Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maji

Hon. Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maji

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Spika, awali ya yote nichukuwe nafasi hii kwanza kukushukuru wewe mwenyewe binafsi na niseme tu niendelee kukutia moyo niseme uendelee kufanya kazi ukiamini Wabunge wengi wako nyumba yako wala usiwe na hofu na yoyote yanayoendelea mtaani au kwenye mitandao ya kijamii, tuko nyuma yako na tunaelewa nini unafanya kwa wakati huu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini kwa kuchangia wizara hii nichukuwe nafasi kumshukuru Mheshimiwa Waziri wa Maji Wizara nzima pamoja na wadendaji wa RUWASA, mheshimiwa Waziri pongezi zote tunazokupa tunakupa kwasababu unatimu nzuri kwa maana ya wizara nzima yenyewe namna ilivyofanya kuanzia Katibu Mkuu na watumishi wote, lakini na RUWASA kwa utekelezaji mzuri wanaoufanya hasa pale unapokuwa unapokuwa umetoa maagizo.

Mheshimiwa Spika, nichukuwe nafasi hii kukushukuru binafsi kwa miradi mbalimbali ambayo umenisaidia, mradi wa Shilati niliwahi kusema ulikuwa na Zaidi ya miaka 15 hauna maji, umefanya Ziara ya siku moja ukatamka neno hivi ninavyozungumza tayari wananchi wale wana maji, nikuombe sasa kwa sehemu iliyosalia ulimalizie fedha walioomba milioni 300 ili angalau maji yaweze kusambaa ndani ya kata yote, lakini ikibidi na kata vijiji jirani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini ukuhishia hapo uliweza kunisaidia pia kwenye vijiji vingine kwa mfano kijiji cha Mwame, Kata ya Komuge, umenisaidia Nyarombo, umenisaidia Sudi, umenisaidia Nyehara na vijiji vingine, niendelee kusema kwa namna unavyokwenda sisi vijana tunafarijika sana. Sasa niseme tu usife moyo, ninachoweza kushauri kwa miaka hii inayokwenda ili angalau tuendelee sisi kukuunga mkono na kwenda na wewe sambamba nitakuwa na ushauri kwa maeneo matatu.

Mheshimiwa Spika, moja nikuombe sana Mheshimiwa Waziri jitahidi sana kuboresha RUWASA kwa maana wakala ya maji vijijini, na katika kuboresha huko wajengee uwezo ili waweze kupata watumishi wa kutosha kwa sababu nilikuwa najaribu kuangalia hotuba yako, kwenye fedha za maelendeleo peke yake maji vijijini Tanzania nzima umetenga Zaidi ya bilioni 360, kwa Mkoa wangu wa Mara umeniwekea Zaidi ya bilioni 21, tazama halmashauri peke yangu Serikali ya Chama cha Mapinduzi chini yako umenipa Zaidi ya bilioni
5.3 ambayo inatakiwa itekelezwe kwa mwaka mmoja wa bajeti.

Mheshimiwa Spika, lakini fedha yote hii kama kuna mtumishi mmoja tu ndani ya halmshauri kwa maana ndiyo engineer utaona namna gani fedha bilioni 35.3 inakwenda kusimamiwa na mtumishi mmoja ambaye inakwenda kusimamiwa na mtumishi mmoja ambaye unaweza kusema ni engineer wa wilaya. Kesho yake naamini, Mheshimiwa Waziri kama usipo wapa uwezo hawa watu wakuongeza watumishi utapita kwenye ziara yawezekana huyu asiwe na wakati mzuri. Niombe sana tuwajengee uwezo watu wa RUWASA ili waweze kuongeza watumishi wa kutosha waweze kukusaidia kusimamia fedha hizi nyingi ambazo mmezitenga kwa ajili kwenye upande wa maendeleo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pili nikuombe sana fedha hizi ambazo zimetengwa ziende kwa wakati kwasababu leo nitaondoka naenda kusema na ninasema kwa uwazi kabisa kwamba Mheshimiwa Waziri kupitia Serikali ya Chama cha Mapinduzi chini ya Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan wilaya yangu imepata bilioni 5.3 kwa ajili ya miradi ya maji, ikienda kwa wakati na ikafika sahihi hautakuwa na ugomvi wowote na Mamlaka za usimamizi wa Maji kote hata hao watu wa RUWASA, kwasababu zitakuwa zinakwenda kwa wakati na wanatimiza yale ambayo wananchi wanahitaji haya mawili, Mheshimiwa Waziri ukiyasimamia vizuri ni Imani yangu, pongezi zote wanazozitoa ndani ya Bunge hili utaendelea kupata kwa miaka yote, kwasababu utawajengea uwezo miradi itakwenda kwa usahihi na kwa muda ambao umepangwa, niamini sana niendelee kukuomba sana fedha hizi ambazo zimetenga, hasa Wizara ya Fedha.

