Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

Hon. Aeshi Khalfan Hilaly

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumbawanga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

MHE. AESHI K. HILALY: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi hii ili na mimi nipate nafasi ya kuchangia katika hii bajeti ya Wizara ya miundombinu, kwanza naomba niipongeze sana Serikali ya Chama Cha Mapinduzi kwa kazi kubwa sana inayoifanya lakini la pili naomba nikipongeze Chama changu kwa ushindi mkubwa kwa Majimbo mawili kule Mkoani Kigoma, ambako kama Mbunge na Wabunge wenzangu tuliteuliwa kwenda kupambana kuhakikisha kwamba Majimbo yale mawili yanarudi kwa Chama Cha Mapinduzi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nina mambo kama matano hivi ambayo ningeomba sana Mheshimiwa Waziri akirudi ili niweze kupata majibu. Huu ni mwaka wangu wa nne nimekuwa hapa nikipitisha bajeti ya kujenga uwanja wa ndege napiga makofi ninawaambia wananchi kule Sumbawanga kwamba uwanja unajengwa na hatimaye mpaka leo uwanja wa ndege wa Sumbawanga haujawahi kujengwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu spika, nimeona kwenye bajeti mwaka huu tena kwamba tutajenga uwanja wa ndege mjini Sumbawanga sasa nilikuwa nataka nikuulize sisi tumekuwa tukipitisha bajeti kila siku na tunarudi kwa wananchi kule kuwaeleza kwamba tutajenga uwanja wa ndege muda fulani, leo ni mwaka wa nne ukienda kwenye Hansard kule utakuta tumepitisha bajeti na uwanja wa ndege haujawahi kujengwa na mwisho wa siku tumeshalipa fidia Mkandarasi yupo site tunaingia gharama lakini uwanja haujengwi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nikajaribu kuuliza nini tatizo kwanini uwanja wa ndege haujengwi? Nilichokijua mimi ni jambo la kushangaza viwanja vya ndege vile vinne au vitano pamoja na kiwanja cha Kigoma nafikiri na Tabora na maeneo mengine imekwamishwa kwa sababu ndogo sana viwanja vya ndege vinasimamiwa na mamlaka ya ndege Tanzania TIA lakini viwanja vinajengwa na TANROADS shida iliyopo kule wafadhili wamegoma kutoa fedha kwa sababu vilitakiwa viwanja vile visimamiwe na TIA na sio TANROADS kujenga viwanja vya ndege. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa ni jambo dogo mno kwanini tunavutana kwanini tusirudishe mamlaka ya viwanja vya ndege iende kwenye viwanja vya ndege TANROADS wajenge barabara kama kawaida. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nikuombe sana jambo hili limechukua miaka minne na nimuombe Waziri akija kutujibu hapa kabla sijapitisha bajeti yake nijue tunakwenda kujenga kweli moja kwa moja mwaka huu au na yenyewe itakuwa ni histori ya kupitisha bajeti kila siku kila siku na mwisho wa siku wananchi wanatuchoka, tumekuwa tukiwaambia tunajenga uwanja na hatuwezi kuujenga. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini la pili mimi Mjumbe wa Kamati ya miundombinu tumepata barabara ya Ntendo Muzye tulipata 0.9-kilometer hata kilometa moja haijafika kwenye bajeti hii nikamuuliza Waziri hivi kweli kumpata mkandarasi wa kuja kujenga 0.9 kilometa, hata kilometa moja haifiki utampata mkandarasi gani?

