Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017- Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. Deogratias Francis Ngalawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017- Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

MHE. DEOGRATIAS F. NGALAWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kupata nafasi ya kuzungumza na kuchangia hoja ya Wizara ya Viwanda. Kwanza nampongeza Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuchaguliwa kwa kishindo na Mawaziri wote kwa namna nzuri wanavyofanya kazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, hoja yangu inajikita zaidi kwenye maeneo ya biashara. Hoja ya nchi kutaka kwenda kwenye viwanda ni nzuri, lakini kitu ambacho nakuwa na wasiwasi nacho ni namna ya utekelezaji wa hoja zetu. Ninavyojua, suala la viwanda ni mtambuka, sasa sijajua kwamba Serikali imejiandaaje katika kuhakikisha kwamba inawaandaa Watanzania katika mapokeo hayo. Ki-mind set Watanzania bado hawajawa tayari kwenye hilo, hivyo wanahitaji training ya namna gani ya kuweza kuipokea.
Mheshimiwa Naibu Spika, leo hii tunapozungumza, tuna wafanyabiashara wengi sana ambao wako informal na kundi hili la wafanyabiashara ni kubwa. Asilimia 70 ya wafanyabiashara wote wa Tanzania wako kwenye kundi ambalo ni la informal. Kwa hiyo, bado Serikali haijafanya mchakato mzuri wa kuhakikisha kwamba tunawaandaa wafanyabiashara wetu ili mwisho wa siku waweze ku-formalise biashara zao.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kwa nini hizi biashara ziko informal? Ziko informal kwa sababu sheria haziko friendly. Tuna kundi kubwa la wafanyabiashara ambao wanashindwa ku-formalize biashara zao kwa sababu ya usajili; namna ya kuzisajili zile biashara inakuwa ni ngumu; na namna ya kupata leseni inakuwa ni ngumu. Leo hii tunaambiwa TIN number ni bure lakini ukijaribu kuangalia na kwenda, kupata hizo TIN number kwa ajili ya kufanyia hizo biashara, zile TIN number zina usumbufu sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, leo hii unaambiwa, unapotaka kuanza kufanya biashara zako ni lazima kwanza utoe kiwango fulani cha hela hata kabla hiyo biashara hujaifanya. Sasa lile linawasumbua sana wafanyabiashara wetu mpaka inafikia kipindi kwamba anaamua acha afanye biashara kiholela, Serikali inakosa kodi na watu wanaweza wakafanya biashara nje ya mfumo sahihi. Nadhani umefika wakati sasa tuendeshe training na ikiwezekana hawa watu wetu tuwatengenezee namna ya kujua fursa za biashara zilizopo na ikiwezekana tupate elimu nzuri ya namna hawa watu wetu watafanya biashara.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye eneo la elimu ya ujasiriamali na fursa za biashara bado tuko nyuma. Kuna fursa nyingi ambazo vijana wetu na watu wetu wanazo na wanatakiwa kuzifanya, lakini hawajawa exposed. Nadhani ifike wakati sasa Serikali ifanye hatua za makusudi kuendesha training kwenye vijiji, kwenye mitaa, ili mwisho wa siku watu wajue ni vitu gani wanaweza kufanya. Kwa sababu fursa zipo zinawazunguka, lakini watu hawajui wafanye nini na mbinu gani watumie. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, leo hii tuna Maafisa Biashara kwenye Manispaa zetu, kuna Maafisa Biashara kwenye Halmashauri zetu, lakini tukijaribu kuwauliza Mpango Kazi wao ni upi? Walio wengi wala hawajui. Waulize Maafisa Biashara kwenye Halmashauri zetu, kuna wafanyabiashara wangapi ndani ya Halmashauri? Hawezi kukupa takwimu. Kwa hiyo, hili nalo ni tatizo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ifike mahali Serikali lazima itambue ina wafanyabiashara wangapi? Hata tunapozungumza kwamba kuna mfumo ule PPP maana yake nini? Kwa sababu kuna watu wengine hawajui. Kwa hiyo, kwa kufanya hivyo, maana yake kwanza tutawatambua wafanyabiashara na mwisho wa siku ni kwamba hata unapoamua kupanga kodi, unapanga kodi kwa watu ambao unawafahamu.
