Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Anthony Calist Komu

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. ANTHONY C. KOMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Nami nianze kuchangia hotuba ya Mheshimiwa Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa masikitiko kwamba kwa kweli ukiitazama hii hotuba yake kuanzia mwanzo mpaka mwisho pale anapokwenda kuomba pesa. Ukijiuliza kwamba ni kitu gani kimoja ambacho kitakuwa kimekamilika baada ya kwisha mwaka huu wa fedha ambao tunauzungumzia, hakuna hata kimoja kitakachokuwa kimekamilika kinachoweza kutupeleka kwenye uchumi wa viwanda na biashara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nawaomba sana Waheshimiwa Wabunge na Serikali kwamba tunapojadili haya mambo, tuwe serious kidogo. Tuangalie kwamba ni wapi tunataka kupeleka nchi hii? Kama ni suala la kujaribu kuwa masters wa kila kitu halafu mwisho wa siku tunajikuta kwamba we are master of none, kwa kweli tutakuwa tunawadanganya wananchi wetu. Hilo ndilo ninaloliona, kwa sababu tunasema kwa mfano tunataka kuwa na viwanda vya kimkakati. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunazungumza kwa miaka nenda rudi kuhusu Mchuchuma na chuma cha Liganga. Tunasema hivi ni viwanda vya kimkakati, lakini ukienda kuangalia fedha zilizotengwa ni kwa ajili ya kwenda kufidia ili watu wapishe maeneo yale kwa ajili ya ujenzi. Ni kwa ajili ya kukamilisha upembuzi yakinifu; lakini tunasema mwakani miezi mitatu ijayo tutaanza uzalishaji. Huu ni uongo! Haya ni maigizo! Hizi ni nyimbo! Sasa nyimbo za aina ya namna hii ni lazima tuachane nazo tuzungumze vitu ambavyo ni tangible, yaani vitu ambavyo vinashikika. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunasema kwamba hivi ni viwanda vya kimkakati, lakini share zetu sisi kwenye chuma cha Liganga na Mchuchuma tuna share 20. Sasa share 20 nafasi yetu ya ku-influence mambo kwenye hiyo miradi, iko wapi? Kwa hiyo, bado tunakwenda kucheza kwenye mikono ya wabia wetu ambao ndio watakaokuwa na influence. Kwa hiyo, hatuwezi kujidai kwamba hivi ni viwanda vya kimkakati wakati hatuna mkakati wowote wa kuhakikisha vinaanza, hatuna makakati wowote wa kuhakikisha kwamba, tunavimiliki ili tuwe na influence.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba sana, Waziri atakapokuja hapa atuambie ni mikakati gani ambayo ni tangible (inayoshikika), ambayo ni mahususi ya kutufanya kweli twende kumiliki hayo maeneo ambayo yanaitwa ni ya kimkakati na ni lini haya maeneo kweli kwa maana ya fedha kwa maana ya bajeti yanaweza yakaanza na tukaona hapa kweli tunapiga hatua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunazungumza kwenda kwenye uchumi wa kati, wakati huo huo tunazungumza habari ya kuwa na private sector yenye nguvu, lakini ukiangalia Serikali yetu ndiyo ambayo inajitahidi kwa nguvu zake zote kuua private sector. Ukienda kwenye deni la Taifa, unakuta tunadaiwa zaidi ya shilingi trilioni 29 sijui, kama sijakosea figures, lakini 1.3 trillion ni madeni ya ndani ambapo ni Wazabuni mbalimbali waliofanya kazi na Serikali, watumishi wa Serikali na Wakandarasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tunapokwenda kwenye huu uchumi wa kipato cha kati tunaenda na nani, kama Serikali kazi yake kubwa ni kuhakikisha kwamba hawa wazawa hawanyanyuki? Mwaka 2015 kuna Mhandishi mmoja alijiua kwa sababu kampuni yake ililemewa na madeni ya Ukandarasi, kwa