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini ninaomba nishukuru baada ya mavutano kidogo Serikali imetusikiliza na hatimaye niipongeze Wizara imetupa kilometa 25. Lakini bado hoja yangu ipo pale pale barabara ya Ntendo-Muzye ndio barabara kubwa ambayo inailisha Mkoa wa Rukwa pamoja na Mbeya kule na Tanzania kwa ujumla. Kilometa kutoka Ntendo kwenda Muzye ni kilometa 35 lakini ukipeleka kilometa 25 tutakuja kwenye utata ule ule wa kilometa 10 nani atazimalizia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niiombe Wizara na nimuombe Waziri wetu wa miundombinu atuongezee baada ya kutupa kilometa 25 atupe kilometa 35 ili tuweze kumaliza barabara ile barabara ile ni kero Mheshimiwa Rais anaijua, Mheshimiwa Waziri Mkuu anaijua na Mawaziri wote wanaopita pale kutoka Ntendo kwenda Muzye barabara ile haipitiki na watu wengi wanakufa. Lakini chakula chote kinatoka bondeni. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nilitaka niombe kwa sababu nimekaa na Mbunge mwenzangu anatoka Kwela lengo kubwa sisi Wabunge mtusaidie ili barabara ile iweze kujengwa kwa kiwango cha lami hizo kilometa 10 tuwaombe Wizara iweze kutuongezea ili tuweze kujenga. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo barabara ya kutoka Matai kwenda Kasesha ina kilometa 51 ukiwapa kilometa 35 tutabakia na kilometa 20 nyingine kwa hasara, na Sumbawanga ni mbali hivi barabara ndogo ndogo hizi au fupi fupi zinazoweza kujenga Dar es salaam ni rahisi zaidi kwasababu wakandarasi wapo karibu na maeneo ambayo wanayapata lakini ukitoa kilometa 25 kwa Sumbawanga kumpata mkandarasi kutoka maeneo mengine ni shinda kubwa mno. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri tunakuombe ili uweze kutusaidia, nazungumzia Bonde la Rukwa, bonde ambalo linakwenda mpaka Chunya mwisho wa siku linafika mpaka kule Mbeya barabara ile mbovu haipitiki, madaraja mabovu, nikuombe sana sisi tunaongea kama mkoa, mkoa wetu ulikuwa uko nyuma na sasa hivi umeanza kupiga hatua kubwa basi tunaomba Serikali na tumuombe Waziri aende akaangalie ile barabara ili iweze kupitika kwa kiwango cha lami. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niongelee standards gauge Wajumbe tulienda kutembelea reli ile iliyojengwa ya kisasa, nataka niseme nichukue nafasi hii kuipongeza sana Serikali, Wabunge wote Wajumbe wote waliofika maeneo yale waliridhika kabisa na utendaji mkubwa wa Serikali wa inavyosimamia mradi ule. Kwa kweli ukiwa nje hawa wananchi ambao labda hawajatembea maeneo yale mkienda kutembelea Waheshimiwa Wabunge ni miujiza kwakweli reli imejengwa vizuri na sisi tuipongeze Serikali iweze kufanya sasa mambo mengine ili tuweze
kukamilisha barabara hii ya Reli iweze kufika Tabora, Kigoma, na kwenda Mwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema haya nirudie tena kumuomba Waziri MV Liemba Lake Tanganyika ziwa kubwa lenye watu wengi lakini leo ni mwaka wa tano meli haitembei watu wanakufa kila siku watu wanaangamia lakini kila tukifika Bungeni tunaambiwa kuna bajeti mwaka huu tunajenga meli, mwaka huu tunatengeneza MV Liemba mwaka huu tunatengeneza MV Mwongozo hakuna meli hata moja iliyotengenezwa. Sasa mimi hoja yangu hapo ni kwamba tunapokuja kupitisha hizi bajeti na mwaka jana tumepitisha MV Liemba inajengwa mpaka leo haijaweza kukarabatiwa tufanye nini sisi Wabunge kwenda kuwaambia kule wananchi? Watupe majibu ili tukienda kule tuwaambie bwana hii meli tumeiondoa kwenye bajeti mpaka pale tutakapokuwa tumepata fedha ili tuweze kujenga meli. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kama hatuna fedha tusiweze kutoa ahadi humu ndani kama tutajenga meli wakati fedha hatuna, nimuombe sana Mheshimiwa Waziri mwaka huu, hiyo meli mpya sasa ikae pembeni tutengezeeni meli zetu zile ambazo tunazijua zianze kazi mpya itakuja baadaye. Lakini humu nimeona tuna Meli mpya mbili sijui tuna meli ya tani 3000 utapakia mzigo wa nani wa tani 300 Lake Tanganyika, kengele ya kwanza. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Ya pili Mheshimiwa ahsante sana.

MHE. AESHI K. HILALY: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.