Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Dr. Alfred James Kimea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. DKT. ALFRED J. KIMEA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii nichangie kwenye hii bajeti ya Wizara ya Elimu. Nina mambo machache sana ya kuchangia kwenye Wizara hii na napenda nijikite hasa kwenye elimu ya juu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kati ya changamoto ambazo zimetolewa imeonekana tuna upungufu wa Wakufunzi au Wahadhiri katika vyuo vyetu, lakini tuangalie ni nini kinasababisha kitu hiki? Kama tunafahamu vyuo vyetu vina tendency ya ku-retain wanafunzi waliofanya vizuri wabaki kufundisha wanafnzi wetu, lakini pia kufanya research ambazo zinasaidia kutatua changamoto zinazopatikana kwenye jamii zetu. Ili mwanafunzi awe retained pale chuoni ni lazima wawe ni wanafunzi wanaofanya vizuri, First Classes ndio zinabakizwa vyuoni. First Class hizi hazihitajiki chuoni tu peke yake, pia mashirika mbalimbali yanatafuta watu hawa. Kwa hiyo, maslahi ya wanaobakishwa pale chuoni ndio yanayosababisha aidha mwanafunzi huyo au wanafunzi hao wazuri wakubali kubaki chuoni au waende sehemu nyingine.

Mheshimiwa Naibu Spika, hapa niishauri Serikali, ione namna ya kuboresha maslahi kwa wataalam wetu hawa ambao wana kazi kubwa ya kufanya research, wana kazi kubwa ya kufundisha wanafunzi wetu vyuoni, ili waweze kuwa na morali ya kubaki vyuoni kuliko kwenda kuajiriwa sehemu nyingine. Huo ndio mchango wangu wa kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, naongea hili kwa kuwa nina uzoefu na nilikuwa miongoni mwa watu hao, labda kwanza naomba ku-declare interest. Nadhani unafahamu ugumu wa kupanda madaraja kwenye vyuo vyetu, tunaajiriwa mara nyingi kutoka vyuoni kama Tutorial Assistant, baada ya kupata Masters tunaenda kuwa Assistant Lecturer na baada ya hapo tunakuwa ma-lecturer aidha kwa ku-publish baada ya kukaa miaka mitatu au kupata Ph.D.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo,watu hawa wanaweza wa-qualify. Mtu amehangaika sana aka-publish au kapata Ph.D anapanda cheo kwa kuandikiwa tu barua umepanda, lakini wanasema tunasubiri Serikali itoe idhini ya kupandishwa vyeo ili mpewe maslahi yenu. Hii inakatisha moyo wakufunzi wetu, inasababisha watu waondoke vyuoni; tunasema Wahadhiri ni wachache, lakini Serikali ndio inasababisha. Kwa kweli, hii ni sehemu nyeti sana, tunaomba maslahi ya watu hao yaangaliwe. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mfano ni wa kwangu mimi mwenyewe, kabla ya kwenda kufanya PhD nili-publish ili niweze kupanda kuwa Lecturer kabla ya kwenda PhD. Nilipewa tu barua ya pongezi kwamba, nime-qualify kuwa Lecturer, lakini hadi leo sijawahi kupata mshahara wa mtu kama Lecturer. Kwa hiyo, nasema wapo wenzangu wengi huko vyuoni wana changamoto kama ya kwangu, naomba tuangaliwe. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kingine, tunajua mazingira ya kusoma hapa Tanzania. Najua unaweza kuwa unafahamu watu ambao wamefanya Ph.D zao hapa Tanzania, kuna changamoto kubwa, lakini changamoto hii inasababishwa na maslahi mabovu ya wasimamizi wa Ph.D zile. Lecturer hana kipato kizuri, inasababisha aanze kutafuta shughuli nyingine za kumuingizia kipato. Utakuta lecturer anafundisha part time vyuo vinne, utakuta lecturer anafuga kuku ili kujiongezea kipato, anaacha kusimamia dissertation za wanafunzi. Kwa hiyo, kama tunataka kupandisha elimu ya vyuo vyetu, basi tuangalie maslahi ya watu hawa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sio hilo tu, pia vyuo vyetu havina fund kwa ajili ya kuendesha research. Sio research tu, ili uweze kutoa watu wa masters na PhD lazima vyuo viwe vime-subscribe kwenye journal nzuri za kimataifa, viwe vina software kwa ajili ya data analysis, lakini vyuo havipatiwi fedha hizi. Kwa hiyo, tunaomba Serikali ivipatie fedha vyuo vyetu ili elimu iweze kukua, hasa research ambazo zinahitajika kwa ajili ya maendeleo ya Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, cha mwisho, naomba Wizara ya Elimu inisikilize kwa makini; kulikuwa kuna institute hapa Tanzania inaitwa African Institute for Mathematical Science. Institute hii ipo South Afrika, Ghana, Tanzania na Rwanda, lakini institute hii inafadhiliwa na wafadhili (Donors) kwa asilimia kubwa na nchi ambayo hii institute ipo nchi hiyo inatoa kiasi kidogo kwa ajili ya uendeshaji wa chuo hicho, lakini Serikali yetu imeshindwa kulipia fedha kidogo kwa ajili ya kuendesha institute hiyo na institute hiyo imekufa. Namwomba Waziri kwenye majumuisho yake aje aniambie kimetokea kitu gani kwa institute hii mpaka kufa?

Mheshimiwa Naibu Spika, institute hii inasaidia researcher wetu, institute hii inasaidia wataalam wetu kuweza kufundishwa jinsi ya ku-apply mathematics kwenye kutatua matatizo kwenye jamii zetu. Imefanya vizuri sana Rwanda na inaendelea kufanya vizuri, imefanya vizuri Ghana na inaendelea kufanya vizuri, Tanzania kuna nini?

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii. Huo ndio ulikuwa mchango wangu. (Makofi)