Mheshimiwa Spika, niombe sana Wizara ya Fedha kwa kushirikiana na Wizara ya Maji fedha hizi mtusaidie sana ambazo zimetengwa kwenye bajeti hii tutengeneze historia kwa mara ya kwanza kwa fedha zinazotengwa kwa ajili ya miradi ya maji kwenda yote kwa asilimia 100 hasa kwenye miradi ya maji hasa mkizingatia Rais Mheshimiwa Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan ni mama ambaye kimsingi na yeye angetamani wamama wote ndani na vijiji vyote ambao kimsingi wanateseka sana na kero ya maji kwa miaka hii michache waweze kuondokana na kero hii ningeshukuru sana kama haya na hii bajeti tuliyoitenga itakwenda kwa wakati. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la pili, nizungumzie sana hii miji 28. Mheshimiwa Waziri nikupongeza sana mwanzoni ilikuwa inazungumzwa 16 lakini leo ndani ya Bunge hili unazungumzia miji 28. Nikuombe usipunguze hata mji mmoja, nenda nayo miji 28 kama ilivyosema kwa sababu tayari ndani ya Bunge hili tunaondoka tukijua miji 28 inakwenda kupata maji ya uhakika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ndani ya jimbo langu nina vijiji 87 lakini vijiji vyenye maji ni 12 peke yake. Vijiji ambavyo vina miradi ni 23; vijiji 52 ndani ya jimbo langu havina mradi wowote wa maji safi na salama. Kwa hiyo, mradi huu wa miji 28 leo hii ukipitisha bomba lile linalotoka Rorya kwenda Tarime maana yake zaidi ya kata 11 zinakwenda kunufanika na mradi huu. Ndiyo mradi ambao sisi watu wa Rorya tunategemea kwa muda mfupi utakuwa umetatua kero kubwa na kwa eneo kubwa. Coverage ya mradi huu ni kubwa sana kuliko hata ukichimba kisima kimoja kimoja kwenye kila Kijiji. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwenye huu mradi wa miji hii, naomba Waziri uipe kipaumbele sana hasa Rorya na Tarime. Watu wa Tarime hawana ziwa, ili wapate maji wanategemea maji ya Ziwa Victoria ambayo kimsingi yanatokea Rorya, Kijiji cha Nyamagaro. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri ukisimamia hili ni imani yangu kwa muda mfupi ndani ya miji hii miradi ya maji itakuwa mizuri na utakuwa umetatua kero kwa asilimia kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la mwisho, Waziri amesema kuna watu wanapita kukagua miradi iliyotekelezewa na Serikali kwa miaka mitano iliyopita kwa kutumia wakandarasi na inawezekana wasiwe wakandarasi lakini fedha zilizokwenda kwa ajili ya miradi ya maji haikutumika sawasawa. Naomba Waziri atilie mkazo suala hili kwa sababu kama fedha zinaendelea kwenda kulekule ambako hakujatengenezwa mfumo mzuri wa kusimamia miradi hii na kuna fedha ilikwenda haikutumika inavyotakiwa maana yake hata hii inayopelekwa yawezekana isitumike vizuri. Naomba sana ukamilishe suala hili ili kila kitu kiende sawasawa.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa.

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana na naunga mkono hoja. (Makofi)