Mheshimiwa Naibu Spika, nizungumzie suala la viwanda. Kwenye hotuba yako Mheshimiwa Waziri, ukurasa wa 52, umezungumzia mradi wa kasi mpya wa kuzalisha chuma ghafi. Mara nyingi huwa napata shida, pale unapozunguza kwamba utatekelezwa halafu usiseme utatekelezwa lini.
Mheshimiwa Naibu Spika, leo hii ndiyo tupo kwenye bajeti ya kwanza ya utekelezaji wa miaka mitano kwa Serikali ya Awamu ya Tano. Naamini unapozungumza mradi, lazima uwe na mahali pa kuanzia na mahali ambapo panatakiwa kuishia. Kwa sababu ukiileta statement too general unakuwa hujatupa tool ya sisi kuku-assess wewe, kwa sababu hata mwakani tukija, utasema hivi hivi, kwamba mradi huu utatekelezwa na Kampuni ya Maganga Matitu Resources Development. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani ifike mahali sasa unapozungumza mradi, hata kama utataka kuutekeleza mwaka 2018, mentioned, kwamba mradi huu utatekelezwa muda fulani na unatarajia labda kwisha muda fulani, hivyo tutakwenda vizuri. Kitu chochote unachokiita ni project lazima kiwe na mwanzo na lazima kiwe na mwisho. That is a project. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini statement zisiwe too general. Leo hii unasema unatekeleza mradi wa makaa ya mawe Mchuchuma kuendeleza utekelezaji wa mradi unganishi wa makaa ya mawe Mchuchuma na chuma cha Liganga, kwenye ukurasa wako wa 161. Chuma cha Liganga tumeshaanza kukisikia toka 1906, kwa hiyo, ni kabla hatujazaliwa na inawezekana hata kabla babu zetu wengine hawajazaliwa. Kwa hiyo, ifike kipindi sasa Serikali iseme, wakati tunauliza swali hili kwenye Wizara ya Madini walituambia kwamba fidia itaanza kulipwa mwezi Juni, mwaka 2016 na mradi utaanza mwezi Machi, 2017.
Mheshimiwa Naibu Spika, nilikuwa natarajia kwenye ripoti ya Mheshimiwa Waziri wa Viwanda ange-mention hii kitu, kwamba mradi wa makaa ya mawe Mchuchuma na chuma cha Liganga utaanza Machi, 2017 kama swali lilivyokuwa limejibiwa na Naibu Waziri wa Nishati na Madini ili tuwe tunakwenda kwa takwimu. Kwa sababu usipotoa takwimu na muda (time frame) maana yake hatutaweza kuku-assess na kuku- pin.
MHE. DEOGRATIAS F. NGALAWA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu hii Serikali tumeshazungumza kwamba ni Serikali ya viwanda na tunatarajia kwamba tutaenda kwa kasi kubwa. Natamani kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri, aseme kinaga ubaga, kwamba tutaanza muda fulani ili tutakapokuja hapa mwakani tuwe na maswali ya kumuuliza. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine, hivi viwanda vya kimkakati kwa sababu ameshasema ni National Flagship Project, haitakiwi kuwa na majibu general. Leo hii watu hawajaandaliwa kwa maana hii miradi itahitaji support. Licha ya ukubwa wa hivi viwanda vinavyokuja kule, nilikuwa natarajia kwamba Mheshimiwa Waziri angesema, kwa sababu makaa ya mawe Mchuchuma na Chuma cha Liganga inaanza, kutakuwa na vitu vya ku-support patakuwa na SIDO; hawa watu tuwaandalie uwezo wa kiufundi ili mwisho wa siku waweze kuji-engage kwenye zile bidhaa au kazi zitakazofanyika na hiyo miradi mikubwa inayokuja. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, leo hii tunavyozungumza hakuna barabara ya lami inayoelekea huko. Wimbo huu umekuwa ukiimbwa muda mrefu na hata marehemu Mheshimiwa Deo Filikunjombe alikuwa akiizungumzia kwa kasi sana hii kitu. Mungu amlaze mahali pema peponi. Haijafanyiwa kitu chochote! Kwa hiyo, tuombe kwamba hivi vitu vingine lazima viwe na support ya sekta nyingine ili kuhakikisha kwamba hili gurudumu linakwenda. (Makofi)
MHE. DEOGRATIAS F NGALAWA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuunga mkono hoja.