Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

Hon. Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi


MHE. FELISTA D. NJAU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii nami nichangie kwenye wizara hii muhimu. Ninapozungumzia kwenye ujenzi na uchukuzi moja kwa moja tunaelekeza kwenye mambo ya miundombinu kama barabara, reli na vitu vinginevyo. Katika sekta hii, imeonesha kukua mfululizo ndani ya miaka minne, imekuwa ikikuwa kwa asilimia 14.4 tangu 2016/2017, 2020/2021. Hii sekta inakua bila kigugumizi pamoja na janga la corona lakini imeiongezea Nchi pato la Taifa asilimia 14.8. Hii ni sekta ya pili kwa kuongezea Nchi pato la Taifa ukitoka kilimo lakini kwa kukua imeibuka kinara sekta hii ni muhimu inahitaji jicho la tatu kwa mustakabali wa Taifa na maendeleo ya mwananchi mmoja mmoja. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaposema hivi ninaona kuna changamoto chache ambazo tunaweza tukizimaliza hii sekta inayoenda kukua na kuwa kinara na pato la Taifa litakuwa zaidi na mwananchi mmoja mmoja ataweza kumiliki uchumi. Nikisema hivyo, ninaweza kusema wakandarasi walioingia mkataba, wakandarasi waliosajiriwa kwenye nchi yetu asilimia 10 tu ndio wageni kwa nchi za nje, asilimia 10. Asilimia nyingine ni wazawa lakini ukifanya upembuzi pale unakuta asilimia 60 ya miradi mikubwa inashikiliwa na asilimia 10 ya wakandarasi wageni. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunashindwa kuwa wazalendo kwasababu Wakandarasi wetu hawakidhi vigezo, kigezo cha kwanza hawana mitaji, hawana mitaji mizuri kwahiyo hawawezi ku-afford kuweza kushika hii miradi mikubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kingine hawana ujuzi wa kutosha, hawana ujuzi wa kutosha kwa hiyo mwisho wa siku tunatakiwa tukae chini tuweze kuwawezesha wakandarasi wetu wawe na ujuzi wa kutosha ili kuweza ku- afford ushindani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kingine ni vifaa vya ujenzi havikai kwenye level moja bei zake zinapanda na kushuka na sometimes hazipo kabisa. Kwa hiyo, mwisho wa siku hawa wataalam wetu wanashindwa kwenda kwenye ushindani wa wakandarasi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninapoongea haya ninasema kwasababu Wakandarasi wetu wakiweza kushika hizi tenda uchumi wa mtu mmoja mmoja ndani ya nchi yetu utakua, lakini pato la Taifa litaongeza kwa sababu watu wetu watakkuwa na fedha mfukoni. Niishauri Serikali katika hili, tunavyoona namna hii tuweze kuwawezesha Wakandarasi wetu waweze kumiliki hii miradi mikubwa ili tuweze kuona matunda. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini ninapotoka mahali hapo, ninaona kabisa barabara nyingi, vilio vingi vya Wabunge humu ndani wanalia juu ya barabara, hawatoki kwenye reli wanaingia kwenye reli ya barabara kwa sababu ndio kero inayomgusa mwananchi wa kawaida kule chini vijijini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara zinazounganisha mikoa kwa mfano barabara zinazounganisha mikoa kuja Dar es Salaam, barabara hizi ni mbovu za mikoa ya kimkakati mikoa ya kilimo. Mikoa ya Njombe, ya Iringa, Mikoa ya Singida barabara hii si salama kwa hiyo wananchi wa kawaida hawawezi kuleta mazao yao Dar es Salaam. Wakifika Dar es Salaam wanakutana na adha nyingine ya mafuriko, Dar es Salaam miundombinu ya mafuriko hakuna mifereji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati wanatengeneza mkakati huo wa barabara waangalie mifereji kwasababu maji haya ya mifereji yamekuwa ndio chanzo cha kukata barabara katika Mkoa wa Dar es Salaam. Lakini mafuriko ukifika Jangwani eneo lile la mkutano kuelekea Kariakoo pale hapapitiki wakati wa mvua ni kwa sababu hakuna miundombinu ya mifereji ambayo ni imara. Ukija barabara ya Tegeta kuelekea Bunju, Boko, Basihaya mifereji hakuna barabara zimejengwa zipo vizuri lakini unakuta magari yame- stuck hayawezi kutembea kwa sababu maji yanajaa barabarani, barabara zinakatika kuisababishia Serikali kupata hasara. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tuone namna gani bora wakati tunapokwenda kuweka miundombinu ya barabara tuona namna bora ya kutengeneza mifereji. Jiji la Dar es Salaam halina miundombinu rafiki, ukiangalia Jiji la Dar es Salaam watu wanasema kuna lami lakini ni asilimia 14 tu ya Jiji la Dar es Salaam wananchi wake wameunganishwa kwenye maji machafu, maji taka asilimia 14. Asilimia nyingine tunachanganyika na maji hayo hayo tunakunywa, magonjwa ya mlipuko Dar es Salaam, wanaotoka mikoani wanakutana nayo, basi ni vurugu tupu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niiombe Serikali, wanajua Mheshimiwa Waziri na Mheshimiwa Naibu Waziri mnajua, miundombinu ya Dar es Salaam si rafiki kila siku watu wanaugua vipindupindu, wanaugua UTI, wanaugua magonjwa kadha wa kadha kwasababu tu ya miundombinu, lakini sio adha nyingine. Niombe kwa sababu ni kitovu cha biashara, twende tukaitengeneze Dar es Salaam na mikoa yake inayounganishwa kuja Dar es Salaam ili tuweze kuimarisha uchumi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ninavyoongea hapa kuna wananchi wangu wa Ununio hawana pa kukaa, barabara hazina mifereji, watu wapo pembezoni wamekaa wametulia hawana pa kwenda mbele wala kurudi nyuma, nyuma zinaelea. Ni Dar es Salaam hapo sio mikoani.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nikiangalia kiini naona ni mitaro niiombe Serikali chonde chonde kipindi kilichopita niliongelea juu ya mitaro pale Nyamachabisi alikuja waziri kipindi kile nafikiri waziri wangu anafahamu. Alikuja kipindi kile Nyamachabisi miundombinu ya mitaro hakuna watu wanaelea. Niombe, niombe Serikali hii ya Mama Samia Suluhu Serikali Sikivu na Mawaziri wake waweze kuweka mikakati mizuri ili wananchi waweze kufanya biashara zao. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ninavyoongelea miundombinu, ninaongelea viwanda huwezi kuwa na viwanda imara kama huna miundombinu. Ninavyoongelea mbiundombinu ninaongelea kilimo, huwezi kuuza mazao yako ya kilimo kama huna miundombinu. ninapoongelea hiyo miundombinu naongelea uwekezaji, wawekezaji wanaanglia miundombinu ndio wanakuja kwenye nchi yetu. Naomba kuwasilisha, ahsante sana. (Makofi)