sababu ya Kandarasi mbalimbali alizofanya kwenye Serikali, akajiua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba kuwe na affirmative action ya kuhakikisha kwamba tunawanyanyua wazawa. Ukienda kwenye ile sheria ya mwaka 2004 ya kuwezesha wazawa waweze kushiriki kwenye uchumi na yenyewe ina walakini mkubwa. Naona Waziri Muhongo hayuko hapa, lakini mwaka 2015 nafikiri kuna mtu mmoja alitaka kuwekeza kwenye gesi na ni mtu maarufu, Dkt. Regnald Mengi akaambiwa yeye level yake ni uchuuzi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka Mheshimiwa Waziri leo atuambie, ili uwe mzawa unayeweza kupewa hadhi ya kuwekeza kwenye vitu ambavyo siyo vya uchuuzi, unapaswa uwe na uchumi wa namna gani? Kwa sababu uchumi wa Mengi kwa jinsi tunavyojua, ni uchumi mkubwa. Kama ni fedha anaweza akawanazo nyingi; kama ni mali zisizohamishika ambazo zinaweza kuwekwa dhamana, anazo ambazo watu wanazifahamu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kama huyo anaambiwa kwamba ni mchuuzi, akachuuze, kwa vyovyote Watanzania walio wengi watakuwa wamekwazika sana na watakuwa wanaogopa kujitokeza kwa sababu watajipima, hivi mimi na Dkt. Regnald Mengi, naweza kwenda? Inawezekana ndiyo maana Mheshimiwa Waziri hapa kila siku anahamasisha watu wajitokeze, hawajitokezi kwa sababu havijatolewa vigezo vya Watanzania ili washiriki kwenye uwekezaji wanapashwa wawe na nguvu zinazofanana namna gani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Waziri na hili naweza nikashika mshahara wako kama hautokuja vizuri. Kwa sababu ni suala la kisera, utuambie ni uwezo wa namna gani unatakiwa ili Watanzania nao waweze kushiriki katika kuwekeza kwenye uchumi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni laxity ya Serikali ya CCM, yaani uzembe wa Serikali ya CCM na kutokufuatilia mambo kwa Serikali ya CCM. Kwa sababu tumeambiwa hapa viwanda vimekufa, lakini viwanda hivi vimekufa na Mheshimiwa Waziri ametuambia katika taarifa zake mbalimbali kutoka kwenye Kamati kwamba viwanda vingine vilitumika kama dhamana kukopa kwenye mabenki, lakini mikopo hiyo haikwenda kutumika kwa ajili ya kuendeleza viwanda, ilitumika kwenye vitu vingine, Serikali ilikuwa wapi? Serikali ilikuwa wapi wakati mtu anakopa fedha akasema anakwenda kufua kiwanda akaenda akafanya mambo mengine ya kwenda China akaenda kuchukua bidhaa kwa ajili ya uchuuzi? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nachelea kusema kwamba, kama tabia hii haitabadilika, kama mienendo ya namna hii haitabadilika, bado tutaendelea kupata matatizo kwa sababu hizi benki ambazo tunataka kuanzisha, zitaanzishwa, pesa zitawekwa kule, watakopa tena, kwa laxity hii hii ya Serikali za CCM, mambo yatakuwa yale yale, business as usual. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana tuangalie ni namna gani. Limezungumzwa suala la kulinda viwanda vya ndani, well and good, lakini unavyozungumza suala la kulinda viwanda vya ndani, usiangalie tu uagizaji wa bidhaa kutoka nje; jiulize vile vile ni kwa nini bidhaa za nje zinakuwa bei rahisi? Zinakuwa bei rahisi kwa sababu mazingira yetu ambayo kimsingi ni jukumu la Serikali kuyafanya yawe yanayofanya viwanda vya kwetu vizalishe bidhaa zinazoweza kushindana kibei, ni magumu. Watu wamechangia hapa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Meshimiwa Peter Surukamba asubuhi alizungumza akaorodhesha…
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.