Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Riziki Saidi Lulida

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. RIZIKI S.LULIDA: Mheshimiwa Spika, awali ya yote, nakushukuru na namshukuru Mwenyezi Mungu aliyenijalia kupata afya njema.
Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile nashukuru kwa hoja iliyowekwa mezani, ni nzuri, lakini namwonea huruma sana shangazi yangu Mheshimiwa Mwijage kuwa atapambana na kazi kubwa sana katika suala la viwanda. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, na-declare Interest, mimi ni Mjumbe katika Kamati ya Uwekezaji. Nimeangalia Uwekezaji na Ubinafsishaji wa Mashirika ya Umma na Taasisi zake kama ni mwiba unaoitafuna nchi hii. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tumeingia katika uwekezaji tukikurupuka, mikataba mibovu, usimamizi mbovu, corruption ndiyo imesimama. Leo tuna Taasisi zaidi ya 200 katika uwekezaji, lakini mpaka sasa hivi ni mashirika machache sana ambayo yanaweza yakatoa faida katika nchi hii. Taasisi hizo naweza nikazitaja ambazo angalau zimeonesha zinaweza zikatupeleka mbele katika dira ya maendeleo ya uwekezaji. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, moja, ni TANAPA. Inapeleka ruzuku katika pato la Taifa; Ngorogoro inatoa Ruzuku katika pato la Taifa; National Housing Corporation inatoa ruzuku katika pato la Taifa na NSSF. Sasa tujiulize, Taasisi nyingine zinategemea ruzuku kutoka Serikalini, kulikuwa na haja gani ya kubinafsisha wakati bado wanakula fedha ya Serikali na zinaingia katika mashirika yao? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuangalia Taasisi nyingi tulizokuwa nazo, hazina Bodi. Bodi ni dira, sasa kama Shirika halina Bodi unategemea nani ataendesha usukani wa Shirika lile? Nani atasimamia matumizi katika shirika lile? Kwa nini tumekaa na mashirika kwa muda mrefu yakiwa hayana Bodi? Nataka nipate majibu katika Taasisi zote kwa nini hazina Bodi? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tumeangalia Taasisi nyingi hazina Business Plan, uliingiaje katika mkataba wa ubinafisishaji na uwekezaji hakuna Business Plan? Matokeo yake unakuta mashirika ambayo hayahusiki na ujenzi wa majumba, sasa hivi wanakimbilia kujenga majengo. Sasa National Housing ipo, NSSF ipo, kwa nini unajenga nyumba sasa hivi? Ni kutokuwa na mwelekeo wa Business Plan yake; sivyo inavyokwenda! (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tunaingia katika suala la Mashirika mbalimbali ambayo tumeangalia. Katika kuyaangalia kwa kweli unapata huruma! Mashirika mengi yana uwezo mdogo wa Watendaji, inaonekana hawana capacity ya kuliongoza Shirika. Kwa nini umempa taasisi mtu ambaye hana uwezo? Matokeo yake, yale mashirika haya-perform. Kama hamjafanya kazi ya kuangalia nani ana-perform, nani ha-perform ina maana tutaendelea kuwa na business as usual. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nilizungumzie Shirika la TANESCO. Shirika la TANESCO wameingia wawekezaji wakubwa, mmojawapo IPTL, Songas, Symbion, wako pale kulila lile shirika. Tufikie mahali tujiulize, nani aliweka ule mkataba mbovu mpaka kufikia hili shirika lisiweze ku-perfom? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, itakuwa kila mwaka; mkataba wa Songas unasikitisha, anasema, mimi nimechukua mkopo, hivyo sitarudisha mkopo ule niliochukuwa Tanzania mpaka kwanza TANESCO anilipe. Bei anayotoa na ya kununulia ni vitu viwili tofauti. Anatoa Dola 13, huyu analipa Dola 21; jamani ni mkataba gani huu? Mnampa mkataba huu mpaka 2020/2025 toka alipoanzia, hana ruhusa ya kuguswa. Jamani, Watanzania tunajipenda hatujipendi! (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tuna huruma na nchi yetu au hatuna huruma na nchi yetu?
