Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

Hon. Tumaini Bryceson Magessa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

MHE. TUMAINI B. MAGESSA: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa nafasi hii ya kuweza kuchangia bajeti na hotuba ya Waziri wa Uchukuzi. Nimpongeze sana Waziri, Naibu Waziri na watendaji wote wa Wizara hii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimebahatika kufika Dar- es-Salaam na miji mingine midogomidogo ambayo


inaendelea kukua Tanzania. Naomba tu niishauri Serikali nimeona pale Dar-es-Salaam tukiendelea kujenga barabara kwa ajili ya kupitisha mabasi ya mwendokasi. Nina mashaka sana kwa ongezeko la watu wale tukiendelea ku-invest kwenye mabasi yale inawezekana tusifanikiwe sana tunatakiwa twende kwenye commuter train. Tuwe na train ya umeme ambayo itakuwa inachukua watu wengi badala ya kuondoka basi moja na watu 65 au watu 30.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, niishauri sana Serikali, iangalie pamoja na mipango iliyofanya katika miji yetu hii inayokua ianze kufikiria namna ya kuweka commuter trains ambazo ni za umeme ili ziweze kupeleka mabehewa
10. Tulifanya majaribio ya train pale inaitwa train ya Mwakyembe Dar-es-Salaam, ilikuwa inachukua watu wengi. Kwa hiyo, niseme wazi miji yote inayokua tuanze kwenda huko sasa tukiendelea tu kusema tutaendelea kuwa na barabara tutajikuta tunaingia carpets, carpets itakuwa constant, lakini operation cost ya kuendesha mabasi itakuwa kubwa na mwisho wa siku miradi hii itakuwa haiwezi kuizalishia nchi hii. (Makofi)


Mheshimiwa Naibu Spika, sasa niende kwenye barabara. Nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri ameonesha wazi kwamba, mpaka Aprili Serikali ilishachangia asilimia 67.2 ya bajeti ya maendeleo ambayo ilikuwa imetolewa na Serikali. Kwa hiyo, ukurasa namba tisa unatuthibitishia kwamba, Serikali imeshatoa pesa asilimia 67.2, lakini ukurasa namba 11 kwenye utekelezaji wa miradi hii kwenye asilimia 67 iliyotolewa inaonesha wazi kwamba, wametekeleza miradi iliyokamilika kwa asilimia 30 tu. Kwa hiyo, 67 ambayo imeingia imeweza kufanikiwa kufanya kazi ya asilimia 30 tu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna mahali hapa naona kabisa kutakuwa na shida ya usimamizi. Nilitegemea ilipoingia asilimia 67.2 tuone na miradi iliyokamilika iwe hata asilimia 50, sasa ni asilimia 30 ikionesha kabisa kuna hoja ya usimamizi hapa. Kwa hiyo, nimshauri Waziri, viongozi wetu walio kule ambao wanafanya kazi kwenye Serikali wahakikishe


kwamba, kile kinachoingia kwenye Wizara kinaweza kuwa kimetumika na wananchi wakaona mafanikio yake.

