Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Santiel Eric Kirumba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA: Mheshimiwa Spika, awali ya yote ningependa kukushukuru kwa kunipa nafasi hii. Ningependa kumpongeza Waziri wa Elimu kwa jinsi anavyofanya kazi yake vizuri, ni mama ambaye anajitoa sana kwenye hii kazi na hata ukimuita kwenye Kamati yoyote ni mwepesi kuhudhuria. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini matatizo yanayowakabili wanafunzi hayana tofauti sana na matatizo ambayo yanawakabili walimu. Walimu unakuta kwa mfano natokea Jimbo la Msalala, Kata ya Bulyankulu walimu ni wachache. Walimu wana changamoto nyingi, wakitoka kazini wanaenda kuchota maji, kule unaweza ukakuta walimu wale labda wakang’atwa na nyoka. Kingine napenda kusema kwamba walimu hawa wamekuwa wakipitia changamoto nyingi sana apart from sisi Wabunge kuwasemea na watu wengine kuwasemea, walimu hawa wana chama chao. Chama chao hiki kimekuwa sio msaada kwa walimu kabisa, walimu wanakatwa asilimia mbili katika mishahara yao kila mwezi lakini mwalimu hata akipata ajali hawezi kusaidia na chama chake. Zaidi kwamba anaonekana atatibiwa na Bima ya Afya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, walimu hawa nimechukua tu kwa ratio ya kawida, walimu 5,000 Tanzania hii ambao wanakatwa shilingi 25,000 kwa mwezi wabachangia milioni 125,000. Kwa mwaka chama cha UWT kwa walimu 5,000 kipanata bilioni 1.5 lakini mwalimu anapostaafu chama hiki kinampa mabati. Kweli kwa miaka yote anayochangia ni kweli anastahili mwalimu kupewa mabati? Tufike mahali sisi wenyewe tunawafanya hawa walimu wanashindwa ku-perform katika kazi zao vizuri. Chama hiki wanalazimishwa automatically kujiunga lakini katika ya CWT inamwambia kwamba mwalimu kujiunga ni hiari yake lakini automatically wanashirikiana na utumishi kuwafanya walimu hawa kuingia na kuwakata hiyo asilimia mbili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ninachoomba Serikali chini ya Wizara ya Elimu, walimu wasilazimishwe kujiunga na hiki chama kwasababu sio msaada kwao. Walimu wana changamoto nyingi lakini CWT haiwasemei chochote zaidi ya kukusanya. CWT ina mabenki, lakini walimu hawanufaiki. Wana kila hela wanazochukua, mahesabu yao hayako wazi. Sijawahi kusikia CWT inatoa mwongozo wowote kwamba mapato na matumizi yaliyotumika mwaka huu yako hivi.

Mheshimiwa Spika, naomba the way CAG anavyopambana na watu wengine naomba sasahivi akaifanyie kazi CWT. Kwasababu haiwezekani walimu wanateseka kiasi hiki, CWT iko kimya! Kuna walimu wamefukuzwa vyeti feki, CWT ni chama tu kilitakiwa kiwape hata washirika wake pesa zozote hata kile kifuta jasho kwa ambao wamefukuzwa lakini CWT imekaa kimya! (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba kwa kweli Waziri wa Elimu hiki chama kifutwe kwasababu walimu wengi wanakuambia hakina manufaa, wanalalamika. Elfu 25,000 kwa mwalimu mmoja kwa mwaka ni 200,000. Mimi kule ninapotoka chumba mwalimu ni shilingi 10,000 kwa hiyo hii kodi ya karibu mwaka mzima.

SPIKA: Mheshimiwa Santiel, kwa hiyo unataka walimu wasiwe na chama.

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA: Mheshimiwa Spika, wajiunge kwa hiari lakini sio kwa kulazimisha kwasababu walimu nao wana changamoto. Nakupa mfano kuna mwalimu Shinyanga alipata ajali, chama kama chama anachangia, kweli leo ukistaafu upewe bati mbili na shughuli zote hizi unazowafanyia wananchi wako? Bundle mbili za bati kweli ni sawa? Tuongee kwa hali halisi. Mwalimu anachangia, ni walimu wangapi wamechangia? Kwa nini hiki chama hakiko wazi? Waache watu wajiunge kwa hiari sio kuwalazimisha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, walimu nao wana haki sidhani hapa kama sisi Wabunge tungelazimishwa kuchangia hela…

SPIKA: Mheshimiwa Santiel kuna mambo mengi inabidi ujifunze bado. (Kicheko)

