Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Taska Restituta Mbogo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. TASKA R. MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwanza kabisa napenda nimpongeza Mheshimiwa Profesa Ndalichako kwa kazi nzuri sana aliyoifanya kwenye Wizara hii ya Elimu. Mchango wangu unaenda moja kwa moja kwenye lugha ya kufundishia, siamini kwamba watoto wakifundishwa Kiswahili wataelewa Zaidi, kwa sababu hata mimi nilijifundishwa kwa lugha ya Kiswahili, nimesoma masomo kutoka darasa la kwanza mpka darasa la saba kwa Kiswahili. Nikaenda Sekondari ya Loleza nikapambana na Kiingereza. Nikasoma geography kwa Kiingereza, history kwa Kiingereza, hesabu kwa Kiingereza, chemistry kwa Kiingereza, biology kwa Kiingereza na masomo mengine yote kwa Kiingereza na tuliweza kufanya hivyo tukaweza kufaulu mitihani. Hoja yangu ni kwamba tuangalie tatizo ni nini, lugha sio tatizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, naamini kwamba tusije tukawandanganya Watanzania tukasema kwamba wakifundishwa kwa Kiswahili ndio wataelewa wakati watoto wetu tunawasomesha kwenye english medium, hiyo itakuwa ni dhambi kubwa sana tumeifanya. Naamini Wabunge humu ndani watoto wao wanasoma kwenye zile shule zilizoanzishwa sasa hivi za English medium, sasa tukianza kujenga hoja hapa kwamba watoto wafundishwe kwa Kiswahili tutakuwa tunawakosea sana Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nafikiri hoja muhimu ni kuangalia tatizo nini, kwa nini wanafunzi hawelewi darasani, lakini tatizo sio lugha. Je, utakuwa unajenga Taifa gani ambalo litakuwa linafundisha lugha moja ya Kiswahili, naamini kwamba lugha ni biashara, lugha ni mtaji na lugha ni elimu. Nasema lugha ni mtaji kwa nini, lugha ni mtaji kwa sababu unapojua lugha nyingi unajua Kifaransa, Kispaniola na Kiingereza, ina maana una-command lugha, hata unapoitwa kwenye interview utakuwa unaenda kujieleza vizuri. Kwa maana kwamba unaweza ukaenda kwenye zile nchi, ukafanya kazi, lakini kama wewe umekaa na lugha moja ina maana huna exposure, huwezi kwenda kufanya kazi hizo nchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo mawazo yangu, ningependa kwanza Mheshimiwa Ndalichako aongeze lugha; lugha nyingi zifundishwe mashuleni kama Kifaransa, Kispaniora na Kiingereza kiwekewe mkazo ili watoto wawe na confidence wanapoitwa kwenye International Organizations, wasiingiwe na ile inferiority complex, wanaanza can you explain yourself, anaanza ho ho ho badala ya kueleza my name is so and so.

Mheshimiwa Naibu Spika, lugha pia ni biashara, mfano unakwenda china unajua Kichina, ina maana wewe uta-bargain biashara za kule China. Kwa hiyo hoja yangu ni kwamba shule ziongezewe lugha za kufundishia, lugha ziwe nyingi, sio lugha moja tu ya Kiswahili.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la pili ambalo ningependa kulizungumza leo ni vitendea kazi kwenye shule zetu za msingi pamoja na sekondari, lakini hasa za msingi. Ningeomba Mheshimiwa Profesa Ndalichako, Waziri wa Elimu awasiliane na Wizara ya Maliasili na Utalii. Kuna misitu mingi sana hasa kule kwenye Bwawa la Nyerere ambako kunajengwa umeme kule Stigler’s Gorge, ile miti inayokata wanatengeneza mbao.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimwombe Mheshimiwa Waziri awasiliane nao, apate zile mbao ili ziweze kutengeneza madawati kwa sababu wanasafisha pale kwenye lile bwawa, kwa hiyo ile miti wanatengeneza mbao lakini zile mbao wanaziuza. Namwomba awasiliane na Wizara ya Maliasili ili mbao ziweze kupatikana madawati yaweze kutengeneza kwa wingi na watoto wetu wasiweze kukaa chini na hapo tutakuwa tumeienzi falsafa ya Hayati Dkt. John Pombe Magufuli ya elimu bure kwa kila Mtanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nafasi bado ipo nilipenda kuzungumzia pia mfumo wa elimu. Mheshimiwa Ndalichako itakuwa ni vizuri sana kwa sababu amesema anakwenda kurekebisha mfumo, tunaomba kwa sababu kulikuwa na kujichanganya hapa katikakati 2015 to 2020, alikuwa amesema watoto watasoma kuanzia darasa la kwanza mpaka darasa la 12 ndio watakuwa wamehitimu, lakini baadaye akaja akarudisha kwenye ile sera zamani tuliyosoma sisi la kwanza mpaka la saba, halafu kwenda sekondari, itakuwa ni vizuri sana aki-review hii sera ya elimu ili tujue Tanzania sera yake elimu ni ipi.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine la mwisho ambalo ningependa kuzungumzia kama muda upo…

Mheshimiwa Naibu Spika, basi nimeona umewasha kipaza sauti, hivyo naunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)