Mheshimiwa Naibu Spika, nihamie sasa jimboni kwangu. Kwenye Ilani ya Chama Cha Mapinduzi inaoneshwa wazi kwamba, kuna barabara inajengwa kutoka Geita kupita Bukoli – Bulyanhulu hadi Kahama, uchambuzi yakinifu umekwishafanyika. Niwapongeze Waheshimiwa Wabunge waliokuwa wanachangia asubuhi, walikuwa wanasema kuna uchambuzi yakinifu, kuna uchambuzi gani, kila aina ya uchambuzi umeshafanyika, lakini barabara hii bado haijajengwa na imewekewa loti tatu; kuna loti ya kwanza kilometa 54, kuna loti ya pili kilometa 61, loti ya tatu kilometa 64, lakini bado hakuna kinachokwenda.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kwa sababu mvua imenyesha sana, pamoja na kwamba, iko kwenye mpango wa kujengewa lami, sasa imeharibika sana kiasi ambacho haipitiki, wananchi wanapata shida kupita pale. Niombe sana kama mipango hii ya Serikali bado iko mbali basi hii periodic maintenance ifanyike, ili wananchi waendelee kuitumia katika viwango vya kawaida wakati tukisubiri lami hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimwombe sana Mheshimiwa Waziri, naamini barabara hii anaifahamu na ni barabara muhimu kwenye eneo letu la kutoka Geita kuja Kahama na badaye kuja Dar-es-Salaam. ina mapato ya kutosha, tujengewe barabara hii ili wananchi wale waweze kuona matunda ya uhuru wa nchi hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, TANROADS kwa kawaida wanatakiwa kusimamia barabara zetu nyingi kwa sababu, TARURA tumethibitisha ndani ya Bunge hili kwamba, Mfuko wao wa ujenzi wa barabara ni mdogo na bahati mbaya sana barabara nyingi ziko TARURA, za vijiji. Sasa napendekeza barabara zote ambazo zimefikia viwango vya kupandishwa hadhi kwa namna ya mgawanyo huu ambao unaendelea kuwepo kati ya TANROADS na TARURA basi zirudi kule ili zipate periodic maintenance ambayo inatambulika kwa sababu,


sasa hatutabiri tena. Mvua imenyesha barabara zote zimekatika, tukiuliza TANROADS anatengeneza? Hapana, sio ya TANROADS hii, ya TARURA hiyo kwa hiyo, haitatengenezwa msimu huo.

Mheshimiwa Naibu Spika, niombe sana Serikali iangalie, tunaomba mara nyingi kupandisha barabara zetu. Kwetu kule tuliomba barabara ya kutoka Katoro kupita Rwamgasa kupita Iseli kwenda mpaka Nyarugusu ipandishwe, wanasema vigezo bado havitoshi. Tumeomba barabara ya kutoka Katoro kupitia Igondo – Nyakamwaga kwenda Kamena, wanasema ni feeder roads bado vigezo haviridhishi. Hizi barabara zinakaa hadi miaka mitano bila kutengenezwa na hivyo zinakuwa hazipitiki.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na hilo ziko ambazo zinatengenezwa kwenye periodic maintenance. Tunazo barabara ya Chibingo kwenda Bukondo Port inatakiwa ifanyiwe periodic maintenance, haijafanyiwa, kwa hiyo, imeanza kuharibika sana na wananchi wanapata shida kupita pale. Vile vile tunayo barabara ya Mgusu kwenda port ya Nungwe kwenda ziwani nayo imeanza kuharibika bado haijafanyiwa periodic maintenance.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunayo pia barabara ya Katoro kwenda Ushirombo, imeanza kutengenezwa, lakini kasi yake ni ndogo. Ningeomba waongeze kasi sana ili wananchi wale sasa mvua hii inapopita barabara hizi ziendelee kupitika, kwa sababu ni feeder roads ambazo zikikatika tunashindwa kufanya zozote katika jimbo letu.

Mheshimiwa Naibu Spika, niseme kama walivyosema wenzangu, kuna mipango mingi sana na watu wanasema pesa hazitoshi, lakini naamini kama Serikali imechangia tulichopanga mwaka jana asilimia 67, halafu sasa bado tunasema leo tuna mwezi mmoja bado mbele, kama itachangia asilimia 10 tutakwenda kwenye asilimia 77. 77, lazima ioneshe kitu ambacho kinaonekana kimetengezwa kwa asilimia 77, lakini utekelezaji wetu kama nilivyosema mwanzo ni asilimia 30.


Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, niombe sana usimamizi kwa maana ya viongozi walioko kwenye wilaya zetu, walioko kwenye mikoa yetu wasimamie vizuri kuhakikisha kwamba miradi hii inakamilika. Ikiwezekana kama tutapata pesa asilimia 70 basi asilimia 70 iwe imefanyika.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya maneno haya, naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)