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA: Mheshimiwa Spika, sijakataa lakini naangalia. Nimechukua changamoto ambazo walimu wanapitia…

SPIKA: Nafikiri hilo siku moja ulinyanyue kwenye Kamati ya Chama upate elimu kidogo ya mambo haya yakoje na nini. Kuna haja ya ku-improve kama kuna improvements lakini ukisema kufuta sasa wabakie empty ndiyo watakuwa wamekwenda, wamerudi nyuma hatua 100? Lakini kama kuna areas of improvement, ndiyo kazi yetu Wabunge lakini kwamba kundi la wafanyakazi wasiwe na, yaani does it… ila kama kuna mapungufu ni areas za ku-improve.

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA: Mheshimiwa Spika, samahani… hoja yangu ilikuwa…

SPIKA: Mheshimiwa waziri ulisimama, Waziri wa Nchi.

T A A R I F A

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Spika, nilikuwa tu nataka kusaidia kwenye eneo hilo kwamba sisi ni wanachama wa Shirika la Kazi Duniani (ILO) na tumesharidhia mikataba na katika mikataba tuliyoridhia iko mikataba ambayo inatutaka tutoe uhuru wa majadiliano kwa wafanyakazi. Uhuru wa majadiliano ndiyo unaojenga uwepo wa vyama vya wafanyakazi kwenye maeneo ya kazi. Na wajibu wa vyama vya wafanyakazi ni kuhakikisha kwamba wao wanakuwa ni daraja la mahusiano kati ya mwajiri na wafanyakazi.

Mheshimiwa Spika, sasa nilichokuwa nataka kukisema hapa ni kwamba CWT iko kwa mujibu wa sheria na taratibu za vyama vya wafanyakazi nchini. Kwa hiyo, kama kuna walimu wanaona kuna matatizo kwa kuzingatia Katiba waliyonayo na miongozo inayoongoza uwepo wa vyama vya wafanyakasi wana fursa na nafasi ya kufanya majadiliano kwa kupitia utaratibu ambao umewekwa kisheria na wakafikia muafaka na vyama hivyo vikaendelea kuwepo. Uwepo wa vyama vya wafanyakazi ni muhimu sana kwenye maeneo ya ajira kuliko kitu kingine chochote. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo ni ushauri tu kama Taarifa. Niseme kwamba, kama yako matatizo iko fursa ya majadiliano na huo ndiyo msingi wa kisheria na sheria za kazi na ajira zinaweka msingi huo wa majadiliano ya pamoja.

SPIKA: Ndiyo maana nikasema Mheshimiwa Santiel kwamba bado kuna mengi ya kujifunza kwa sababu hawa wako kila Wilaya. Kila jimbo mlipo wapo CWT na wanafanya kazi pale na Mkurugenzi ambaye ndiyo mwajiri wa walimu katika wilaya ile. Ule uonevu wote n.k wanafanya kazi huko huko kimya kimya.

Mkitaka hicho chama kiwe ni cha kupiga kelele mtatoka jasho hasa ninyi Chama Tawala. Kumbuka kundi la walimu ndiyo kundi kubwa kuliko kundi lolote lile la wafanyakazi. Kwa hiyo, hawa watu wanaofanya kazi kubwa ambayo ninyi wengine hamuijui mkafikiri kwamba zawadi yao ni kupigwa tu humu ndani n.k ndiyo maana nikasema there is a lot to learn sometimes. Bado una dakika mbili au ziliisha? Wanasema moja lakini nakuongeza ya pili.

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA: Mheshimiwa Spika, kikubwa nilichokuwa naomba kwasababu kuna Tume ya Utumishi wa Walimu, lakini ninachoomba walimu kwenye chama hiki wasilazimishwe kujiunga. Wajiunge kwa hiari kwasababu Katiba yao inawaambia kwamba watumishi hawa wajiunge kwa hiari na sio kama hivi inavyopitia kwa utumishi kwamba automatically anakuwa amejiunga. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimepitia kuwauliza walimu wengi, ni kweli wanakwambia hawajawahi kuandika barua yoyote ya kujiunga kwa hiyo inaenda automatically, kwasababu Katiba ipo…

SPIKA: Si umeshaambiwa ni sheria?

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA: … mimi naomba kwamba…

SPIKA: Sasa kaa chini!

Uwe unaelewa. Ukiona unakwenda mahali unatafuta kaa na Waheshimiwa Mawaziri n.k upate elimu Mheshimiwa Santiel.