Mheshimiwa Naibu Spika, nakuja katika Bodi ya Sukari. Bodi ya Sukari imekaa pale tu kama bodi lakini haina meno, kazi inafanywa na Wizara. Wizara ndiyo wanatoa vibali vibovu vyote vya sukari. Sukari inaandikwa inakwenda nje ya nchi, kumbe inauzwa Tanzania hapa hapa, sukari inaletwa kama malighafi, siyo malighafi, iko katika viwanda. Wanachofanya, inatembea karatasi, sukari ikishateremshwa karatasi inapita katika vituo vyote kama Lorry hii imepita na sukari mpaka inafika Tunduma, lakini sukari iko bado mjini hapa! Kwa faida ya nani? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tujiulize na sisi Watendaji ambao Watanzania wote wamekosa uzalendo, ndiyo maana wenzetu Kenya wanatupita au Rwanda wanatupita; uzalendo wa Watendaji ni mdogo sana! (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nakuja katika upande wa viwanda. Mikoa ya Lindi, Mtwara na Pwani tulikuwa na Viwanda vya Korosho 13, vile viwanda vyote vimefungwa. Matokeo yake, kama Mkoa wa Lindi, hatuna ajira kwa viwanda hivyo. Hata kiwanda kimoja Lindi hamna! Unategemea wale Wamachinga watakwenda wapi? Wakija Dar es Salaam wanafukuzwa! Lindi viwanda mmevifunga, wanakwenda wapi?
Mheshimiwa Naibu Spika, ile korosho sasa, ule ndiyo mwiba, amepewa sura pana ananunua korosho vijijini sasa hivi! Wanapewa kununua ufuta vijijini! Hivi jamani panya umemwingiza kwenye ghala, unategemea nini? Ufuta sasa hivi hauna bei maalum, ufuta umelimwa vya kutosha, lakini sasa hivi unaambiwa sh. 1,300/= ukienda hapa sh. 2,000/=. Matokeo yake hata soko la ufuta hakuna! Tunategemea kuletewa mafuta mabovu kutoka nje! Hivi jamani mnaziona cancer zilizojaa Tanzania? Magonjwa ya figo mnayaona yalivyojaa Tanzania? Tunakula mafuta machafu, ufuta wetu tunaupeleka nje ya nchi. Tujiulize, tuna vision? Tuna mission? Are we responsible? We are not responsible. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tumefikia mahali tuko business as usual. Naomba tuambiwe, ule ufuta ambao umezalishwa, maana yake sasa hivi Tanzania ni nchi ya pili kuuza ufuta duniani, lakini tunaagiza mafuta kutoka nje; kwa sababu gani tunakula mafuta mabovu? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa nini mnatuendeleza mpaka leo tunakula mafuta machafu wakati tuna ufuta, karanga, pamba na alizeti; ni kwa sababu gani mnatufanyia mambo kama haya? Mko serious? Hamko serious, mmekaa kuangalia corruption, nitapata bei kiasi gani, nitapata fedha kiasi gani, basi! (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, masikitiko yangu makubwa, naangalia vijana ambao wanayumba yumba. Hizi korosho zinapelekwa nje kama raw material, tunapeleka ajira nje! Wanafanya makusudi kuhakikisha Mtanzania hapati ajira katika nchi hii. Wakiwa na viwanda vyao, Mtanzania hana nafasi! Ufuta wetu ambao ni bora, korosho zetu zilizokuwa bora, pamba tunapeleka nje ili kutoa ajira nje. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka majibu, Mheshimiwa Waziri atakapokuja kumalizia aniambie, ajira ya vijana kwa viwanda mlivyofunga itapatikana lini? Tujiwekee time frame kwa vile viwanda vilivyofungwa vya Mtwara, Masasi, Nachingwea, Lindi na Kibaha vitafunguliwa lini ili tuone kweli makucha yapo? Kama havijafunguliwa, mwakani nitauliza tena swali hili hili! Vijana wanazurura, wanahangaika!
Mheshimiwa Naibu Spika, nilikwenda Nachingwea, tulikuwa katika msafara wa viongozi, maghala yale ndani mna mbao mpaka juu. Jiulize, yeye amepewa kiwanda kwa ajili ya korosho, zile mbao zinafanya kazi gani? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Viwanda vya Urafiki; tumekwenda Urafiki vile viwanda ndani kumejaa ma-pampers na vitu vingine. Je, tuna vision na biashara zetu? Business Plan zetu zinasema nini? Yule wa Kiwanda cha Urafiki alikuwa atengeneze nguo, amejaza na viwanda; amechukuliwa hatua gani? Tunataka tujue, hatua gani amechukuliwa? Kama hatujajua amechukuliwa hatua gani, itakuwa ni watu ambao wanaachwa. Anakamatwa na pembe, mnaambiwa, bwana, hajui Kiswahili, ndiyo maana yake tunavyofanya sasa hivi! (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, viwanda vyetu havina thamani, vimekuwa maghala, watu wanaweka vitu vingine; hivyo kilichowekwa pale siyo. Tunataka tujue Action Plan, Business Plan zetu zinakwendaje? Tupo kwa kujenga au tupo kuwaachia wageni na uwekezaji wao uwe wa kutubomoa? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, nawashukuruni sana.