angemwambia dereva arudishe uongo, ukweli yule pale anasema kweli hali ni mbaya sana sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa bahati nzuri barabara ile kabla ya awamu hii alifika Rais wa Awamu ya Nne baada ya kuona matatizo kwenye ile barabara akatoa ahadi ya kujenga kwa kiwango cha nini cha lami. Miaka kumi ile imepita tumefika Awamu ya Tano ikatolewa ahadi imepita na bahati nzuri Awamu hii ilikuwa ya Tano imeingiliana hivi Rais wa sasa hivi ndiye aliyepita kule alienda akaja akatupa ahadi.


Mheshimiwa Naibu Spika, nimeuliza swali hapa majibu yale hayaeleweki mpaka sasa hivi sijui nitawaambia nini wananchi wa Mbinga kwamba lini ile barabara itaanza kujengwa na naomba sasa ile ni ahadi ya Rais wa nchi hii. Naomba kupata ufafanuzi lini ahadi ile inaenda kutelezwa ni pamoja na barabara ya kutoka Kigonsera kwenda hadi Matili lakini hiyo barabara inaenda mpaka Hinda kwa Mheshimiwa Eng. Stella Manyanya na yenyewe ipo hivyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, niliuliza swali hapa hiyo ni ahadi ya Rais kwamba tunakwenda kujenga barabara hizi kwa kiwango cha lami Mheshimiwa…

NAIBU SPIKA: Ahsante sana muda umeisha Mheshimiwa kengele imeshagonga.

MHE. BENAYA L. KAPINGA: Sio ya kwanza?

NAIBU SPIKA: Ni ya pili!

MHE. BENAYA L. KAPINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, basi kwa shida sana naunga mkono hoja. (Makofi)